DC mpya wa Ikungi, Singida atumbuliwa ndani ya masaa 24

Kanyunyu

JF-Expert Member
May 2, 2012
335
495
DC mpya wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida Mwl. Fikiri Avias Saidi uteuzi wake umetenguliwa leo, ameteuliwa ndugu Miraji Mtaturu ambae alikuwa katibu wa CCM mkoani Mwanza.

Ngoma inogile.

=========

Juni 26 mwaka huu Rais John Pombe Magufuli alitangaza kuteua Wakuu wa Wilaya zote nchini, na Wakuu wa Mkoa watatu. Kati ya Wakuu wa Wilaya 139 walioteuliwa, 39 wamebakishwa katika nafasi zao huku 100 wakiwa ni wapya.

Katika hali ya kushangaza siku moja baada ya orodha hiyo kutangazwa, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa mkuu wa wilaya ya Ikungi iliyopo mkoani Singida. Rais Magufuli alitengua uteuzi wa Bwana Fikiri Avias Said ndani ya masaa 24 tangu uteuzi wake.

Sababu kuu ya Rais kutengua Uteuzi huu ameisema leo hii wakati wa hafla ya kuwaapisha Wakuu wote walioteuliwa, ni kwamba jina lilikosewa, na kusema kwamba Mkuu wa Wilaya halali wa Ikungi ni Bwana Miraji Mtaturu ambaye ni Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mwanza,
 
Magufuli ni Mkurupukaji. Lawama zote kwa Chama Cha Majipu (CCM) na JK kwa kutupatia Kiongozi wa namna hii.

Ushauri: Mh. Magufuli, kwa hulka, Silka na tabia yako, watu hawatamani kufanya kazi na wewe. Wanaoendelea hawana mbadala tu. Wakiupata watakuacha pekee yako. Nia yako ni njema lakini badili mbinu za Uongozi.
 
Tuachane na utaratibu wa ku suprise vyeo. Ndugu Kinana aliwahi kukataa nafasi ya Ukuu wa Mkoa wakat wa Jakaya, Jk akasema alijifunza tangu hapo akawa ha consult mtu akitaka kumteua, Prof Muhongo nae awali alikataa mara tatu uteuzi mpaka alipoteuliwa tena bila ya kutaarifiwa awali.
Jamaa aache shuguli zake zinazompatia kipato cha siku moja sawa na pato la DC la wiki nzima tena bila ya kunyenyekea nyenyekea wala kujipendekeza pendekeza
 
Kwan ajira zote si zimesitishwa jaman au wakuu Wa wilaya malipo yao hayatok hazina
 
Back
Top Bottom