DED Mteule Korogwe, Kwa hili Nakupongeza Rais Magufuli

Pagan Amum

JF-Expert Member
Aug 28, 2015
1,932
4,395
Kati ya vijana vichwa waliopo nchi hii kwa sasa moja wao ni huyu mteule DED wa Korogwe, George John Nyaronga. Ni Mwalimu/Dr wa hesabu Open University....

Ni kijana mwenye uwezo mkubwa sana wa kuchanganua mambo. Ana IQ kubwa sana, ni jasiri, mjengaji wa hoja vizuri na kubwa zaidi ni muadilifu...

Nimefanya naye kazi nyingi sana kwa hakika wana~Korogwe wamepata jembe. Na kwa muda mfupi watanzania tutaona uwezo wa huyu kijana... Na ninamtabiria kufika mbali katika hii serikali ya Rais Magufuli!...

#Pongezi kwa Rais Magufuli
#Hongera sana wana~Korogwe... Tahadhari tu kwa watumishi wa Korogwe, mjiandae kufanya kazi, tena kwa bidii sana. Ni kijana asiye na mchezo katika kazi.... Anapiga kazi kwa juhudi zote, na msishangae mtakuwa mnamuona anafika ofisini saa 10 za alfajiri, na kutoka saa 6 usiku...
 
Ni wa huku Musoma. Kaka yake anaitwa Peter nyaronga yupo wizara ya maliasili. Hamna cha ujiniasi wala IQ hapo
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom