Ushuzi tupu.....Safi kabisa endelezeni urithi mlioachiwa na marehemu Jiwe , muasisi wa ubabe , uvunjifu wa sheria , katiba , utekaji , kujimwa bafai , uuaji , ubambikiaji kesi , haya vijana wamerithi utapeli , ufisadi .
Heheheeeee. The "Original sin" continues tormenting.MBUNGE wa Songwe (CCM), Philipo Mulugo, amemtuhumu Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Samuel Jeremiah, kwamba ametishia kumuua.
Amedai kuwa chanzo cha kutishiwa na mkuu huyo wa wilaya ni kutokana na kumfuatilia kuhusu matumizi ya fedha za michango ya wawekezaji na anadai kwamba anamkwamisha kufanya maendeleo wilayani hapa.
Mulugo alimweleza hayo Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia jenerali Nicodemus Mwangela, mbele ya kikao cha wadau wa zao la ufuta kilichojumuisha watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, madiwani, wanunuzi wa zao hilo, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakulima.
Hili ni tishio la pili la kutishia kuuawa kwa kiongozi baada lile la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mbozi, Hanji Godigodi ambaye alidai kutishiwa kuuawa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Henerico Mkola, na taarifa za tukio hilo kuripotiwa kituo cha polisi Vwawa na namba (RB) MBZ/IR/200/2021.
Akizungumza katika kikao hicho, Mulugo alisema vitisho dhidi yake kutoka kwa mkuu huyo wa wilaya, vimekuja baada ya kuwa mstari wa mbele kuwatetea wakulima wa zao hilo ambao hawako tayari kwa sasa kupeleka mazao yao kuuza kwa mfumo wa stakabadhi ghalani uliokuwa umetangazwa na serikali ya wilaya.
Mbunge huyo alisema mkuu huyo wa wilaya pia haelewani na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, jambo ambalo amesema si jema kwenye uongozi na linakwamisha maendeleo.
Naye Katibu wa CCM wa Wilaya ya Songwe, Gerald Mwadalu, alipopewa dakika mbili kuzungumza, alimwambia mkuu wa mkoa kuwa kiongozi huyo wa wilaya hana uhusiano mzuri pia na madiwani na viongozi wa chama.
Mwadalu licha ya kukatishwa mara kwa mara na Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza, alidai kuwa chama kimejitahidi mara kadhaa kumwita kwenye vikao ili wajadiliane lakini mara zote amekuwa akikaidi.
Katibu huyo alimkabidhi Mkuu wa Mkoa nyaraka kuhusu mwenendo wa mkuu huyo wa wilaya.
Wakati katibu huyo akiendelea kuzungumza huku akirekodiwa na waandishi wa habari, ghafla mkuu wa mkoa aliingilia kati na kuamuru waandishi wa habari kuacha kurekodi mambo anayoyasema.
Pia Mwengela aliagiza polisi kuzishikilia kamera za waandishi hao kabla ya kutoka katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambako mkutano huo ulikuwa ukifanyika.
Akijibu tuhuma hizo, Jeremiah alisema kwa kifupi kuwa kama mbunge huyo anao ushahidi wa jambo hilo la kutishiwa maisha, anapaswa kwenda kutoa taarifa polisi.
Naye Mwengela aliingilia kati na baadaye akasema mbali na kuwapatanisha viongozi hao huko nyuma na kudhani yameisha, amejionea hali halisi ilivyo na kwamba kwa hekima alizojaliwa atazidi kuketi nao kwa ajili ya kuleta mshikamano.
Ippmedia
Mambo ya fweza tu hapo
Ova
Iko hivi issue pale ni zao la ufuta, kule hua kuna wahindi wanaweza kuingia sasa ili wanunueshambani na wasiguswe wanawahi kukata pesa kwa DC hapo mambo ya stakabadhi ghalani yanapigwa danadana na mkulima akienda kuiuzia serikali bei ni ndogo sasa wanakubaliana kwa hesabu fulani mkuu utachukua kiasi kadhaa, sasa mbunge anaona posho inampita juu kwa juu ndio ugomvi unaanzia hapo sasa
Madhalimu hawajawahi kuwa na mwisho mwema, lazima walane hata wao kwa wao ili ile kauli ya "ukiishi kwa upanga ,utakufa kwa upanga" ili itimieWhy kugombania fito kwenye ujenzi wa nyumba moja?
Duuh watu mpaka wanataka kupasuana.
