Muju4
JF-Expert Member
- Oct 27, 2014
- 5,321
- 7,158
Nimefurahi sana inatakiwa tuwe na maneno ya kufariji.Nilipokua mdogo, kuna mama alikua mwanachama wa Legio Maria, alifariki siku ya Ijumaa Kuu, wakati wa misa ya mazishi Paroko alisema huyu mama kufariki Ijumaa Kuu ni bahati kubwa, siku aliyofariki Yesu Kristu.
Rais Magufuli laifariki katika mwezi wa Kwaresima, huu ni mwezi wa toba. Kifo katika mwezi huu kina maana kubwa. Ni ishara ya kusamehewa yote uliyoomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu.
Pumzika kwa amani Rais wetu, tumekusamehe na utusamehe. Duniani hakuna mkamilifu.
Mungu akubariki sana.
Pumzika kwa amani JPM.