GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Mkurugenzi wa Kilosa aliyeandika barua kwa wananchi kuwa watawagawia hekari mia mbili na hamsini badala ya mia nne toka kwa muwekazaji amejutia kosa lake mara tatu mbele ya Rais yaani nimekosa mimi, nimekosa mimi na nimekosa sana.
Mkurugenzi huyo ameponea chupuchupu kutumbuliwa baada ya kuagiza barua aliyoiandika kwa wananchi mwezi May 2020 airekebishe pale pale kwa kutumia peni na kuandika yafuatayo "Mimi Mkurugenzi ninawaomba radhi wananchi kwani nimekosa sana na nimekosa sana sitarudia tena na hii barua ya kugawa ardhi nimeifuta rasmi"
Mkurugenzi huyo akiwa anatetemeka kwa uwoga yaani ndembe ndembe ameonyesha ujasiri wa hali ya juu kwa kuomba msamaha.
Hili liwe funzo kwa vijana kuwa bora ukaonekana mjinga na mlamba viatu lakini ukatetea kibarua chako na familia yako.
Vijana msikubali kufa na tai shingoni kwa sasa Ajira hakuna.
Kwa jinsi JPM alivyokasirika Mkurugenzi alikuwa anaondoka pale pale lakini akili yake ya kuamua kutubu makosa na kujutia .JPM amempa nafasi ya pili ya kufanya kazi kwa wana Kilosa.
Mkurugenzi Kilosa hoyee!
Mkurugenzi huyo ameponea chupuchupu kutumbuliwa baada ya kuagiza barua aliyoiandika kwa wananchi mwezi May 2020 airekebishe pale pale kwa kutumia peni na kuandika yafuatayo "Mimi Mkurugenzi ninawaomba radhi wananchi kwani nimekosa sana na nimekosa sana sitarudia tena na hii barua ya kugawa ardhi nimeifuta rasmi"
Mkurugenzi huyo akiwa anatetemeka kwa uwoga yaani ndembe ndembe ameonyesha ujasiri wa hali ya juu kwa kuomba msamaha.
Hili liwe funzo kwa vijana kuwa bora ukaonekana mjinga na mlamba viatu lakini ukatetea kibarua chako na familia yako.
Vijana msikubali kufa na tai shingoni kwa sasa Ajira hakuna.
Kwa jinsi JPM alivyokasirika Mkurugenzi alikuwa anaondoka pale pale lakini akili yake ya kuamua kutubu makosa na kujutia .JPM amempa nafasi ya pili ya kufanya kazi kwa wana Kilosa.
Mkurugenzi Kilosa hoyee!