Alichofanya Mbunge ni kuwa upande wa wananchi walio mchagua, wakulima hawataki kuuza kwa mfumo wa stakabadhi gharani maana kuna hela walikopeshwa na wafanya biashara, sasa serikali ikisema inunue, wale wafanya biashara watalipwa nini?Iko hivi issue pale ni zao la ufuta, kule hua kuna wahindi wanaweza kuingia sasa ili wanunueshambani na wasiguswe wanawahi kukata pesa kwa DC hapo mambo ya stakabadhi ghalani yanapigwa danadana na mkulima akienda kuiuzia serikali bei ni ndogo sasa wanakubaliana kwa hesabu fulani mkuu utachukua kiasi kadhaa, sasa mbunge anaona posho inampita juu kwa juu ndio ugomvi unaanzia hapo sasa
Tunaruka masomo ya maadili ya uongoziMBUNGE wa Songwe (CCM), Philipo Mulugo, amemtuhumu Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Samuel Jeremiah, kwamba ametishia kumuua.
Amedai kuwa chanzo cha kutishiwa na mkuu huyo wa wilaya ni kutokana na kumfuatilia kuhusu matumizi ya fedha za michango ya wawekezaji na anadai kwamba anamkwamisha kufanya maendeleo wilayani hapa.
Mulugo alimweleza hayo Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia jenerali Nicodemus Mwangela, mbele ya kikao cha wadau wa zao la ufuta kilichojumuisha watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, madiwani, wanunuzi wa zao hilo, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakulima.
Hili ni tishio la pili la kutishia kuuawa kwa kiongozi baada lile la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mbozi, Hanji Godigodi ambaye alidai kutishiwa kuuawa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Henerico Mkola, na taarifa za tukio hilo kuripotiwa kituo cha polisi Vwawa na namba (RB) MBZ/IR/200/2021.
Akizungumza katika kikao hicho, Mulugo alisema vitisho dhidi yake kutoka kwa mkuu huyo wa wilaya, vimekuja baada ya kuwa mstari wa mbele kuwatetea wakulima wa zao hilo ambao hawako tayari kwa sasa kupeleka mazao yao kuuza kwa mfumo wa stakabadhi ghalani uliokuwa umetangazwa na serikali ya wilaya.
Mbunge huyo alisema mkuu huyo wa wilaya pia haelewani na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, jambo ambalo amesema si jema kwenye uongozi na linakwamisha maendeleo.
Naye Katibu wa CCM wa Wilaya ya Songwe, Gerald Mwadalu, alipopewa dakika mbili kuzungumza, alimwambia mkuu wa mkoa kuwa kiongozi huyo wa wilaya hana uhusiano mzuri pia na madiwani na viongozi wa chama.
Mwadalu licha ya kukatishwa mara kwa mara na Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza, alidai kuwa chama kimejitahidi mara kadhaa kumwita kwenye vikao ili wajadiliane lakini mara zote amekuwa akikaidi.
Katibu huyo alimkabidhi Mkuu wa Mkoa nyaraka kuhusu mwenendo wa mkuu huyo wa wilaya.
Wakati katibu huyo akiendelea kuzungumza huku akirekodiwa na waandishi wa habari, ghafla mkuu wa mkoa aliingilia kati na kuamuru waandishi wa habari kuacha kurekodi mambo anayoyasema.
Pia Mwengela aliagiza polisi kuzishikilia kamera za waandishi hao kabla ya kutoka katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambako mkutano huo ulikuwa ukifanyika.
Akijibu tuhuma hizo, Jeremiah alisema kwa kifupi kuwa kama mbunge huyo anao ushahidi wa jambo hilo la kutishiwa maisha, anapaswa kwenda kutoa taarifa polisi.
Naye Mwengela aliingilia kati na baadaye akasema mbali na kuwapatanisha viongozi hao huko nyuma na kudhani yameisha, amejionea hali halisi ilivyo na kwamba kwa hekima alizojaliwa atazidi kuketi nao kwa ajili ya kuleta mshikamano.
Ippmedia
Iko hivi issue pale ni zao la ufuta, kule hua kuna wahindi wanaweza kuingia sasa ili wanunueshambani na wasiguswe wanawahi kukata pesa kwa DC hapo mambo ya stakabadhi ghalani yanapigwa danadana na mkulima akienda kuiuzia serikali bei ni ndogo sasa wanakubaliana kwa hesabu fulani mkuu utachukua kiasi kadhaa, sasa mbunge anaona posho inampita juu kwa juu ndio ugomvi unaanzia hapo sasaNyote hamjui hali ya Songwe, DC kajitahidi sana na hiyo wilaya mpya, kapiga kazi mno kwa maendeleo ya Songwe pale Mkwajuni katika sekta zote kuanzia afya, elimu n.k. Mulugo ana tabia za wivu na watu wake aliowapanga wanamfitini sana DC. Dc anasimamia maelekezo lengwa ya Serikali na yupo very strict na ujingaujinga unaoendelea. Watu wa Songwe ni wazito haswa jamaa anawaweza.