DC wa Songwe adaiwa kutishia kumuua Mbunge wa Songwe kwa kufuatilia fedha za Wawekezaji wa mazao

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,480
9,241
MBUNGE wa Songwe (CCM), Philipo Mulugo, amemtuhumu Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Samuel Jeremiah, kwamba ametishia kumuua.

Amedai kuwa chanzo cha kutishiwa na mkuu huyo wa wilaya ni kutokana na kumfuatilia kuhusu matumizi ya fedha za michango ya wawekezaji na anadai kwamba anamkwamisha kufanya maendeleo wilayani hapa.

Mulugo alimweleza hayo Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia jenerali Nicodemus Mwangela, mbele ya kikao cha wadau wa zao la ufuta kilichojumuisha watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, madiwani, wanunuzi wa zao hilo, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakulima.

Hili ni tishio la pili la kutishia kuuawa kwa kiongozi baada lile la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mbozi, Hanji Godigodi ambaye alidai kutishiwa kuuawa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Henerico Mkola, na taarifa za tukio hilo kuripotiwa kituo cha polisi Vwawa na namba (RB) MBZ/IR/200/2021.

Akizungumza katika kikao hicho, Mulugo alisema vitisho dhidi yake kutoka kwa mkuu huyo wa wilaya, vimekuja baada ya kuwa mstari wa mbele kuwatetea wakulima wa zao hilo ambao hawako tayari kwa sasa kupeleka mazao yao kuuza kwa mfumo wa stakabadhi ghalani uliokuwa umetangazwa na serikali ya wilaya.

Mbunge huyo alisema mkuu huyo wa wilaya pia haelewani na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, jambo ambalo amesema si jema kwenye uongozi na linakwamisha maendeleo.

Naye Katibu wa CCM wa Wilaya ya Songwe, Gerald Mwadalu, alipopewa dakika mbili kuzungumza, alimwambia mkuu wa mkoa kuwa kiongozi huyo wa wilaya hana uhusiano mzuri pia na madiwani na viongozi wa chama.

Mwadalu licha ya kukatishwa mara kwa mara na Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza, alidai kuwa chama kimejitahidi mara kadhaa kumwita kwenye vikao ili wajadiliane lakini mara zote amekuwa akikaidi.

Katibu huyo alimkabidhi Mkuu wa Mkoa nyaraka kuhusu mwenendo wa mkuu huyo wa wilaya.

Wakati katibu huyo akiendelea kuzungumza huku akirekodiwa na waandishi wa habari, ghafla mkuu wa mkoa aliingilia kati na kuamuru waandishi wa habari kuacha kurekodi mambo anayoyasema.

Pia Mwengela aliagiza polisi kuzishikilia kamera za waandishi hao kabla ya kutoka katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambako mkutano huo ulikuwa ukifanyika.

Akijibu tuhuma hizo, Jeremiah alisema kwa kifupi kuwa kama mbunge huyo anao ushahidi wa jambo hilo la kutishiwa maisha, anapaswa kwenda kutoa taarifa polisi.

Naye Mwengela aliingilia kati na baadaye akasema mbali na kuwapatanisha viongozi hao huko nyuma na kudhani yameisha, amejionea hali halisi ilivyo na kwamba kwa hekima alizojaliwa atazidi kuketi nao kwa ajili ya kuleta mshikamano.

Ippmedia
 
MBUNGE wa Songwe (CCM), Philipo Mulugo, amemtuhumu Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Samuel Jeremiah, kwamba ametishia kumuua.

Amedai kuwa chanzo cha kutishiwa na mkuu huyo wa wilaya ni kutokana na kumfuatilia kuhusu matumizi ya fedha za michango ya wawekezaji na anadai kwamba anamkwamisha kufanya maendeleo wilayani hapa.

Mulugo alimweleza hayo Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia jenerali Nicodemus Mwangela, mbele ya kikao cha wadau wa zao la ufuta kilichojumuisha watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, madiwani, wanunuzi wa zao hilo, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakulima.

Hili ni tishio la pili la kutishia kuuawa kwa kiongozi baada lile la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mbozi, Hanji Godigodi ambaye alidai kutishiwa kuuawa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Henerico Mkola, na taarifa za tukio hilo kuripotiwa kituo cha polisi Vwawa na namba (RB) MBZ/IR/200/2021.

Akizungumza katika kikao hicho, Mulugo alisema vitisho dhidi yake kutoka kwa mkuu huyo wa wilaya, vimekuja baada ya kuwa mstari wa mbele kuwatetea wakulima wa zao hilo ambao hawako tayari kwa sasa kupeleka mazao yao kuuza kwa mfumo wa stakabadhi ghalani uliokuwa umetangazwa na serikali ya wilaya.

Mbunge huyo alisema mkuu huyo wa wilaya pia haelewani na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, jambo ambalo amesema si jema kwenye uongozi na linakwamisha maendeleo.

Naye Katibu wa CCM wa Wilaya ya Songwe, Gerald Mwadalu, alipopewa dakika mbili kuzungumza, alimwambia mkuu wa mkoa kuwa kiongozi huyo wa wilaya hana uhusiano mzuri pia na madiwani na viongozi wa chama.

Mwadalu licha ya kukatishwa mara kwa mara na Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza, alidai kuwa chama kimejitahidi mara kadhaa kumwita kwenye vikao ili wajadiliane lakini mara zote amekuwa akikaidi.

Katibu huyo alimkabidhi Mkuu wa Mkoa nyaraka kuhusu mwenendo wa mkuu huyo wa wilaya.

Wakati katibu huyo akiendelea kuzungumza huku akirekodiwa na waandishi wa habari, ghafla mkuu wa mkoa aliingilia kati na kuamuru waandishi wa habari kuacha kurekodi mambo anayoyasema.

Pia Mwengela aliagiza polisi kuzishikilia kamera za waandishi hao kabla ya kutoka katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambako mkutano huo ulikuwa ukifanyika.

Akijibu tuhuma hizo, Jeremiah alisema kwa kifupi kuwa kama mbunge huyo anao ushahidi wa jambo hilo la kutishiwa maisha, anapaswa kwenda kutoa taarifa polisi.

Naye Mwengela aliingilia kati na baadaye akasema mbali na kuwapatanisha viongozi hao huko nyuma na kudhani yameisha, amejionea hali halisi ilivyo na kwamba kwa hekima alizojaliwa atazidi kuketi nao kwa ajili ya kuleta mshikamano.

Ippmedia
Wote ni CCM
 
MBUNGE wa Songwe (CCM), Philipo Mulugo, amemtuhumu Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Samuel Jeremiah, kwamba ametishia kumuua.

Amedai kuwa chanzo cha kutishiwa na mkuu huyo wa wilaya ni kutokana na kumfuatilia kuhusu matumizi ya fedha za michango ya wawekezaji na anadai kwamba anamkwamisha kufanya maendeleo wilayani hapa.

Mulugo alimweleza hayo Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia jenerali Nicodemus Mwangela, mbele ya kikao cha wadau wa zao la ufuta kilichojumuisha watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, madiwani, wanunuzi wa zao hilo, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakulima.

Hili ni tishio la pili la kutishia kuuawa kwa kiongozi baada lile la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mbozi, Hanji Godigodi ambaye alidai kutishiwa kuuawa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Henerico Mkola, na taarifa za tukio hilo kuripotiwa kituo cha polisi Vwawa na namba (RB) MBZ/IR/200/2021.

Akizungumza katika kikao hicho, Mulugo alisema vitisho dhidi yake kutoka kwa mkuu huyo wa wilaya, vimekuja baada ya kuwa mstari wa mbele kuwatetea wakulima wa zao hilo ambao hawako tayari kwa sasa kupeleka mazao yao kuuza kwa mfumo wa stakabadhi ghalani uliokuwa umetangazwa na serikali ya wilaya.

Mbunge huyo alisema mkuu huyo wa wilaya pia haelewani na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, jambo ambalo amesema si jema kwenye uongozi na linakwamisha maendeleo.

Naye Katibu wa CCM wa Wilaya ya Songwe, Gerald Mwadalu, alipopewa dakika mbili kuzungumza, alimwambia mkuu wa mkoa kuwa kiongozi huyo wa wilaya hana uhusiano mzuri pia na madiwani na viongozi wa chama.

Mwadalu licha ya kukatishwa mara kwa mara na Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza, alidai kuwa chama kimejitahidi mara kadhaa kumwita kwenye vikao ili wajadiliane lakini mara zote amekuwa akikaidi.

Katibu huyo alimkabidhi Mkuu wa Mkoa nyaraka kuhusu mwenendo wa mkuu huyo wa wilaya.

Wakati katibu huyo akiendelea kuzungumza huku akirekodiwa na waandishi wa habari, ghafla mkuu wa mkoa aliingilia kati na kuamuru waandishi wa habari kuacha kurekodi mambo anayoyasema.

Pia Mwengela aliagiza polisi kuzishikilia kamera za waandishi hao kabla ya kutoka katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambako mkutano huo ulikuwa ukifanyika.

