SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 43,714
- 60,721
Nadhani DC Jerry Muro ameshaichoka hiyo Nafasi aliyonayo, kwani kwa Maelezo yake haya sidhani kama yakimfikia Rais JPM atabakia kuwa DC.
Anamsingizia Mh. Rais, ukweli Rais hajawakataza kukomesha kilimo cha bangi, alichosema ni kuwa wakikuta shamba la bangi wawalazimishe wananchi wa eneo hilo kuifyeka na kuiharibu bangi hiyo na kamwe kazi hiyo isifanywe na askari wetu.
Jerry Muro hawezi kukwepa kikombe hicho kwani yeye ndiye mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama Wilayani kwake,sasa kama Kamati nzima imeboronga hadi Mh. Rais kuamua itumbuliwe yeye anaponaje hapo?