Mkuu madaraka ni matamu. Hebu fikiria uatoa tu "tamko weka ndani" OCD anakupigia saluti mtu anaswekwa rumande bila hata kuchukuliwa maelezo.Lengo la maelezo haya yote ni Nini hasa wakati unayo mamlaka ya Kamata weka ndani?
Pili kazi iliyokupeleka uliifanya kwa capacity ipi? Kamati ya usuluishi? Wajumbe wake ni kina Nani? Je ulikua na instruments zipi kukufanya itekeleze jukumu Hilo? Kuingia kwenye makazi ya mtu hata Kama wewe ni kiongozi Kama huna Ruhusu ni kosa. Hujuwa na RB Wala sijui warrant ya mahakama au polisi kwa vyovyote walikua na haki ya kutokukusikiliza Wala kukukaribisha kwenye makazi yao.
Mama alisema " ukinizingua tutazinguana" lakini pia alisema " sijakuchagua uende ukawapandishie mabega"
Mh. Jipime Kama unatosha kwenye hiyo nafasi, jishushe kwa kujiuzulu. Kama mama itapendeza atakurudisha au kukupa kazi ingine Biblia inasema " ajikwezae atashushwa"