DC Amsweka ndani mwanasheria Arusha sakata la hotel Ngurdoto

Waziri2025

Senior Member
Sep 2, 2019
148
379
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amemfanyia umafya wa hali ya juu mwanasheria Msomi na wakili wa kujitegemea, Edmund Ngemela kwa kosa la kumtetea mwajiri sakata la wafanyakazi wa Hotel ya Ngurdoto.

DC Muro alifika katika hotel hiyo na kuzungumza na wafanyakazi ambao baadhi yao walipatiwa barua ya kupunguzwa kazi,na baada ya kuwasikiliza alimtaka wakili huyo kueleza undani wa sakata hilo.

Hata hivyo Muro alionyesha kutoridhika na maelezo ya wakili huyo na baada ya kumalizika kwa kikao hicho alimwamuru wakili huyo kuongozana naye hadi kituo cha polisi USA River.

Baada ya kufika DC Muro alimpeleke kaunta ya Polisi na kumwagiza askari waliokuwepo hapo kumweka ndani hadi hapo atakapojisikia kumtoa.

Hata hivyo wakili huyo baadaye aliwasiliana na wanasheria wenzake na kuweza kutoka mahabusu baada ya Masaa kadhaa kusota Lukapu .

DC Muro alimtaka mwanasheria huyo kusitisha barua za kuwafukuza kazi wafanyakazi 50 wa hotel hiyo ,huku Wakili Ngemela akimwambia DC huyo kwamba hana mamlaka ya kisheria ya kuamuru mwajiri kutomfukuza mfanyakazi wake ila mwenye mamlaka ni tume ya usuluhishi (CMA) ama mahakama.

Wakili Ngemela anaitetea kampuni ya Ngurdoto katika kesi ya madai ya wafanyakazi walioipeleka mahakamani hotel hiyo wakidai malimbikizo ya mshahara.
 
Wekeni mkatab awa Barick hadharani.

Vp ule mtambo wa kuchenjua makinikia unafanya kazi? Au bado mnaendelea na upembuzi yakinifu?

Na makinikia? Nasikia hamsafirishi tena kwenda ng'ambo..yale yaliyokuwa pale bandarini mmerudisha Kahama?
Sijui Mataga watakuelewa,
Zama za kina Jery Muro zimeisha waanze kukabidhi ofisi.
 
Sijui Mataga watakuelewa,
Zama za kina Jery Muro zimeisha waanze kukabidhi ofisi.
Wanajidai kisa maafisa kipenyo wanajua wana back up ...ya kitengo wapumbavu sanaa zama hizi sio zao
 
Kisheria mwanasheria hawezi kuwa sehemu ya anachotete kwa kuwa tu anatetea mtuhumiwa.

Ifike mahala sheria hii iondolewe au iwe ni ruhusa vyombo vya dola kushitakiwa kwa matendo yao!! Haki nyingi katika nchi masikini hazipatikani kwa sababu walio na mamlaka, wamepewa pia mamlaka ya kuvunja haki za watu bila kushitakiwa!!
 
Ila mama Samia aangalie asije kugeuka kasuku aimbaye wimbo mzuri lakini hauna matokeo.

Hawa vijana ni kama walivutishwa bange na mwendazake na hawajali kwenda na hisia zake au maagizo yake.

Hata Spika Ndugai ni kama bado anaamini Magufuli amelala tuu ataamka na Samia ni yuleyule Makamu wa Rais ambaye Magu alikuwa anamsifia "mnamuona mweupe na mzuri?" hivyo hambabaishi.

Bila kuwafyeka watendaji kama hao huyu mama ataaibika pamoja na nia yake nzuri
 
DC Muro alimtaka mwanasheria huyo kusitisha barua za kuwafukuza kazi wafanyakazi 50 wa hotel hiyo ,huku Wakili Ngemela akimwambia DC huyo kwamba hana mamlaka ya kisheria ya kuamuru mwajiri kutomfukuza mfanyakazi wake ila mwenye mamlaka ni tume ya usuluhishi (CMA) ama mahakama.
Duh Muro kaingia cha kike! Kujua sharia raha sana
 
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amemfanyia umafya wa hali ya juu mwanasheria Msomi na wakili wa kujitegemea, Edmund Ngemela kwa kosa la kumtetea mwajiri sakata la wafanyakazi wa Hotel ya Ngurdoto.

DC Muro alifika katika hotel hiyo na kuzungumza na wafanyakazi ambao baadhi yao walipatiwa barua ya kupunguzwa kazi,na baada ya kuwasikiliza alimtaka wakili huyo kueleza undani wa sakata hilo.

Hata hivyo Muro alionyesha kutoridhika na maelezo ya wakili huyo na baada ya kumalizika kwa kikao hicho alimwamuru wakili huyo kuongozana naye hadi kituo cha polisi USA River.

Baada ya kufika DC Muro alimpeleke kaunta ya Polisi na kumwagiza askari waliokuwepo hapo kumweka ndani hadi hapo atakapojisikia kumtoa.

Hata hivyo wakili huyo baadaye aliwasiliana na wanasheria wenzake na kuweza kutoka mahabusu baada ya Masaa kadhaa kusota Lukapu .

DC Muro alimtaka mwanasheria huyo kusitisha barua za kuwafukuza kazi wafanyakazi 50 wa hotel hiyo ,huku Wakili Ngemela akimwambia DC huyo kwamba hana mamlaka ya kisheria ya kuamuru mwajiri kutomfukuza mfanyakazi wake ila mwenye mamlaka ni tume ya usuluhishi (CMA) ama mahakama.

Wakili Ngemela anaitetea kampuni ya Ngurdoto katika kesi ya madai ya wafanyakazi walioipeleka mahakamani hotel hiyo wakidai malimbikizo ya mshahara.
Kwenye administrative law imewekwa wazi kwamba mtu yeyote anayefanya kazi kwa niaba ya serikali chochote anachokifanya lazima akifanye within the authority of the law otherwise, that person acts arbitrarily (ultra vires).
 
Unapoongea jambo ni lazima uwe na uhakika nalo. Je Lissu aliwatetea Accasia kwa kesi ipi na hiyo kesi ni namba ngapi na ya mwaka gani na iliendeshwa na Mahakama ipi? Au umeamua kuropoka kwa kuwa unamchukia Lissu?
Mkuu na waliolike. Je nimemtaja Lissu?
 
Back
Top Bottom