OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,187
- 103,707
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Siriel Mchembe amelazimika kupiga marufuku Wanandoa wa Wilaya hiyo kuacha kusoma msg kwenye simu za wenzao ili kuepusha migogoro na vifo vitokanavyo na wivu wa kimapenzi, ameyasema haya kwenye maziko ya Kijana wa miaka 35 aliyeuwawa kwa kukatwa mapanga na kuchomwa visu kutokana na wivu wa mapenzi.
Wazazi wa Kijana huyu wamesema Mtoto wao ni kweli alishawahi kufumaniwa na Mwanamke wa Mtu lakini baadae alimlipa Mume wa Mwanamke huyo shilingi laki sita ili asamehe tukio hilo lakini sasa imewashangaza Mtoto wao kuuwawa kinyama.
Mama mzazi wa Marehemu amesema Mwanamke huyo alimwambia Mtoto wake kuwa hana Mume na hata baada ya kufumaniwa Mwanamke huyo aliendelea kumfatafata Marehemu
"Nilimwambia sikutaki wewe Mtoto lakini bado anakuja, anamletea Mwanangu majanga, naomba Serikali inisaidie waliomuua Mwanangu" ——— amesema Mama wa Marehemu.
Wazazi wa Kijana huyu wamesema Mtoto wao ni kweli alishawahi kufumaniwa na Mwanamke wa Mtu lakini baadae alimlipa Mume wa Mwanamke huyo shilingi laki sita ili asamehe tukio hilo lakini sasa imewashangaza Mtoto wao kuuwawa kinyama.
Mama mzazi wa Marehemu amesema Mwanamke huyo alimwambia Mtoto wake kuwa hana Mume na hata baada ya kufumaniwa Mwanamke huyo aliendelea kumfatafata Marehemu
"Nilimwambia sikutaki wewe Mtoto lakini bado anakuja, anamletea Mwanangu majanga, naomba Serikali inisaidie waliomuua Mwanangu" ——— amesema Mama wa Marehemu.