DC Muro awashukia Viongozi wa dini wanaoishi kwa Sadaka

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
VIONGOZI wa dini wametakiwa kuondoa dhana ya kuishi kwa kutegemea sadaka za waumini na michango ya wahisani badala yake wafanyekazi kwa bidii ikiwemo kutumia taaluma zao kuinua uchumi wa Taifa.


Kauli hiyo ameitoa mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro ,ambaye alilazimika kutiririkwa na machozi mara kwa mara wakati watumishi hao wa mungu wapatao 300 wakishusha maombi ya nguvu kwa rais John Magufuli, yaliyofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha ualimu Patandi kilichopo wilayani humo na kushirikisha maaskofu,Mapadri na wachungaji.

Askofu wa kanisa la Blessing Altar, Isaya Sezya amesema kuwa rais Magufuli ni mzalendo na ameonyesha dhamira ya kweli ya kulikomboa taifa kwa kupambana na mafisadi waliokuwa wananufaika na rasilimali za nchi kwa maslahi yao binafsi.


Muro aliwataka viongozi wa madhehubu hayo kufanya kazi kwa bidii ikiwemo kutumia taaluma zao kujenga uchumi badala ya kukaa na kutegemea sadaka kama sehemu ya kipato chao.


Kuhusu malalamiko yaliyowasilishwa ofisini kwake na baadhi ya wananchi juu ya makanisa yanayomea kama uyoga kwenye makazi ya watu Muro alisema ni vyema makanisa hayo yakawa na vifaa maalum vya kuzuia sauti kutoka nje ili kuepuka kusumbua watu nyakati za usiku wakati wa maombi.

Alisema kwa kipindi chake atakachokuwa mkuu wa wilaya hiyo hakuna kanisa litakalofungwa na serikali na kwamba atashirikiana na viongozi wa makanisa hayo kufanya harambee kwa ajili ya kujenga makanisa yenye vifaa maalum vya kuzuia sauti.

IMG-20190519-WA0003.jpeg
IMG-20190519-WA0007.jpeg
 
Sijamuelewa pale anaposema kuwa viongozi wa dini wasitegemee Sadaka na badala yake watumie taaluma zao ili kuweza kuishi

Hivi anajua kuwa watumishi wa Mungu ni walezi wa jamii yote wanayoiongoza??

Atawaambiaje watumishi watumie taaluma yao kujiongeza kimapato na wasitegemee sadaka kutoka kwa waumini wao??
 
Akifanikiwa kujenga kanisa moja tu lenye vifaa maalum vya kuzuia sauti tutaarifiane tafadhali.
 
Siamini kama kwenye huo mkusanyiko palikuwa na mapadri wa Catholic. Labda ututajie jina na parokia alikotoka huyo Padri/mapadri
 
VIONGOZI wa dini wametakiwa kuondoa dhana ya kuishi kwa kutegemea sadaka za waumini na michango ya wahisani badala yake wafanyekazi kwa bidii ikiwemo kutumia taaluma zao kuinua uchumi wa Taifa.


Kauli hiyo ameitoa mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro ,ambaye alilazimika kutiririkwa na machozi mara kwa mara wakati watumishi hao wa mungu wapatao 300 wakishusha maombi ya nguvu kwa rais John Magufuli, yaliyofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha ualimu Patandi kilichopo wilayani humo na kushirikisha maaskofu,Mapadri na wachungaji.

Askofu wa kanisa la Blessing Altar, Isaya Sezya amesema kuwa rais Magufuli ni mzalendo na ameonyesha dhamira ya kweli ya kulikomboa taifa kwa kupambana na mafisadi waliokuwa wananufaika na rasilimali za nchi kwa maslahi yao binafsi.


Muro aliwataka viongozi wa madhehubu hayo kufanya kazi kwa bidii ikiwemo kutumia taaluma zao kujenga uchumi badala ya kukaa na kutegemea sadaka kama sehemu ya kipato chao.


