DECEMBER MOSI,siku ya ukimwi duniani,TIBA YA UKIMWI bado pasua kichwa.

Mshinga

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
3,532
1,124
leo ni siku ya ukimwi duniani,watu wanahimizwa kwenda kupima ukimwi.
MATUMAINI YA CHANJO NA TIBA.
mwaka 2010 ilikuwa ni mwaka wa mafanikio makubwa kwa dakitali na mtafiti nguli,dr Fauce wa NIAD marekani ambaye ana historia ndefu kufanikisha hatua nyingi juu ya ukimwi,kuanzia alipovibainisha virus vyenyewe miaka ya 80,baadae akatengeneza ARV inasaidia sana sasa,2010 aliitangazia dunia kuwa amefakia mafanikio ya kimaabara ya kuua VVU vyote zaidi ya sampuli 200 kutoka maeneo tofauti duniani bila kuathiri cell,na ndipo obama akaahidi mpaka 2014 dawa ya ukimwi itakuwa tayari na kuufyeka kabisa ukimwi.
HATA HIVYO MAGUMU BADO YAPO.
kuna vipingamizi 3 vinavyosumbua wanasayansi
1. latent HIV-kuna virus ambavyo vinakuwa mwilini lakini havipo active,na vinaweza kubakia latent kwa muda wote wa uhai wa binadamu,na kitu kibaya dawa inaua virus active tu,na kuna muda na mazingira latent virus zinageuka kuwa active na hapo ni sawa na kwamba mtu hajatibiwa,nini suluhisho la latent virus?
 
suluhisho la latent virus ni kuzi-amsha kwa nguvu(triggering latent virus),na zikiamshwa kwa nguvu na zikawa active basi zitauawa mara moja,tatizo nini hapa?Mechanism iliyopendekezwa haijaweza kuamsha virus vyote,vichache sana viliamka,na vingine vinamka baada ya kuamshwa mara nne ama zaidi,lakini bado ni vichache tu vinaweza kuamshwa kwa nguvu,na siku mgongwa akitumia dawa virusi vyote na vile vilivyoamshwa kwa nguvu vitakufa,lakini vile latent vitabaki,na hapa mtu akipima ataonekana hana virus,lakini akiacha tu kutumia dawa,basi vinaanza kuamka tena vyenyewe,kazi inaanza upya,CHANGAMOTO INAFANYIWA KAZI kuhakisha latent virus zote zinaamshwa na kuuawa.
2.virus reserviour,hapa ni kama sehemu ambapo virus vingi vinajihifadhi,bado ni vigumu kuwaondoa wote katika eneo hili,japo wengi wanaweza kuondolewa,wakiwa kwenye T-cell ndo inakuwa rahisi kuwaangamiza.
3.changamoto ya tatu ni kuharibiwa kwa mfumo wa ulinzi.
MATIBABU YA UKIMWI MPAKA SASA YANAWEZEKANA CHINI YA MAZINGIRA MAALUMU,yapi hayo?Endelea.
 
1.mpaka sasa mtoto aliyezaliwa na ukimwi anaweza kutibiwa na kupona kabisa kama ataanza kupewa dawa mara tu akizaliwa,mfano yule mtoto wa mississip,alianzishiwa dozi akiwa na siku mbili
2.mtu akiambukizwa ukimwi,anaweza kutibiwa na kupona kama atawahi matibabu masaa chini ya 12 toka aambukizwe,lakini baada ya hapo utata unaanza,na dawa hii kwa sasa inatumiwa sana kuzia ukimwi kwa wanawake waliobakwa,ndio maana wanashauri mtu akibakwa awahi hospitalini ili kama atakuwa ameambukizwa akimeza hii dawa ukimwi kwishineyi. kwa sasa dawa hii ililipotiwa kutumiwa na makahaba kenya kujikinga na ukimwi,wanafanya peku na yeyote lakini baada tu ya sex wanabugia dawa hii wanabaki bila maambukizi kabisa.,tuendelee?Maelezo yote ni kwa msaada wa aidsmap.com
 
Tiba Zipo japo hazijathibitishwa rasmi, Zipo shuhuda nyingi za watu waliotumia dawa fulanifulani halafu wakapona kabisa na leo wako mtaani wanadunda
 
Back
Top Bottom