Déjà Vu inathibitisha binadamu tulishawahi kuishi maisha tunayoishi leo tangia kale

Pole sana mkuu..wewe una ugonjwa wa akili (psychosis ) wahi ukatibiwe..
Deja vu ni scenario ya kawaida kwa wagonjwa..

Kama unahisi uliwahi kuishi zamani unafikiri zamani hio hoteli ilikuwepo??
Ungesema labda uliona mabanda ya nyasi hapo ningekuelewa lakini kusema uliona hotel ya kisasa kabisa halafu useme ni past life yako huo ni ugonjwa...

Pole sana mkuu na get well soon

Kila mtu ana ugonjwa wa akili tatizo ni kuutambua
 
This is one of those things unaongea unahisi you are super smart kumbe umeenda chaka mbaya.
Deja-vu doesn't prove anything, umekuja na hypothesis yako ambayo huwezi prove in any scientific way au hata any physical way possible, itaishia kua hivyo "maneno"
 
Perfect analysis!

But unajua Duniani tunaishi kwenye dunia mbili at the same time...this physical world and spiritual world.. Yaani dunia tunayoiona na Dunia tusiyoiona ndio maana kuna majini na viumbe kadhaa visivyoonekana vinavyoishi Duniani na at the same tunaishi na sisi humu humu but hatuvioni ila vyenyewe vinaweza kutuona sababu viko rohoni.

Sasa kuna possibility tukifa tunaendelea kuexist spiritually in this world for hundreds of years to come, maana hapa Duniani kuna spiritual being kibao wanaishi for so many years. Wengine hadi wanatuonea donge tunavyogegeda kimwili na wanatuingia na kutupangia nani tumgegede na nani tusimgegede kwa manufaa yao. Refers majini na roho wengine.
Kwahiyo wewe sasa hivi ukitembea na bibi au babu wa miaka 70 inakua si wewe uliyegegeda ni maroho ndio yamegegeda?
 
Kuna mambo mengi binadamu huwa tunaota na yanatokea kweli. Kuna ndugu yetu mmoja yeye alikua anapandisha mizimu ya babu zake, siku moja mizimu ilisema kuwa mambi mengi yanayotokea maishani mwetu huwa tumeshaonyeshwa ndotoni lakini huwa tunapuuzia ndoto tunazoota. Mimi kama kuna jambo baya linataka kunitokea jicho la kulia huwa linacheza kwa muda mrefu sana hata miezi, na kama kuna jambo jema basi jicho la kushoto hucheza sana.
 
Kuna kipindi nilikuwa naota ndoto kuwa kuna sehemu ina majimaji na majanimajani halafu pembeni ya hayo majani kuna vyoo viwili na kimoja kina pazia ila kimoja hakina.
Hii ndoto ilikuwa inajirudia kwa mwezi mara moja. Na wala sikuwa naitilia maanani.

Basi ndoto ikakata na nikaendelea na maisha yangu.
Sasa siku moja nimeenda kumtembelea rafiki yangu maeneo ya Kipawa, tukaingia sehemu kula na akasema tutembee mwa mguu kwenda kwangu.
Ile tumepiga hatua kama kumi nageuka pembeni nikaona vyoo viwili, kimoja hakina pazia na kimoja kina pazia na hivo vyoo viko sehemu kama ina majimaji na majanimajani.
Yaani yale mazingira niliyoyaona ni sawasawa na ndoto niliyokuwa naipata kwa miezi karibu 3.
Palepale nikamwambia yule rafiki yangu, asante kwa kunipitisha njia hii....ndoto niliyokuwa naiota leo nimeiona.
Nilisimama kama dk 10 nashangaa yale ninayoyaona.
Hadi yule rafiki yangu akawa ananishangaa.

Haya mambo kweli yapo...na mimi ni shahidi.
Kweli yapo.
mkuu hiyo ni angelic massage ,malaika wako kuna ujumbe anataka kukwambia lakini kutokana na state zenu tofauti anashindwa ,ni kama wewe uwe kanisani halafu unataka mwambia askofu hajafunga zipu ,utaishia kuonesha ishara tu ,wapo watu huiona namba fulani kila mahali unaamka asubuhi unaina 07:20 ukielekea kazini linakuovertake gari T720BGA Ununua kifurushi kinagoma kucheki salio ni Tshs 720.00 ,ukiwapelekea watu wa angelic massaga interpretation wanatable wanakuchana na hiyo inamaana yake usikute hapo pana madini au dawa ya gonjwa lako sugu etc
 
me sio mara moja wala mara mbili huwa najikuta natokea katika mazingira ambayo nishawah kuwepo siku za nyuma ila nakua sikumbuki lile eneo nilfka mda gan but kumbuku znakuepo kabisa kama nilfka na nikafanya kile kile ambacho nakifanya mda huo au kumuona mtu aliyevalia nguo sawa na mtu niliyewah kumuona nyuma na akifanya kitu kile kile kama cha yule wa nyuma sa hua nabaki najiulza ni nini kinachopelekea hdi hali ile kutokea au kama mleta mada ulvo sema au tushawahi kuishi kabla ya kuzaliwa...!!!?
 
Kuna kitu nmejiuliza wakati nasoma hii kitu, kumbukumbu hutuzwa katika sehemu gani!? (ubongo au nafsi),naomba mnisaidie maana nachanganyikiwa hapa
 
Kuna kits kinaitwa 'time paradox' wengi time tunaifaham kama kitu chenye sehemu tatu, past,present na future. Lakini Huo sio ukweli wote kuhusiana na time, walau kwenye 3D, ni kweli ila kwenye hyper dimension si kweli. Time kwenye hyper dimension haiku a past, wala present wala future, kuna 'NOW', ambapo hapo kwenye now, wewe ndiyo unazaliwa,unakufa,unaowa au kuolewa unaanza chekechea ndiyo unspoken master yako nk vyote vinafanyika NOW.
Waikato mwingine tunaziakses hizo nukta zap NOW, hasa tukilala kwenye kill tunachoita ndoto nk, wakati mwingine kwa baadhi ya watu wanazicross hizo line za NOW wakiwa wako full awake lakini kwa muda mchache sana .
Tunapo zi access hizo point tukiwa awake...... Dejavu!
 
Good day, good people!
Déjà vu ni neno lenye asili ya kifaransa likimaanisha "already seen, lived" yaani unakutana na situation, event, scenario au hali yeyote ambayo unakuja kugundua ulishawai kuishi hiyo hali au hayo maisha ya muda huo zamani iliyopita. Hiyo ndio inakuwa déjà vu. Yaani akili yako na roho yako inakiri kabisa ulishawai kuona, kukutana au kuhisi kitu flani hapo zamani but umekutana nacho tena ukiwa na umri huo huo na muda huo huo..then akili na nafsi yako zinakiri kabisa Ku experience na kuishi that situation before. Then that's déjà vu.
Kilichonifanya nikaandika haya ni kwamba Leo Niko hapa kigali, Rwanda sehemu moja inaitwa kanombe....nilikuwa nataka kupata lunch hivyo nikajikuta nimeenda straight hadi kwenye restaurant ambayo nikajikuta nahifahamu kwa jina though iko Rwanda na sijawahi kufika before..hii nikaignore but nilipoingia ndani mhudumu aliekuja kunihudumia alikuwa anamuita yule wa kaunta mama na alinisemesha kinyarwanda nikamuelewa vizuri ilhali sijui kinyarwanda kabisa then nikaletewa msosi nilipoanza kula nikajikuta naijua scenario nzima itakayotokea hadi mwisho wake ambapo nilihisi wataniuliza juu ya bei na upatikanaji wa Mchele wa bongo... Na kweli mwishoni kabisa wakaniuliza juu ya Mchele wa bongo. Akili yangu ilikuwa imepigwa butwaa maana yale maisha Ninakumbuka niliwahi kuyaishi mwanzoni..but this time imetokea Rwanda hadi mgahawa naujua tena Kwa jina then hadi vitendo vyote. Wow! What's behind this? Labda kabla ya kuzaliwa niliwahi kuishi Rwanda? Sijui? Sasa nimeyajuaje kuanzia mazingira hadi mgahawa? I'm confused vibaya hapa!
Kimsimgi baada ya kufikiria kwa muda mrefu nimehisi kuna possibility our spirits might be very old...kabla hatujazaliwa kuna uwezekano tulikuwa tunaexist million of years back maana nina uhakika roho zetu zinauwezo wa kutambua hata maeneo, sura, vitu n.k tulivyovipitia miaka ya nyuma sana hivyo zilishawai kuyaishi hayo maisha husika.
Na kwa kupitia déjà vu nimeanza kuamini kwamba binadamu tunaishi kwenye illusion ya space and time and we are immortal and exist forever in the universe of infinity na roho inatuthibitishia kupitia ubongo kwamba haya maisha tulishawai kuyaishi hapo awali tukiwa na umri huu huu na muda ulikuwa huu huu.
Vipi ilishawai kutokea kwako umekutana na scenario ndogo then ubongo na roho yako vikakumbuka kwamba ulishawai kuipitia au kuishi back then? What your experience on this? Ilishatokea kwako?
View attachment 788767View attachment 788770
Hii hali hali ilishawahi kunitokea pia,nakumbuka siku moja nlitoka safari nkarudi nyumbani nkaenda kwa bibi kumsalimu lakini kuanzia nakaribia kufika nyumbani kwake mpaka nakaribishwa na mazungumzo yote nilikua nayajua,nilikua najua anachosema sasa na baada ya hapo.nlihisi kuchanganyikiwa kidogo maana haikuwa kawaida
 
Tengemeza Uzi mwingine ukisema jinsi Mandela effect inaprove kuna multiple universe
 
Back
Top Bottom