BADO MMOJA
JF-Expert Member
- Jul 19, 2012
- 2,196
- 1,338
Habari kutoka wilaya ya Bukombe zinaeleza kuwa Tabibu wa zamu Johaness Makobwe katika hospitali ya wilaya ya Bukombe amekataa kumtibu mgonjwa aliyefika hospitalini hapo usiku wa kuamkia leo kwa madai kuwa amechoka hivyo mgonjwa huyo aje asubuhi.
Bila kujali ana hali gani, habari zaidi zinaeleza kuwa ndugu wa mgonjwa walimpigia simu mkuu wa wilaya usiku huo huo na DC alikwenda kumuamsha Medical Officer Incharge wakaenda naye hospitalini hapo na kuthibitisha madai ya ndugu wa mgonjwa kisha DC akamfukuza kazi palepale.
Mara baada ya kumfukuza, MO i/c alianza kumtetea Tabibu yule mpaka sasa haijajulikana kama kweli tamko la DC litatekelezwa au DC atashindwa nguvu na MO I/C. Ngoja tusubiri
==================
Bila kujali ana hali gani, habari zaidi zinaeleza kuwa ndugu wa mgonjwa walimpigia simu mkuu wa wilaya usiku huo huo na DC alikwenda kumuamsha Medical Officer Incharge wakaenda naye hospitalini hapo na kuthibitisha madai ya ndugu wa mgonjwa kisha DC akamfukuza kazi palepale.
Mara baada ya kumfukuza, MO i/c alianza kumtetea Tabibu yule mpaka sasa haijajulikana kama kweli tamko la DC litatekelezwa au DC atashindwa nguvu na MO I/C. Ngoja tusubiri
==================
MKUU wa Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Amani Mwenegoha, amemfukuza kazi Dkt. Johanes Makobwe, aliyekuwa zamu wa Hospitali ya Wilaya ya Mjini Ushirombo mkoani Geita usiku wa kuamkia leo kwa uzembe na kukataa kumtibu mtoto mwenye umri wa miezi 6.
Mwenegoha ameiambia FikraPevu amechukua hatua hiyo ili iwe funzo kwa waganga na wauguzi wengine wanaofanya manyanyaso ya kupokea rushwa na kunyanyapaa wagonjwa Hospitalini hapo.
Mkuu huyo amesema alipofika Hospitalini hapo saa kumi na mbili asubuhi alimkuta mganga huyo akiwa amelala ndipo akampigia simu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dkt. Maja Susuma, aliyefika na kumpatia matibabu mtoto huyo mwenye umri wa miezi 6.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari ndani ya hospitali hiyo vinaeleza kuwa Mkuu huyo wa wilaya amechukua hatua hizo baada ya kupigiwa simu na wazazi wa mtoto aliyefikishwa Hospitalini hapo saa kumi za usiku ili kupatiwa matibabu lakini mganga wa zamu alikataa kumtibu.
Sababu zinazotajwa kuwa ndizo zilizosababisha mganga huyo kutomtibu mgonjwa huyo ni madai aliyoyatoa kuwa Mganga ambaye angeingia zamu asubuhi ndiye ambaye angepaswa kumhudumia mtoto huyo.
Chanzo chetu cha habari kimedokeza kuwa, mhudumu huyo wa afya anatuhumiwa kwamba alikuwa amekwenda kuangalia mpira wa mechi ya ligi kuu kati ya Real Madrid C.F na F.C Barcelona iliyochezwa jana usiku Novemba 21, 2015.
Soma zaidi =>Mganga wa zamu afukuzwa kazi kwa uzembe, Ni baada ya kukataa kumtibu Mtoto wa miezi 6