Katika kile kinachoonekana ni udhaifu wa watendaji wa wateule wa Mh. Rais Jakaya Kikwete Mh Novatus Makunga dc wa Hai amelalamikiwa na wananchi wa kwa kushindwa kutatua migogoro ya vijiji na kata mbalimbali na kuwa chanzo na mlezi wa migogoro ya uongozi ktk maeneo tofauti tofauti ambayo nitayafafanua hapa chini.
MGOGORO KIJIJI CHA ISUKI KATA YA MASAMA KATI: Mnamo tar 24-12-2012 mh DC akiambatana na DED (mkurugenzi) hai walifika kijj cha isuki kuja kusikiliza kero za wananchi dhidi ya m/kiti wao wa kijiji ya kutofanya mikutano ya kisheria tangu achaguliwe 2009.Kwenye mkutano huo wananchi walimkataa m/kiti huyo ila DC akamlinda kwa kutumia polisi.
-Aliahidi kutuma timu ya ukaguzi badala yake wale wananchi waliokuwa mstari wa mbele kudai TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZ YA KIJIJI WALIFUATWA NA POLISI NA KUTENGENEZEWA KESI YA KUFANYA VURUGU na kesi ipo mahakamani kwa maelekezo ya DC-NOVATUSI MAKUNGA.
-Amekuwa akiingilia utendaji wa halmashauri na kujifanya ni sehemu ya baraza la madiwani. Mfano mnamo tar 21/5/2013 madiwani walihoji azimio la utatuzi mgogoro wa mas/kat na kujulishwa kuwa DC ameunda tume ya kushughulikia suala hilo jambo ambalo liliwakasirisha madiwani na kuhoji DC ni nan kwenye baraza la madiwani? Madiwani walikataa majibu hayo na kumwagiza mkurugenz kushughulikia na kumuonya DC asiingilie maamuzi ya baraza la madiwani.
-Amekuwa akitoa maelekezo kwa mkurugenzi kutoshughulikia malalamiko yanayoletwa na wananchi juu ya utendaji mbovu wa watendaji wa vijiji na kata.
-Amekuwa akitumia magari ya halmashauri kwa shughuli zake za kikazi na binafsi na baadaye kudai posho huku akujuwa hana fungu la DC kwenye halmashauri wakati yeye ni mtumishi wa serikali kuu.
NI CHANZO NA MLEZI WA MGOGORO WA SHAMBA LA NKWANSIRA. Amewatapeli wananchi (vyama vya ushirika) waliokuwa na mgogoro na uongozi wa bodi ya shamba ambayo imeshindwa kuwasomea wananchi mapato na matumizi ya shamba chini ya usimamizi wao. Aliahidi kufikisha suala lao kwa waziri wa chakula na ushirika ili kulipatia ufumbuzi badala yake amesimamia ubinafsishaji wa shamba hilo kwa mwekezaji mwingine kupitia bodi ile iliyokataliwa na bila vyama vya ushirika/wananchi kujulishwa.
KUINGILIA KESI ZILIZOKO MAHAKAMANI
Kesi ya ndg LEVIS LEWIS Vs KADCO uwanja wa ndege KIA ambapo kauli yake ya tar 21/5/2013 ktk mtandao wa fb alimwagiza ndg Levis kuondoka kwenye nyumba za kadco huku akijua Levis ni mpangaji halali jambo ambalo tar 30/5/2013 mahakama ya kitengo cha ardhi moshi ilifuata uamuzi wa Mh. Makunga.
Amekuwa akiwapa kiburi wenyeviti wa na watendaji wa wa vijiji na kata wanaaovurunda katika utumishi wao kwa kuingiza siasa katika utendaji. Mfano tar 03/2/2013 alikaa kikao na wenyeviti wanne wa vijiji vya kata ya masama kati na kuwashauri kuandika barua kwa waziri mkuu kumlalamikia diwani wa kata hiyo (CHADEMA) ushauri ulitekelezwa tar 5/2/2013.
MGOGORO KIJIJI CHA ISUKI KATA YA MASAMA KATI: Mnamo tar 24-12-2012 mh DC akiambatana na DED (mkurugenzi) hai walifika kijj cha isuki kuja kusikiliza kero za wananchi dhidi ya m/kiti wao wa kijiji ya kutofanya mikutano ya kisheria tangu achaguliwe 2009.Kwenye mkutano huo wananchi walimkataa m/kiti huyo ila DC akamlinda kwa kutumia polisi.
-Aliahidi kutuma timu ya ukaguzi badala yake wale wananchi waliokuwa mstari wa mbele kudai TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZ YA KIJIJI WALIFUATWA NA POLISI NA KUTENGENEZEWA KESI YA KUFANYA VURUGU na kesi ipo mahakamani kwa maelekezo ya DC-NOVATUSI MAKUNGA.
-Amekuwa akiingilia utendaji wa halmashauri na kujifanya ni sehemu ya baraza la madiwani. Mfano mnamo tar 21/5/2013 madiwani walihoji azimio la utatuzi mgogoro wa mas/kat na kujulishwa kuwa DC ameunda tume ya kushughulikia suala hilo jambo ambalo liliwakasirisha madiwani na kuhoji DC ni nan kwenye baraza la madiwani? Madiwani walikataa majibu hayo na kumwagiza mkurugenz kushughulikia na kumuonya DC asiingilie maamuzi ya baraza la madiwani.
-Amekuwa akitoa maelekezo kwa mkurugenzi kutoshughulikia malalamiko yanayoletwa na wananchi juu ya utendaji mbovu wa watendaji wa vijiji na kata.
-Amekuwa akitumia magari ya halmashauri kwa shughuli zake za kikazi na binafsi na baadaye kudai posho huku akujuwa hana fungu la DC kwenye halmashauri wakati yeye ni mtumishi wa serikali kuu.
NI CHANZO NA MLEZI WA MGOGORO WA SHAMBA LA NKWANSIRA. Amewatapeli wananchi (vyama vya ushirika) waliokuwa na mgogoro na uongozi wa bodi ya shamba ambayo imeshindwa kuwasomea wananchi mapato na matumizi ya shamba chini ya usimamizi wao. Aliahidi kufikisha suala lao kwa waziri wa chakula na ushirika ili kulipatia ufumbuzi badala yake amesimamia ubinafsishaji wa shamba hilo kwa mwekezaji mwingine kupitia bodi ile iliyokataliwa na bila vyama vya ushirika/wananchi kujulishwa.
KUINGILIA KESI ZILIZOKO MAHAKAMANI
Kesi ya ndg LEVIS LEWIS Vs KADCO uwanja wa ndege KIA ambapo kauli yake ya tar 21/5/2013 ktk mtandao wa fb alimwagiza ndg Levis kuondoka kwenye nyumba za kadco huku akijua Levis ni mpangaji halali jambo ambalo tar 30/5/2013 mahakama ya kitengo cha ardhi moshi ilifuata uamuzi wa Mh. Makunga.
Amekuwa akiwapa kiburi wenyeviti wa na watendaji wa wa vijiji na kata wanaaovurunda katika utumishi wao kwa kuingiza siasa katika utendaji. Mfano tar 03/2/2013 alikaa kikao na wenyeviti wanne wa vijiji vya kata ya masama kati na kuwashauri kuandika barua kwa waziri mkuu kumlalamikia diwani wa kata hiyo (CHADEMA) ushauri ulitekelezwa tar 5/2/2013.