Akijibu tuhuma hizo, Jeremiah alisema kwa kifupi kuwa kama mbunge huyo anao ushahidi wa jambo hilo la kutishiwa maisha, anapaswa kwenda kutoa taarifa polisi.

Naye Mwengela aliingilia kati na baadaye akasema mbali na kuwapatanisha viongozi hao huko nyuma na kudhani yameisha, amejionea hali halisi ilivyo na kwamba kwa hekima alizojaliwa atazidi kuketi nao kwa ajili ya kuleta mshikamano.

Ippmedia
 
Hawa ni wenyewe kwa wenyewe,hakuna shida. Sanasana kila mmoja hapo ajifunze kuheshimu haki. Maana sisi huwa hatujali haki, tunatazama power pekee ambayo nayo huisha wakati fulani. Mulugo,kwa mfano, alishawahi kuwa na power, sijui kama aliheshimu haki.
 
MBUNGE wa Songwe (CCM), Philipo Mulugo, amemtuhumu Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Samuel Jeremiah, kwamba ametishia kumuua.

Amedai kuwa chanzo cha kutishiwa na mkuu huyo wa wilaya ni kutokana na kumfuatilia kuhusu matumizi ya fedha za michango ya wawekezaji na anadai kwamba anamkwamisha kufanya maendeleo wilayani hapa.

Mulugo alimweleza hayo Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia jenerali Nicodemus Mwangela, mbele ya kikao cha wadau wa zao la ufuta kilichojumuisha watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, madiwani, wanunuzi wa zao hilo, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakulima.

Hili ni tishio la pili la kutishia kuuawa kwa kiongozi baada lile la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mbozi, Hanji Godigodi ambaye alidai kutishiwa kuuawa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Henerico Mkola, na taarifa za tukio hilo kuripotiwa kituo cha polisi Vwawa na namba (RB) MBZ/IR/200/2021.

Akizungumza katika kikao hicho, Mulugo alisema vitisho dhidi yake kutoka kwa mkuu huyo wa wilaya, vimekuja baada ya kuwa mstari wa mbele kuwatetea wakulima wa zao hilo ambao hawako tayari kwa sasa kupeleka mazao yao kuuza kwa mfumo wa stakabadhi ghalani uliokuwa umetangazwa na serikali ya wilaya.

Mbunge huyo alisema mkuu huyo wa wilaya pia haelewani na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, jambo ambalo amesema si jema kwenye uongozi na linakwamisha maendeleo.

Naye Katibu wa CCM wa Wilaya ya Songwe, Gerald Mwadalu, alipopewa dakika mbili kuzungumza, alimwambia mkuu wa mkoa kuwa kiongozi huyo wa wilaya hana uhusiano mzuri pia na madiwani na viongozi wa chama.

Mwadalu licha ya kukatishwa mara kwa mara na Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza, alidai kuwa chama kimejitahidi mara kadhaa kumwita kwenye vikao ili wajadiliane lakini mara zote amekuwa akikaidi.

Katibu huyo alimkabidhi Mkuu wa Mkoa nyaraka kuhusu mwenendo wa mkuu huyo wa wilaya.

Wakati katibu huyo akiendelea kuzungumza huku akirekodiwa na waandishi wa habari, ghafla mkuu wa mkoa aliingilia kati na kuamuru waandishi wa habari kuacha kurekodi mambo anayoyasema.

Pia Mwengela aliagiza polisi kuzishikilia kamera za waandishi hao kabla ya kutoka katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambako mkutano huo ulikuwa ukifanyika.

Akijibu tuhuma hizo, Jeremiah alisema kwa kifupi kuwa kama mbunge huyo anao ushahidi wa jambo hilo la kutishiwa maisha, anapaswa kwenda kutoa taarifa polisi.

Naye Mwengela aliingilia kati na baadaye akasema mbali na kuwapatanisha viongozi hao huko nyuma na kudhani yameisha, amejionea hali halisi ilivyo na kwamba kwa hekima alizojaliwa atazidi kuketi nao kwa ajili ya kuleta mshikamano.

Ippmedia
Kijani kitupu, wacha waparuane. Kambare mwenye ndevu kubwa ametoweka, sasa kambare wanaogelea bila mpangilio.
 
Safi kabisa endelezeni urithi mlioachiwa na marehemu Jiwe , muasisi wa ubabe , uvunjifu wa sheria , katiba , utekaji , kujimwa bafai , uuaji , ubambikiaji kesi , haya vijana wamerithi utapeli , ufisadi .
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom