Egnecious
JF-Expert Member
- Jul 8, 2015
- 875
- 960
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi leo ametoa zawadi ya mchele, nyama, mafuta ya kupikia na maharagwe kwa watumishi wa ngazi za chini wakiwemo madereva, makarani na wahudumu kama shukrani ya utumishi wao katika mwaka huu unaoisha wa 2016 na sikukuu za Xmas na Mwaka mpya ujao.
"Mimi na Mkurugenzi tunawashukuru sana kwa utumishi wenu kwa kipindi chote tangu tulipoteuliwa kuja hapa, hasa nyinyi wafanyakazi wa ngazi za chini. Bila nyinyi tusingefanikiwa. Mna mchango mkubwa katika kuifikisha Kinondoni hapa ilipo sasa. Endeleeni na moyo huo wa upendo. Mungu awabariki sana."
Alisema Mkuu wa Wilaya.
"Mimi na Mkurugenzi tunawashukuru sana kwa utumishi wenu kwa kipindi chote tangu tulipoteuliwa kuja hapa, hasa nyinyi wafanyakazi wa ngazi za chini. Bila nyinyi tusingefanikiwa. Mna mchango mkubwa katika kuifikisha Kinondoni hapa ilipo sasa. Endeleeni na moyo huo wa upendo. Mungu awabariki sana."
Alisema Mkuu wa Wilaya.