DC aumbuka kumfukuza diwani wa CHADEMA jukwaani

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
MKUU wa Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, Meja mstaafu Bahati Matala, nusura avuruge kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru yaliyofanyika wilayani hapa, baada ya kumtimua jukwaani Diwani wa Kata ya Majengo (Chadema), Bobson Wambura, hali iliyopingwa na wafuasi wa chama hicho. Sakata hilo lililotokea juzi saa 5:00 asubuhi kwenye uwanja wa halmashauri ya wilaya, Matala alipanda jukwaani na kuanza kuwatambulisha viongozi waliojumuika akiwamo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Masanje, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri, Eliza Bwana na Mwenyekiti wa halmashauri, Alfred Mhanganya.

Matala baada ya kumwona diwani huyo akiwa amekaa na viongozi hao jukwaani, kwa kutumia kipaza alitangaza akimtaka Wambura kuondoka mara moja. “Bobson ondoka jukwaani mara moja,” alifoka Matala. Hatua hiyo iliwakasirisha watu wengi waliokuwa wamehudhuria na kuanza kuguna, hali ambayo ilitulizwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Masanje ambaye alichukua kipaza sauti haraka kutoka kwa Matala, huku akimtaka diwani huyo kurejea mara moja jukwaani na kusalimia wananchi.

“Bobson tafadhali rudi uwasalimie wananchi wako, sioni sababu ya kumfukuza diwani wa Chadema kwenye jukwaa hili, leo tunasherekea miaka 50 ya uhuru wakati mwaka 1961 tunajitawala, uhuru ulikuwa wa Watanzania wote siyo Chadema wala CCM, sherehe hizi ni za watu wote,” alisema Masanje huku akishangiliwa na wananchi. Licha ya Masanje kupinga uamuzi wa mkuu huyo wa wilaya, alirudia tena upya utambulisho wa madiwani wote akiwataka wasimame na kuwapungia mkono wananchi.

“Waheshimiwa madiwani popote mlipo pamoja na Bobson simameni muwapungie mikono wananchi,” alisema Matala.Akizungumzia hatua hiyo, baada ya kumalizika kwa sherehe hizo, Wambura alisema alisikitishwa na kitendo cha mkuu wa wilaya kumfukuza jukwaani, ilhali maadhimisho hayo yalikuwa yanafanyika kwenye eneo lake na kwamba, atafikisha suala hilo kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, utoaji zawadi kwenye kada mbalimbali zilizoshiriki maadhimisho hayo nusura uingie dosari baada ya mwanamke mmoja, kuangua kilio mbele ya mgeni rasmi kutokana na kuchakachuliwa kwa zawadi yake ya Sh100,000 aliyoahidiwa kwa kushinda mbio za baiskeli upande wa wanawake.

Kilio hicho kilianza baada ya Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Kapteni mstaafu James Yamungu, kutangaza Sh50,000 iliyomfanya mwanamke huyo kupinga na kuangua kilio.Baada ya kuona hali hiyo Yamungu alitaka kuongeza fedha yake kuokoa jahazi, lakini Katibu Tawala Wilaya ya Kahama, Orest Mushi, alianzisha mchango wa papo kwa hapo.


Source: Mwananchi
 
Katika hali ya kuonyesha chuki na ubaguzi wa hali ya juu, DC wa Shinyanga Meja Bahati Matata amtimua katika jukwaa Diwani wa Kata ya Majengo (Chadema), Bobson Wambura. Jamani, tunaelekea wapi ?

Pata habari kamili :
MKUU wa Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, Meja mstaafu Bahati Matala, nusura avuruge kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru yaliyofanyika wilayani hapa, baada ya kumtimua jukwaani Diwani wa Kata ya Majengo (Chadema), Bobson Wambura, hali iliyopingwa na wafuasi wa chama hicho.

Sakata hilo lililotokea juzi saa 5:00 asubuhi kwenye uwanja wa halmashauri ya wilaya, Matala alipanda jukwaani na kuanza kuwatambulisha viongozi waliojumuika akiwamo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Masanje, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri, Eliza Bwana na Mwenyekiti wa halmashauri, Alfred Mhanganya.

