DC,MD Na VA KUCHAGUA VIONGOZI WAPYA

houseboy

Member
Jul 22, 2007
39
3
Wabongo waishio MD,DC na VA hivi karibuni watachagua viongozi wapya baada ya viongozi wa sasa muda wao kuisha,kuna wabongo wengi wanataka kugombea nafasi mbalimbali za uongozi,uchunguzi umeonyesha uchaguzi huu utakuwa na mshikomshiko mkubwa sana baada ya kuonekana kuna makundi zaidi ya matano yote yakiwania uongozi,je ni nani ataibuka mshindi?kuna manufaa yoyote kuwa na jumuia kama hizi?.kwa nini watu sasa wanataka kugombea kuliko miaka ya nyuma.
 
Bwana Houseboy,
hapa JF we dare talk openly kwa hiyo wewe toa dukuduku lako, au at least toa details basi, chama kinaitwaje au toa url ya website yake tupate details.

Hizo point za "makundi matano", "wengi kutaka kugombea uongozi", "uchaguzi kuwa na mshikomshiko" naona zimekaa kishabikishabiki zaidi na siyo kulingana na "uchunguzi" ambao unadai umeonyesha hivyo.
 
Kama Jumuia hii ingeendeshwa kwa kufuata madhumuni yake ya awali na pia Katiba yake na kama wanachama wangeifanya Jumuia hii ni yao badala ya kuwabwagia viongozi wake, sina shaka yoyote Jumuia hii ingekuwa ya manufaa kwa wanachama wenyewe na hali kadhalika kwa Watanzania wengine kule nyumbani.

Lakini, wapi! Kama kawaida yetu, wanaoongoza hawajui wanakuongozea wala wanachokiongoza na wanaoongozwa, hawajui wanakotaka kuongozwa. Ili muradi, "bora liende." Jumuia hii, ilianzishwa, kama nakumbuka sawasawa mwaka 1990. Na mpaka leo hii,haina chochote kinachoweza kuorodheshwa, kama mafanikio yake ni majungu juu ya mafiga.

Kinachogombewa ni kutafuna vijisenti kidogo na ile sifa ya kujiita kwa cheo utakachopewa baada ya uchaguzi. Kingine, ni kule kujikomba komba na kimbele mbele, wanapokuja wakubwa kutoka nyumbani.

Hawa viongozi waliopo sio tu wamemaliza muda wao wa uongozi bali wameupitiliza. Bila ya kushinikizwa, hata huo uchaguzi wenyewe usingezungumzwa, sembuse ya kufanyika.

Cha ajabu ni kuwa hawa viongozi waliopo, ndio waliokuwa mstari wa mbele, katika kuwalaumu viongozi waliokuwa kabla yao kwa makosa hayo hayo ambao nao sasa wanaonekana kuyafanya.

Makundi ni lazima katika uchaguzi wowote. Kila mgombea mtarajiwa, anawajibika kuunda na kuwa na kundi lake la kupanga na kutekeleza mikakati yake ya kutafutia ushindi.

Nawatakia wote pamoja na Jumuia yenyewe mafanikio katika kutuletea mabadiliko yenye matumaini.
 
Kama Jumuia hii ingeendeshwa kwa kufuata madhumuni yake ya awali na pia Katiba yake na kama wanachama wangeifanya Jumuia hii ni yao badala ya kuwabwagia viongozi wake, sina shaka yoyote Jumuia hii ingekuwa ya manufaa kwa wanachama wenyewe na hali kadhalika kwa Watanzania wengine kule nyumbani.

Lakini, wapi! Kama kawaida yetu, wanaoongoza hawajui wanakuongozea wala wanachokiongoza na wanaoongozwa, hawajui wanakotaka kuongozwa. Ili muradi, "bora liende." Jumuia hii, ilianzishwa, kama nakumbuka sawasawa mwaka 1990. Na mpaka leo hii,haina chochote kinachoweza kuorodheshwa, kama mafanikio yake ni majungu juu ya mafiga.

Kinachogombewa ni kutafuna vijisenti kidogo na ile sifa ya kujiita kwa cheo utakachopewa baada ya uchaguzi. Kingine, ni kule kujikomba komba na kimbele mbele, wanapokuja wakubwa kutoka nyumbani.

Hawa viongozi waliopo sio tu wamemaliza muda wao wa uongozi bali wameupitiliza. Bila ya kushinikizwa, hata huo uchaguzi wenyewe usingezungumzwa, sembuse ya kufanyika.

Cha ajabu ni kuwa hawa viongozi waliopo, ndio waliokuwa mstari wa mbele, katika kuwalaumu viongozi waliokuwa kabla yao kwa makosa hayo hayo ambao nao sasa wanaonekana kuyafanya.

Makundi ni lazima katika uchaguzi wowote. Kila mgombea mtarajiwa, anawajibika kuunda na kuwa na kundi lake la kupanga na kutekeleza mikakati yake ya kutafutia ushindi.

Nawatakia wote pamoja na Jumuia yenyewe mafanikio katika kutuletea mabadiliko yenye matumaini.

Mimi naanzisha jumuia huko tayari kujiunga?
 
Bin Maryam, huoni kuwa una jukumu la kunifafanulia kwanza, unaanzisha Jumuia ya namna gani na kwa ajili ya nini ili niweze au nisiweze kujiunga nayo?
 
Bin Maryam, huoni kuwa una jukumu la kunifafanulia kwanza, unaanzisha Jumuia ya namna gani na kwa ajili ya nini ili niweze au nisiweze kujiunga nayo?

Samahani nimechelewa kujibu posti, unajua tena tupo kwenye siasa na jazba za BOT.
 
Bin Maryam, huoni kuwa una jukumu la kunifafanulia kwanza, unaanzisha Jumuia ya namna gani na kwa ajili ya nini ili niweze au nisiweze kujiunga nayo?

Hapa kwetu jumuia zinaanzishwa na zinakufa. Na tatizo la kufa kwa jumuia hizi ni kufuata mfumo wa Chama Cha Mapinduzi na jumuia zake. Lazima uwe mwanachama na ulipe ada. Kama Gavana wa BOT anashindwa kujizuia kuvuta uchache, je mbeba mabox mwenzangu atakunywa maji ya bendera na pesa za jumuia?

Hivyo naanzisha chama chenye kufuata Model ya maisha ya vijiji Tanzania. Uanachama wako katika jumuia ni kushiriki na pesa zako kaa nazo mwenyewe. Yakitokea matatizo jikune pale unapoweza (ON-DEMAND), wanachama wenzako wataangalia mchango. Na ukipata matatizo watakusaidia kama vile wewe ulivyo wasaidia. Na kusipokuwa na matatizo jirushe kwa kadri ya uwezo wako.
 
Back
Top Bottom