DC Victoria Mwanziva: Miaka Miwili ya Rais Samia imekuwa ya Neema na Baraka tele kwa Wana-Ludewa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,893
940

DC VICTORIA MWANZIVA - MIAKA MIWILI YA RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN NDANI YA WILAYA YA LUDEWA

Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, Victoria Mwanziva amesema; kwa hakika Miaka Miwili imekuwa ya Neema na Baraka tele kwa Wana-Ludewa, kwani Rais Samia amekuwa akiitazama Wilaya kwa jicho la upekee sana. Wananchi wa Ludewa wameshuhudia Miradi mikubwa na ya fedha nyingi ikija ndani ya Wilaya.

1. Ludewa imepata Shilingi Bilioni 2.6 kwaajili ya ufunguzi wa barabara za Mwambao.

2. Ludewa imepata Shilingi 2.8 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Milioni 500 za ujenzi wa Ikulu, na Milioni 150 za ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi (DED )

3. Ludewa imepata Shilingi 5.4 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo.

4. Ludewa imepata Shilingi 179 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha zege Lusitu - Mawengi.

5. Ludewa imepata Shilingi 5.4 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa barabra eneo la Mlima Kimelembe ambao ulikuwa chanzo cha ajali nyingi.

6. Ludewa imepata Milioni 900 kwaajili ya ukarabati wa Hospitali ya Wilaya, Milioni 250 kwaajili ya ujenzi wa jengo la ICU Hospitali ya Wilaya, Milioni 500 kukamilisha kituo cha Afya Mundindi, na ujenzi wa zahanati 16 ambapo nne zimeshakamilika na zinatoa huduma (Mholo, Nsisi, Mdilidili na Lifua), huku 12 zikiendelea na ujenzi (Mkiu, Kimelembe, Ndowa, Chimbo, Liunji, Lihagule na Mbongo, Sagalu, Ludewa kijijini, Kimata, Nsele na Mbugani).

7. Ludewa imepata fedha za miradi ya Maji, Kata ya Mawengi wamepewa Bilioni 2, Mavala Bilioni 1, Mavanga Bilioni 1.5, Luvuyo Bilioni 1.5, Madope Milioni 508, Lifua na Manda Milioni 600 na kata ya Ludewa Bilioni 7.

8. Ludewa imepata minara ya simu mipya 7 ambayo inatoa huduma na mwaka huu tunarajaia kuanza ujenzi wa minara mingine sita.

9. Ludewa imepata Ujenzi wa daraja mto Ruhuhu, ambalo limeokoa wananchi wengi wa Kata ya Ruhuhu kuliwa na Mamba

10. Ludewa imepata Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Lubonde ambayo kiasi cha Sh. 470 Milioni kutoka Serikali kuu na Milioni 55.5 kutoka mapato ya ndani yametumika na imeanza kutoa huduma, ujenzi wa maabara mpya 12, ujenzi wa vyumba 41 vya madarasa S/M na Vyumba 81 S/Sekondari

11. Ludewa imepata zaidi ya Bilioni 10.3 kwaajili ya ujenzi wa barabra vijijini kupitia TARURA.

#LudewaYetu

WhatsApp Image 2023-03-24 at 01.04.02.jpeg
WhatsApp Image 2023-03-24 at 01.04.03(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-24 at 01.04.05(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-24 at 01.04.05(2).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-24 at 01.04.05.jpeg
WhatsApp Image 2023-03-24 at 01.04.04(1).jpeg
 
wakishashiba ni kusifia tu , huyu dada maisha yake ni kujikomba ccm yani ukiwatoa ccm hawa maisha yao ni magumu sana
Hakika!
Ukisoma bandiko lote hakuna jambo jipya. Alafu nani katengeneza hizo wenyewe wanaita Graphics zenye picha ya Mh Rais? Very low standard, yaani bongo watu wapowapo tu.
 
Kwa hiyo hata minara ya simu mama Samia kajenga? Duh tuna safari ndefu sana!
Kama barabara ya zege kutoka Lusitu hadi Mawengi ilianza kipindi cha Jiwe na mpaka anafariki ilikuwa imeshafika mbali.
Shule za sekondari na zahanati wananchi wanashiriki ujenzi kwa 100% kama kusomba tofali, mawe nk. lakini sifa anapewa mmoja.
Kuna muda tunasifia hadi tunazidisha aise!
 