Kuhusu malalamiko yaliyowasilishwa ofisini kwake na baadhi ya wananchi juu ya makanisa yanayomea kama uyoga kwenye makazi ya watu Muro alisema ni vyema makanisa hayo yakawa na vifaa maalum vya kuzuia sauti kutoka nje ili kuepuka kusumbua watu nyakati za usiku wakati wa maombi.

Alisema kwa kipindi chake atakachokuwa mkuu wa wilaya hiyo hakuna kanisa litakalofungwa na serikali na kwamba atashirikiana na viongozi wa makanisa hayo kufanya harambee kwa ajili ya kujenga makanisa yenye vifaa maalum vya kuzuia sauti.

View attachment 1102217View attachment 1102219
Hajui kwa biblia imeagiza viongozi wa dini watatupandia vya rohoni na sisi tuwapandie vya mwilini?
Au hajui kuwa wanatakiwa kula vya madhabahuni?
Viongozi wa dini wana wito na akumbuke wameitwa,kutegemea vya madhabahuni ni sawa. Zaka ni haki yao kibiblia na wanafanya kazi sawa na yeye anavyoenda ofisini.
Watu wanashida na zinahitaji huduma masaa yote,wakienda maofisini hao wenye shida nani awahudumie?
 
VIONGOZI wa dini wametakiwa kuondoa dhana ya kuishi kwa kutegemea sadaka za waumini na michango ya wahisani badala yake wafanyekazi kwa bidii ikiwemo kutumia taaluma zao kuinua uchumi wa Taifa.


Kauli hiyo ameitoa mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro ,ambaye alilazimika kutiririkwa na machozi mara kwa mara wakati watumishi hao wa mungu wapatao 300 wakishusha maombi ya nguvu kwa rais John Magufuli, yaliyofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha ualimu Patandi kilichopo wilayani humo na kushirikisha maaskofu,Mapadri na wachungaji.

Askofu wa kanisa la Blessing Altar, Isaya Sezya amesema kuwa rais Magufuli ni mzalendo na ameonyesha dhamira ya kweli ya kulikomboa taifa kwa kupambana na mafisadi waliokuwa wananufaika na rasilimali za nchi kwa maslahi yao binafsi.


Muro aliwataka viongozi wa madhehubu hayo kufanya kazi kwa bidii ikiwemo kutumia taaluma zao kujenga uchumi badala ya kukaa na kutegemea sadaka kama sehemu ya kipato chao.


Kuhusu malalamiko yaliyowasilishwa ofisini kwake na baadhi ya wananchi juu ya makanisa yanayomea kama uyoga kwenye makazi ya watu Muro alisema ni vyema makanisa hayo yakawa na vifaa maalum vya kuzuia sauti kutoka nje ili kuepuka kusumbua watu nyakati za usiku wakati wa maombi.

Alisema kwa kipindi chake atakachokuwa mkuu wa wilaya hiyo hakuna kanisa litakalofungwa na serikali na kwamba atashirikiana na viongozi wa makanisa hayo kufanya harambee kwa ajili ya kujenga makanisa yenye vifaa maalum vya kuzuia sauti.

View attachment 1102217View attachment 1102219
Na yy asichukue mshahara wa ukuu wa wilaya......km sio kutegemea mshahara asingekua mwendwazim vile kusaka ukuu wala wilaya......sadaka ndo ujira wao km yy anavyopokea mshahara
 
Muro anaelewa kuwa viongozi wa dini ni walezi wa jamii? Wanaitwa kwenye mashauri, misiba, ugonjwa. Pamoja na hayo wana jukumu la kulea vijana. Kuna walioyaona haya asilete siasa kwenye dini.
😂😂😂😂naona unatetea ugali. Pigeni kaz .wewe utakua ni nabii na mtume Sky Eclat
 
Labda angeshauri watumie vizuri sadaka. Ila kuacha sadaka alafu waende wakafanye Kazi.
Ipo siku mtaenda kanisani alafu mkakosa mapadre wa kuwaongoza. Mkiuliza mtajibiwa wameenda kwenye mishe mishe zao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom