Behaviourist
JF-Expert Member
- Apr 8, 2016
- 39,901
- 95,404
Katika hali ya kustaajabisha, DC wa Arusha Kenani Kihongosi ambae aliwahi kutoa 'Singo' niliyoambatanisha hapo chini ya kumsifia Magufuli kwa kudai kuwa Magufuli alikuwa ni jembe la kila kitu aibuka na kudai kuwa Magufuli alikuwa ni fisadi.
Anadai kuwa katika awamu hiyo Serikali ilikuwa haiweki wazi kuwa imekopa nini na kwa matumizi gani.
Kilichonifanya nilete huu uzi siyo tu kumshangaa Bwana huyu bali nataka niweke wazi kuwa Tanzania hatuendelei kwa sababu ya kuwa na viongozi wanafiki.
Anachomaanisha huyu Bwana ni kwamba alikuwa anajua kabisa kuwa Magufuli alikuwa ni fisadi lakini hakusema kipindi Magufuli akiwa hai ili kulinda ugali wake.
Katika Mataifa yaliyo serious viongozi huweka misimamo yao mbele kwa maendeleo ya Taifa.Viongozi huwa wapo tayari kujiuzulu au kufukuzwa kazi kwa maslahi mapana ya Taifa.
Lakini huku kwetu ni tofauti.Viongozi wapo tayari kutetea ujinga,ufisadi,wizi,mauaji,ukandamizaji wa wananchi na kadhalika ili kulinda ugali wao.Hapa Tanzania viongozi wapo tayari kumtetea kiongozi aliebadilika kuwa kichaa au mwendawazimu ili kulinda nyadhifa zao.
Katika hali kama hii usitegemee Taifa kuendelea kamwe.Hii ni kwa sababu pale kiongozi anapoamua kubadilika kuwa fisadi,mwizi,mkandamizaji au hata kichaa basi hulindwa na chama chake pamoja na viongozi wengine waliopo madarakani ambao lengo lao ni kulinda nyadhifa zao na wala siyo kutetea maslahi mapana ya Taifa.
CCM kwa miaka mingi imekuwa ikitoa viongozi wa aina ya huyu Bwana na ndiyo maana Tanzania miaka nenda haiendelei.Ni muda muafaka sasa CCM kukaa pembeni ili kupisha vyama vingine vya siasa ambavyo vina maono pamoja na nia ya dhati ya kulikomboa Taifa hili.
Anadai kuwa katika awamu hiyo Serikali ilikuwa haiweki wazi kuwa imekopa nini na kwa matumizi gani.
Kilichonifanya nilete huu uzi siyo tu kumshangaa Bwana huyu bali nataka niweke wazi kuwa Tanzania hatuendelei kwa sababu ya kuwa na viongozi wanafiki.
Anachomaanisha huyu Bwana ni kwamba alikuwa anajua kabisa kuwa Magufuli alikuwa ni fisadi lakini hakusema kipindi Magufuli akiwa hai ili kulinda ugali wake.
Katika Mataifa yaliyo serious viongozi huweka misimamo yao mbele kwa maendeleo ya Taifa.Viongozi huwa wapo tayari kujiuzulu au kufukuzwa kazi kwa maslahi mapana ya Taifa.
Lakini huku kwetu ni tofauti.Viongozi wapo tayari kutetea ujinga,ufisadi,wizi,mauaji,ukandamizaji wa wananchi na kadhalika ili kulinda ugali wao.Hapa Tanzania viongozi wapo tayari kumtetea kiongozi aliebadilika kuwa kichaa au mwendawazimu ili kulinda nyadhifa zao.
Katika hali kama hii usitegemee Taifa kuendelea kamwe.Hii ni kwa sababu pale kiongozi anapoamua kubadilika kuwa fisadi,mwizi,mkandamizaji au hata kichaa basi hulindwa na chama chake pamoja na viongozi wengine waliopo madarakani ambao lengo lao ni kulinda nyadhifa zao na wala siyo kutetea maslahi mapana ya Taifa.
CCM kwa miaka mingi imekuwa ikitoa viongozi wa aina ya huyu Bwana na ndiyo maana Tanzania miaka nenda haiendelei.Ni muda muafaka sasa CCM kukaa pembeni ili kupisha vyama vingine vya siasa ambavyo vina maono pamoja na nia ya dhati ya kulikomboa Taifa hili.