Matala baada ya kumwona diwani huyo akiwa amekaa na viongozi hao jukwaani, kwa kutumia kipaza alitangaza akimtaka Wambura kuondoka mara moja.

“Bobson ondoka jukwaani mara moja,” alifoka Matala. Hatua hiyo iliwakasirisha watu wengi waliokuwa wamehudhuria na kuanza kuguna, hali ambayo ilitulizwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Masanje ambaye alichukua kipaza sauti haraka kutoka kwa Matala, huku akimtaka diwani huyo kurejea mara moja jukwaani na kusalimia wananchi.

“Bobson tafadhali rudi uwasalimie wananchi wako, sioni sababu ya kumfukuza diwani wa Chadema kwenye jukwaa hili, leo tunasherekea miaka 50 ya uhuru wakati mwaka 1961 tunajitawala, uhuru ulikuwa wa Watanzania wote siyo Chadema wala CCM, sherehe hizi ni za watu wote,” alisema Masanje huku akishangiliwa na wananchi.
Licha ya Masanje kupinga uamuzi wa mkuu huyo wa wilaya, alirudia tena upya utambulisho wa madiwani wote akiwataka wasimame na kuwapungia mkono wananchi.

“Waheshimiwa madiwani popote mlipo pamoja na Bobson simameni muwapungie mikono wananchi,” alisema Matala.Akizungumzia hatua hiyo, baada ya kumalizika kwa sherehe hizo, Wambura alisema alisikitishwa na kitendo cha mkuu wa wilaya kumfukuza jukwaani, ilhali maadhimisho hayo yalikuwa yanafanyika kwenye eneo lake na kwamba, atafikisha suala hilo kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, utoaji zawadi kwenye kada mbalimbali zilizoshiriki maadhimisho hayo nusura uingie dosari baada ya mwanamke mmoja, kuangua kilio mbele ya mgeni rasmi kutokana na kuchakachuliwa kwa zawadi yake ya Sh100,000 aliyoahidiwa kwa kushinda mbio za baiskeli upande wa wanawake.

Kilio hicho kilianza baada ya Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Kapteni mstaafu James Yamungu, kutangaza Sh50,000 iliyomfanya mwanamke huyo kupinga na kuangua kilio.Baada ya kuona hali hiyo Yamungu alitaka kuongeza fedha yake kuokoa jahazi, lakini Katibu Tawala Wilaya ya Kahama, Orest Mushi, alianzisha mchango wa papo kwa hapo.
Habari hii imeandikwa na gazeti la Mwananchi.
DC amtimua jukwaani diwani wa Chadema
 
Meja mstaafu ni mkuu wa wilaya na kapteni mstaafu ni mkuu wa mkoa na luteni mstaafu ni waziri. Ni mwendo wa amri kwa amri
 
Ninawasiwasi mkubwa kuwa hizi zawadi za uDC na uRC wanapewa watu wasiostahili kabisa na kutofahamu majukumu yao. Haikuhitaji kwenda shule ili kuwa na busara kwenye hili. Inaonyesha jinsi wanavyowachukulia wapinzani ni wahalifu. Diwani anachaguliwa na anatambulika kikatiba, DC /RC sijajua wapo kwa mujibu upi.
 
MKUU wa Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, Meja mstaafu Bahati Matala, nusura avuruge kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru yaliyofanyika wilayani hapa, baada ya kumtimua jukwaani Diwani wa Kata ya Majengo (Chadema), Bobson Wambura, hali iliyopingwa na wafuasi wa chama hicho. Sakata hilo lililotokea juzi saa 5:00 asubuhi kwenye uwanja wa halmashauri ya wilaya, Matala alipanda jukwaani na kuanza kuwatambulisha viongozi waliojumuika akiwamo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Masanje, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri, Eliza Bwana na Mwenyekiti wa halmashauri, Alfred Mhanganya.

Matala baada ya kumwona diwani huyo akiwa amekaa na viongozi hao jukwaani, kwa kutumia kipaza alitangaza akimtaka Wambura kuondoka mara moja. “Bobson ondoka jukwaani mara moja,” alifoka Matala. Hatua hiyo iliwakasirisha watu wengi waliokuwa wamehudhuria na kuanza kuguna, hali ambayo ilitulizwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Masanje ambaye alichukua kipaza sauti haraka kutoka kwa Matala, huku akimtaka diwani huyo kurejea mara moja jukwaani na kusalimia wananchi.

“Bobson tafadhali rudi uwasalimie wananchi wako, sioni sababu ya kumfukuza diwani wa Chadema kwenye jukwaa hili, leo tunasherekea miaka 50 ya uhuru wakati mwaka 1961 tunajitawala, uhuru ulikuwa wa Watanzania wote siyo Chadema wala CCM, sherehe hizi ni za watu wote,” alisema Masanje huku akishangiliwa na wananchi. Licha ya Masanje kupinga uamuzi wa mkuu huyo wa wilaya, alirudia tena upya utambulisho wa madiwani wote akiwataka wasimame na kuwapungia mkono wananchi.

“Waheshimiwa madiwani popote mlipo pamoja na Bobson simameni muwapungie mikono wananchi,” alisema Matala.Akizungumzia hatua hiyo, baada ya kumalizika kwa sherehe hizo, Wambura alisema alisikitishwa na kitendo cha mkuu wa wilaya kumfukuza jukwaani, ilhali maadhimisho hayo yalikuwa yanafanyika kwenye eneo lake na kwamba, atafikisha suala hilo kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, utoaji zawadi kwenye kada mbalimbali zilizoshiriki maadhimisho hayo nusura uingie dosari baada ya mwanamke mmoja, kuangua kilio mbele ya mgeni rasmi kutokana na kuchakachuliwa kwa zawadi yake ya Sh100,000 aliyoahidiwa kwa kushinda mbio za baiskeli upande wa wanawake.

Kilio hicho kilianza baada ya Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Kapteni mstaafu James Yamungu, kutangaza Sh50,000 iliyomfanya mwanamke huyo kupinga na kuangua kilio.Baada ya kuona hali hiyo Yamungu alitaka kuongeza fedha yake kuokoa jahazi, lakini Katibu Tawala Wilaya ya Kahama, Orest Mushi, alianzisha mchango wa papo kwa hapo.


Source: Mwananchi

DC = DoaChangu
 
Habari za ndani ni kwamba Bobson ni maarufu sana hapa Kahama na alikuwa kaandaa maandamano ya kumpinga mkuu huyo wa Wilaya kwa kuchakachua mahindi ya msaada
 
Hivi vyeo vya Ukuu wa Mikoa na Wilaya ni byeo vya KISIASA hapa nchini kwetu au ni vyeo vya KI-UTUMISHI wa kiserikali kuhudumia wananchi wote bila kuendeleza misingi fulani fulani za kisiasa??????????

Kwa mambo kama haya na yale yaliotokea kule Igunga, inabidi watu tufike mahala tuone sababu KUFANYA VYEO HIVI VIWE VYA KIUTUMISHI ZAIDI, watu kutuma maombi ya kazi kiushindani kama kazi nyinginezo ili tuondokane kabisa na hawa watu wenye kuwakera wananchi kiasi hiki.
 
matala ni miongoni mwa ma dc wapumbavu sana.hana upeo hana akili..jimewahi kuganya naye kazi nikiwa buzwagi mine..he is bogus
 
Wakipata funzo kutoka kwa wananchi, tunaisingizia cdm! Mkuu wa wilaya mpumbavu namna hii wananchi wanaweza kumchukulia hatua gani wakati hawamfahamu wala hawajui alipowatokea zaidi ya kuambiwa tu ameteuliwa na rais. Tafakari...
 
MaDC wengine bwana! Wanaendelea kucheza ngoma ya CCM ambayo mdundo wake ulishaisha siku nyingi.
 
Nadhani dawa iwe ileile aliyopewa Kimario kule Igunga ndio watajua wanapaswa kutenda kwa haki dhidi ya waajiri wao ambao ni wananchi na si CCM
 
MKUU wa Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, Meja mstaafu Bahati Matala, nusura avuruge kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru yaliyofanyika wilayani hapa, baada ya kumtimua jukwaani Diwani wa Kata ya Majengo (Chadema), Bobson Wambura, hali iliyopingwa na wafuasi wa chama hicho. Sakata hilo lililotokea juzi saa 5:00 asubuhi kwenye uwanja wa halmashauri ya wilaya, Matala alipanda jukwaani na kuanza kuwatambulisha viongozi waliojumuika akiwamo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Masanje, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri, Eliza Bwana na Mwenyekiti wa halmashauri, Alfred Mhanganya.

Matala baada ya kumwona diwani huyo akiwa amekaa na viongozi hao jukwaani, kwa kutumia kipaza alitangaza akimtaka Wambura kuondoka mara moja. “Bobson ondoka jukwaani mara moja,” alifoka Matala. Hatua hiyo iliwakasirisha watu wengi waliokuwa wamehudhuria na kuanza kuguna, hali ambayo ilitulizwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Masanje ambaye alichukua kipaza sauti haraka kutoka kwa Matala, huku akimtaka diwani huyo kurejea mara moja jukwaani na kusalimia wananchi.

“Bobson tafadhali rudi uwasalimie wananchi wako, sioni sababu ya kumfukuza diwani wa Chadema kwenye jukwaa hili, leo tunasherekea miaka 50 ya uhuru wakati mwaka 1961 tunajitawala, uhuru ulikuwa wa Watanzania wote siyo Chadema wala CCM, sherehe hizi ni za watu wote,” alisema Masanje huku akishangiliwa na wananchi. Licha ya Masanje kupinga uamuzi wa mkuu huyo wa wilaya, alirudia tena upya utambulisho wa madiwani wote akiwataka wasimame na kuwapungia mkono wananchi.

“Waheshimiwa madiwani popote mlipo pamoja na Bobson simameni muwapungie mikono wananchi,” alisema Matala.Akizungumzia hatua hiyo, baada ya kumalizika kwa sherehe hizo, Wambura alisema alisikitishwa na kitendo cha mkuu wa wilaya kumfukuza jukwaani, ilhali maadhimisho hayo yalikuwa yanafanyika kwenye eneo lake na kwamba, atafikisha suala hilo kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, utoaji zawadi kwenye kada mbalimbali zilizoshiriki maadhimisho hayo nusura uingie dosari baada ya mwanamke mmoja, kuangua kilio mbele ya mgeni rasmi kutokana na kuchakachuliwa kwa zawadi yake ya Sh100,000 aliyoahidiwa kwa kushinda mbio za baiskeli upande wa wanawake.

Kilio hicho kilianza baada ya Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Kapteni mstaafu James Yamungu, kutangaza Sh50,000 iliyomfanya mwanamke huyo kupinga na kuangua kilio.Baada ya kuona hali hiyo Yamungu alitaka kuongeza fedha yake kuokoa jahazi, lakini Katibu Tawala Wilaya ya Kahama, Orest Mushi, alianzisha mchango wa papo kwa hapo.


Source: Mwananchi

Nashindwa kuelewa hawa Ma-DC wanafanya kazi kwa maslahi ya nani kwa kweli,wako pale kulinda maslahi ya chama au wananchi,kisa nini mpaka amfukuze diwani wa CDM...huu ni uchafu wa wazi na udhalilishaji ambao nilitegemea DC akamatwe haojiwe kwanini anamdhalilisha kiongozi aliyechaguliwa na wananchi wakati yeye kateuliwa na Raisi tena kimagumashi magumashi....Viongozi wa CCM wanapaswa kufahamu ipo siku watatoka madarakani,na wanayoyafanya kwa wananchi sasa watafanyiwa pia baada ya chama kingine kuingia madarakani..tuwe na nidhamu kabla atujapewa nidhamu kwa lazima...Huyu mkuu wa wilaya anahitaji kipigo cha kumnyoosha adabu...
 
Back
Top Bottom