DC Gondwe aagiza Wanafunzi watatu wafukuzwe Shule kwa kujihusisha na vitendo viovu

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Godwin Gondwe, ameagiza kufukuzwa kwa wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Toangoma iliyopo wilayani Temeke, Dar es Salaam kwa kosa la kujihusisha na vitendo viovu (ngono) ambapo ni kinyume na maadili ya shule.

Gondwe ametoa agizo hilo leo alipotembelea shule hiyo kwa lengo la kutaka kupata ukweli wa kile kilichoripotiwa na vyombo vya habari siku chache zilizopita kuhusiana na kukithiri kwa vitendo vya ngono katika shule hiyo, huku akiutaka Uongozi wa Shule hiyo pamoja na Uongozi wa Kata, kuchukua hatua za haraka kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimeonekana kukithiri shuleni hapo.

Aidha, Gondwe ameagiza kupigwa kwa kura ya siri kwa kila darasa ili kuwabaini wanafunzi wote wanaojihusisha na vitendo hivyo na baada ya kuwabaini wafanyiwe uchunguzi wa kitabibu kuthibitisha tuhuma hizo na wakithibitika wazazi wao wapewe taarifa na hatua kali za kisheria zichukuliwe ikiwemo kuondolewa shuleni.

Gondwe ametoa siku saba kwa uongozi wa shule na wa Kata ikishirikiana na uongozi wa Mtaa kuweka mikakati ya pamoja ili kuangalia njia ya kutokomeza vitendo hivyo.

Chanzo: IPP Media
 
Kwa mtazamo wangu kuwafukuza haiwezi kuwa tiba kwa vijana hao. Bado wadogo sana na hawafanyi mambo kwa utashi bali kwa msukumo wa miili yao. Nusara zaidi inatakiwa kutumika kwenye hili kwa manufaa ya watoto hao ikiwezekana hata kuwahamisha shule kuwapeleka shule zingine huku wakiwa chini ya uangalizi.
 
Nchi ya kusadikika always watawala wake wana maamuzi ya mihemko,huyu DC amewafukuza shule kwa kutumia sheria gani?lini nchi yetu utawala bora utatamalaki?kabla ya kujiuliza why kuna tatizo hili DC amekimbilia tulikoangukia sio tulipojikwaa, tuelewe ni haki ya kikatiba kwa kila mtoto kupata ELIMU sio fukuza fukuza isiyoleta tija.

Nina hasira mno hasa nikikumbuka kilichotokea Mkwawa CNE baada ya principal Mshana kuondolewa kwa majungu na kuletwa principal mpya ambaye yeye maamuzi yote ya kwake ilikuwa ni kufukuza tu na akasahau kuwa kuna kitu kinaitwa Karma na kilichotokea yeye alifukuzwa pia tena alifukuzwa duniani sio chuoni!
 
Mabinti wapimwe kama wametumika kitu ambacho ni rahisi,

ila vijana wa kiume nao watapimwa kwa kutumia kipimo gani kujua kuwa wametumia
 
Kila siku nasema wazazi ndiyo wanaharibu watoto.

Ona Sasa wanafanya ngono wadogo kabsa

Mzaz anaona lakin anakula buyu Kama vile mkubwa mwenzake

Ndiyo jamii tunayotengeneza.

Kosa lilitokea pale walipokataza hakuna kumchapa mtoto fimbo.

Mtavuna mlicho panda
 
mabinti wapimwe kama wametumika kitu ambacho ni rahisi,

ila vijana wa kiume nao watapimwa kwa kutumia kipimo gani kujua kuwa wametumia
Ndiyo maana vijana wanakosa bikra kumbe ilisha tolewa siku nying Sana
 
What about looking at the root cause of the problem?Talking to the parents,teachers,looking at how these kids are being raised up?
As bad as this thing is, kumfukuza mtoto shule sio suhluhisho maana wataenda nyumbani,watakutana na watoto wengine wataendeleza hayo mambo. Mbaya zaidi kama ni familia za maisha ya chini,huo ndio utakua mwisho wa ndoto zao za elimu.Matokeo yake? Vibaka ,wavuta bangi na wahuni.

Elimu ni zaidi ya masomo ya darasani, wazazi na walimu wangepewa nafasi ya kukaa na watoto kuongea nao kuwaonya na kuweka namna ya kuwalinda kabla ya uamuzi wa kuwafukuza.

Anyways nawaonea huruma hawa watoto,I hope they get the HELP they deserve.

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
 
Kuna uzi ulitupiwa humu mapema leo kuhusu wanafunzi wa shule hiyo ya tuangoma..
Itakuwa jamaa walipitia humu na waliuona
Na wakafanya kazi

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom