DC Kilombero apiga marufuku kwa mtu yeyote kufanya sherehe bila kibali

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,261
cd06bdb93db4d2524e9acd3c8a169b3e.jpg
Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Bw. James Ihunyo amepiga marufuku kwa mtu yeyote kufanya sherehe bila kibali kutoka kwa mtendaji wa eneo husika ikiwa pamoja na na kuuza chakula kiholela jambo litakalo saidia mavuno yaliyopatikana msimu huu kutumika kwa uangalifu na kujikinga na athari za njaa zinazoweza kujitokeza kwa msimu ujao.

Chanzo ITV channel
 
Hakuna zuio la kuuza chakula kiholela zaidi ya athari za kipindupindu tu, kauli hii ni ya uoga tu
 
kuuza chakula kiholela jambo litakalo saidia mavuno yaliyopatikana msimu huu kutumika kwa uangalifu na kujikinga na athari za njaa zinazoweza kujitokeza kwa msimu ujao.
Hapa ndio sijamuelewa, anataka watu wasiwe na chakula?!
 
Kulima walime wenyewe

Kypanda wapande wenyewe

Kuuza muwapangie

Kwenye sherehe muwaelimishe wananchi kuwa kawaida vinahitaji kibali.....sema wengi hufanya kienyeji tu
 
Hapa ndio sijamuelewa, anataka watu wasiwe na chakula?!
Hapo maana yao ni kuhifadhi chakula.

Kwa mtazamo wao ni kuwa kuuza chakula kiholela au kufanya sherehe kupika chakula kingi kutasababisha kuwepo na njaa

Haya matamko hayana mshiko Kwakweli
 
Hapo maana yao ni kuhifadhi chakula.

Kwa mtazamo wao ni kuwa kuuza chakula kiholela au kufanya sherehe kupika chakula kingi kutasababisha kuwepo na njaa

Haya matamko hayana mshiko Kwakweli
Hapa naona ni kuingilia maisha binafsi. Hivi vyuo vya kilimo kwanini visiwe na maeneo ya kutosha na kulima kwa kiasi kikubwa?! Hii naona ni mojawapo ya njia ambayo ingesaidia baada ya mavuno wangeuza, sasa mtu alime we umkomalie mipango...
 
cd06bdb93db4d2524e9acd3c8a169b3e.jpg
Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Bw. James Ihunyo amepiga marufuku kwa mtu yeyote kufanya sherehe bila kibali kutoka kwa mtendaji wa eneo husika ikiwa pamoja na na kuuza chakula kiholela jambo litakalo saidia mavuno yaliyopatikana msimu huu kutumika kwa uangalifu na kujikinga na athari za njaa zinazoweza kujitokeza kwa msimu ujao.

Chanzo ITV channel
Achukuliwe mkojo;!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Safi, shughuri ni nyingi hadi watoto hawaendi shule...

Angalau wapate kabarua ka kupiga mziki mtaani, watasaidia kupunguza sherehe zisizo za lazima..DC safiii!!...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom