Mzalendo_Mwandamizi
JF-Expert Member
- Dec 12, 2007
- 1,117
- 4,764
Drill is the same: kila anayehama "acha aende zake"... eti alikuwa na mapungufu flani, japo laiti ungejaribu kuyataja mapungufu hayo kabla hajahama ungeambulia matusi.
Both Chadema na CCM wana uhasama mkubwa dhidi ya ukweli. Waambie ukweli utaitwa kila aina ya jina baya kama si kutukanwa kila aina ya tusi.
Lakini ukweli una tabia moja ya msingi: kuukataa ukweli hakuufanyi kuwa uongo. Ukweli hubaki kuwa ukweli.
Na moja ya ukweli ambao ndugu zangu wa Chadema wanaukwepa ni kwamba kuna virusi vinavyokitafuna chama hicho, virusi vya asili (vinavyopandikizwa na Kitengo: mbunge mmoja wa chama hicho ni afisa wa kitengo sambamba na diwani mmoja) na virusi vilivyoingia kwa kasi mwaka 2015 wakati chama hicho kilipolamba matapishi yake - kwa kumwandama Lowassa miaka 9 mfululizo kuwa ni fisadi kabla ya kumpokea na kumfanya mgombea urais.
Intelijensia ya Chadema ilikuwa imara sana enzi za kina Dokta Slaa. Ndio iliyoiwezesha Chadema kupata nyaraka mbalimbali muhimu zilizokiwezesha chama hicho kuwa mahiri katika kuibua ufisadi.
Na intelijensia hiyo ilikuwa mahiri pia katika kubaini hujuma mbalimbali dhidi ya chama hicho.
Yayumkinika kuhisi kuwa laiti ingekuwa zama hizo, basi huenda wenye mipango ya kuhama wangejulikana mapema na pengine kuchukuliwa hatua stahili.
Ni rahisi kujihadaa kuwa "acha waende" ilhali hamjui WHO IS NEXT. Kwa sababu hata Lowassa alikuwa anasema hivyo hivyo "acha waende" lakini nae kafuata mkumbo.
Ni rahisi kujihadaa kuwa hamahama hii haina athari lakini kama Chadema itajihangaisha kufikiria athari za hamahama hiyo sio kwa wanachama wao bali "watu wasio na vyama" - kundi muhimu kabisa katika siasa za chaguzi za Tanzania - itabaini kuwa ina kazi ya ziada kulishawishi kundi hilo kuwa chama hicho kinastahili kuendelea kuaminiwa.
Back to swali la msingi: Je Chadema inaweza kutuambia WHO IS NEXT (and may be WHO ISN'T)?
Both Chadema na CCM wana uhasama mkubwa dhidi ya ukweli. Waambie ukweli utaitwa kila aina ya jina baya kama si kutukanwa kila aina ya tusi.
Lakini ukweli una tabia moja ya msingi: kuukataa ukweli hakuufanyi kuwa uongo. Ukweli hubaki kuwa ukweli.
Na moja ya ukweli ambao ndugu zangu wa Chadema wanaukwepa ni kwamba kuna virusi vinavyokitafuna chama hicho, virusi vya asili (vinavyopandikizwa na Kitengo: mbunge mmoja wa chama hicho ni afisa wa kitengo sambamba na diwani mmoja) na virusi vilivyoingia kwa kasi mwaka 2015 wakati chama hicho kilipolamba matapishi yake - kwa kumwandama Lowassa miaka 9 mfululizo kuwa ni fisadi kabla ya kumpokea na kumfanya mgombea urais.
Intelijensia ya Chadema ilikuwa imara sana enzi za kina Dokta Slaa. Ndio iliyoiwezesha Chadema kupata nyaraka mbalimbali muhimu zilizokiwezesha chama hicho kuwa mahiri katika kuibua ufisadi.
Na intelijensia hiyo ilikuwa mahiri pia katika kubaini hujuma mbalimbali dhidi ya chama hicho.
Yayumkinika kuhisi kuwa laiti ingekuwa zama hizo, basi huenda wenye mipango ya kuhama wangejulikana mapema na pengine kuchukuliwa hatua stahili.
Ni rahisi kujihadaa kuwa "acha waende" ilhali hamjui WHO IS NEXT. Kwa sababu hata Lowassa alikuwa anasema hivyo hivyo "acha waende" lakini nae kafuata mkumbo.
Ni rahisi kujihadaa kuwa hamahama hii haina athari lakini kama Chadema itajihangaisha kufikiria athari za hamahama hiyo sio kwa wanachama wao bali "watu wasio na vyama" - kundi muhimu kabisa katika siasa za chaguzi za Tanzania - itabaini kuwa ina kazi ya ziada kulishawishi kundi hilo kuwa chama hicho kinastahili kuendelea kuaminiwa.
Back to swali la msingi: Je Chadema inaweza kutuambia WHO IS NEXT (and may be WHO ISN'T)?