Huyu DC Victoria anapenda sana kucheza na media, cheap publicity, akicheza muda si mrefu Mama anampiga chini kama yule aliyeigiza kutekwa kwa Mh. Rais.

Huyu DC ni mipicha picha kila kona, anadhani yuko FB au Instagram au Badoo, kila kona anaweka mapicha na picha yake kila kona kujitangaza, picha nani anataka ya DC kila kona mipicha yake, huyu akicheza Mama Samia anakula kichwa.. Jamani, wachapa kazi hawana muda wa kujitangaza hovyo hovyo mitandaoni..
 

DC VICTORIA MWANZIVA - MIAKA MIWILI YA RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN NDANI YA WILAYA YA LUDEWA

Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, Victoria Mwanziva amesema; kwa hakika Miaka Miwili imekuwa ya Neema na Baraka tele kwa Wana-Ludewa, kwani Rais Samia amekuwa akiitazama Wilaya kwa jicho la upekee sana. Wananchi wa Ludewa wameshuhudia Miradi mikubwa na ya fedha nyingi ikija ndani ya Wilaya.

1. Ludewa imepata Shilingi Bilioni 2.6 kwaajili ya ufunguzi wa barabara za Mwambao.

2. Ludewa imepata Shilingi 2.8 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Milioni 500 za ujenzi wa Ikulu, na Milioni 150 za ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi (DED )

3. Ludewa imepata Shilingi 5.4 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo.

4. Ludewa imepata Shilingi 179 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha zege Lusitu - Mawengi.

5. Ludewa imepata Shilingi 5.4 Bilioni kwaajili ya ujenzi wa barabra eneo la Mlima Kimelembe ambao ulikuwa chanzo cha ajali nyingi.

6. Ludewa imepata Milioni 900 kwaajili ya ukarabati wa Hospitali ya Wilaya, Milioni 250 kwaajili ya ujenzi wa jengo la ICU Hospitali ya Wilaya, Milioni 500 kukamilisha kituo cha Afya Mundindi, na ujenzi wa zahanati 16 ambapo nne zimeshakamilika na zinatoa huduma (Mholo, Nsisi, Mdilidili na Lifua), huku 12 zikiendelea na ujenzi (Mkiu, Kimelembe, Ndowa, Chimbo, Liunji, Lihagule na Mbongo, Sagalu, Ludewa kijijini, Kimata, Nsele na Mbugani).

7. Ludewa imepata fedha za miradi ya Maji, Kata ya Mawengi wamepewa Bilioni 2, Mavala Bilioni 1, Mavanga Bilioni 1.5, Luvuyo Bilioni 1.5, Madope Milioni 508, Lifua na Manda Milioni 600 na kata ya Ludewa Bilioni 7.

8. Ludewa imepata minara ya simu mipya 7 ambayo inatoa huduma na mwaka huu tunarajaia kuanza ujenzi wa minara mingine sita.

9. Ludewa imepata Ujenzi wa daraja mto Ruhuhu, ambalo limeokoa wananchi wengi wa Kata ya Ruhuhu kuliwa na Mamba

10. Ludewa imepata Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Lubonde ambayo kiasi cha Sh. 470 Milioni kutoka Serikali kuu na Milioni 55.5 kutoka mapato ya ndani yametumika na imeanza kutoa huduma, ujenzi wa maabara mpya 12, ujenzi wa vyumba 41 vya madarasa S/M na Vyumba 81 S/Sekondari

11. Ludewa imepata zaidi ya Bilioni 10.3 kwaajili ya ujenzi wa barabra vijijini kupitia TARURA.

#LudewaYetu

View attachment 2563704View attachment 2563705View attachment 2563706View attachment 2563707View attachment 2563708View attachment 2563709
Sio Ludewa tu Mama amefanya Maendeleo Tanzania nzima ila kati ya kitu kikubwa alichokifanya kwa miaka miwili ni kuimarisha diplomasia ya uchumi, democrasia pamoja na kubadili sera ya biashara na uwekezaji
 
Back
Top Bottom