Hai: DC Sabaya aagiza wamiliki wa mabasi kukamatwa kwa tuhuma za kuhujumu miundombinu ya Reli Dar-Moshi

jd41

JF-Expert Member
Aug 23, 2015
3,756
4,842
Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ameagiza wamiliki wawili wa mabasi kufika kituo cha polisi Boma n'gombe leo kabla ya saa 12 jioni, kwa tuhuma za kuandaa genge la watu wanaohujumu miundombinu ya reli.

Watuhumiwa hao ni Clemence Mbowe anayemiliki mabasi ya Machame Safari, na Rodrick Uronu anayemiliki mabasi ya Lim Safari.

Mbowe alipoulizwa na Mwananchi kuhusu tuhuma hizo alisema si za kweli na kwamba DC anataka tu kuwachafua, amesema kama wana tuhuma angewaita ofisini maana yeye ni kiongozi hivyo haoni sababu kwa nini aongee kwenye mkutano wa hadhara, atatafuta haki yake mahakamani.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya ameagiza wamiliki wawili wa mabasi kukamatwa kwa tuhuma za kuunda genge la uhalifu kwa lengo la kuhujumu miundombinu ya reli ili kuathiri usafiri wa treni ya abiria kati ya Dar es Salaam - Moshi.

Wafanyabiashara hao waliotakiwa kuripoti kituo cha Polisi Bomang'ombe leo Jumapili Januari 19, 2020 kabla ya saa 10 jioni ni Clemence Mbowe anayemiliki mabasi ya Machame Safari na Rodrick Uronu anayemiliki mabasi ya Lim Safari.

Kwa mahojiano waliofanya na @moshifm1 Clemence Mbowe amesema kuwa tuhuma hizo za yeye kuhujumu sio za kweli na kwamba yeye yupo Dar es salaam na ameona kwenye mitandao ya kijamii hivyo atakuja Moshi na kufika ofisini kwa Sabaya kutaka kujua tuhuma hizo.
 
DC HAI AAGIZA KUKAMATWA WAMILIKI WA MABASI KWA KOSA LA KUUNDA GENGE LA UHALIFU ILI KUHUJUMU MIUNDOMBINU

Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya ameagiza wamiliki wawili wa mabasi kukamatwa kwa tuhuma za kuunda genge la uhalifu kwa lengo la kuhujumu miundombinu ya reli ili kuathiri usafiri wa treni ya abiria kati ya Dar es Salaam- Moshi.

Wafanyabiashara hao waliotakiwa kuripoti kituo cha Polisi Bomang'ombe leo Jumapili Januari 19, 2020 kabla ya saa 10 jioni ni Clemence Mbowe anayemiliki mabasi ya Machame Safari na Rodrick Uronu wa mabasi ya Lim Safari.

Kwa mahojiano waliofanya na MOSHI FM 90.7 Clemence Mbowe amesema kuwa tuhuma hizo za yeye kuhujumu siyo za kweli na kwamba yeye yupo Dar es salaam na ameona kwenye mitandao ya kijamii hivyo ataenda Moshi na kufika ofisini kwa Sabaya kutaka kujua tuhuma hizo.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni muendelezo wa Mbambiko wa kesi za uhujumu uchumi unaondelea hapa nchini

Viongozi hawa ambao hawajachaguliwa na wananchi na ambao wamepewa madaraka ya kinyampara ya kikoloni ni kizingiti kikubwa sana kwa ustawi wa Demokrasia nchini

Huu ni wakati muafaka wa kuibadilisha hii katiba
 
Kupuuzia habari kama hizi ni ukosefu wa hekima, bila kujali ni nani anasema...kama kweli kuna hujuma Wahusika washughulikiwe..ila asionewe Mtu.
Hujuma wapi,kukosa abiria ndo hujuma?.
Abiria wameshaisha Arusha na Kilimanjaro wote wameshamaliza mikoani.

Huo mkutano ndo mahakamani hapo?.
Kama ana ushahidi apeleke mahakamani siyo kupiga Lomon,weka ushahidi mezani Kama unao watu wawajibike.
 
Wanahujumu kivipi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Inashangaza sana. Yaani kati ya kampuni lukuki za mabasi ya Dar /Moshi hawa wawili tu ndiyo wapange uhujumu wa reli?! Ina maana wao tu ndiyo wameathirika na ujio wa Treni?!

Isitoshe Shirika la Reli lina kikosi cha polisi ambao moja ya kazi zao ni kushughulikia wahujumu wa mali za shirika. Hawa wako kimya.Kama Sabaya anaona hawafai aombe apewe uongozi wa kikosi cha polisi reli.
 
Back
Top Bottom