Daycare

Neytemu

Member
Nov 7, 2010
83
1
Nafikiria kuanzisha day care hapa Dar lengo hasa likiwa ni kwa ajili ya watoto ambao hawajaanza shule.
nimepata tu wazo ila kwa kweli sijui ni wapi ntatakiwa kuanzia namaanisha kwa vitu kama kujua mambo gani ya muhimu ya kuzingatia,leseni,location,changamoto na mtaji wa kuanzia unawezagharimu kiasi gani?Je inaweza kunilipa hii?

nakaribisha mchango wenu wanajf
 
NeyTemu,
tuanzishe pamoja,niwe mmbia ktk hiyo daycare,location iwe Town,i mean city centre,walengwa wakiwa young couples,single mothers etc,ili wakati wanaenda kazini wanawadrop watoto wao and mchana wanakuja kunyonyesha if possible ,etc.you can aim for niche market which is willing to pay premium for quality service.
what do you think?
nimeona ulaya some daycare have online webcamera access which is password protected.parents can view the activities of thier kids while they are still at work.imagine sisterdoo wa Voda,Airtel,barclays ,standard charterd etc,yupo officini wakati anafanya kazi anaweza kumcheki mtoto wake online every half hour etc.i have a good location inmind,mtaji itategemea tunaanza na watoto wangapi.
Nafikiria kuanzisha day care hapa Dar lengo hasa likiwa ni kwa ajili ya watoto ambao hawajaanza shule.
nimepata tu wazo ila kwa kweli sijui ni wapi ntatakiwa kuanzia namaanisha kwa vitu kama kujua mambo gani ya muhimu ya kuzingatia,leseni,location,changamoto na mtaji wa kuanzia unawezagharimu kiasi gani?Je inaweza kunilipa hii?

nakaribisha mchango wenu wanajf
 
Dah hilo bonge la wazo, dah ukiazisha hiyo kwanza ni mpya kwa bongo then itakuwa nzuri sana mana now watu wengi wanaacha watoto nyumbani mchana wanatoka kazini wanakwenda kuwanyonyesha.lakini wakiwa town watoto itakuwa simple sana mzazi kuja kumnyonyesha then anarudi kazini jioni anampitia dah bonge la wazo hilo.ila mtaji mzeee mana ili upate wengi iwe town.
Dah kumbe wako watanzania wabunifu tatizo mtaji
 
Kibe mtaji sio tatizo ,tatizo ni kupata interested investors,we will run the day as a business,and shareholding could be sold,to raise capital etc.
je unamtoto mdogo? nadhani itakuwa vizuri kuwa na list ya interested parents .ili kupima soko tarajiwa
Dah hilo bonge la wazo, dah ukiazisha hiyo kwanza ni mpya kwa bongo then itakuwa nzuri sana mana now watu wengi wanaacha watoto nyumbani mchana wanatoka kazini wanakwenda kuwanyonyesha.lakini wakiwa town watoto itakuwa simple sana mzazi kuja kumnyonyesha then anarudi kazini jioni anampitia dah bonge la wazo hilo.ila mtaji mzeee mana ili upate wengi iwe town.
Dah kumbe wako watanzania wabunifu tatizo mtaji
 
yap.ingekua vyema zaidi kufanya research kwanza ili kupata uhakika wa soko japo natumaini soko lipo ila tu ni kwa kiasi gani?
 
Fuatilia kwanza sheria ya nchi inasemaje? je inakulinda wewe na inamlinda clients? unajua system zetu huku si kama za ulaya, and babies real need care. what happens na umejitayarishaje siku kama watoto wanakunywa uji ambao unga wake ume-expire who will defend you. Vipi kuhusu kodi, maana daycare ni gharama, je marketability ikoje? which is cheaper for majority kumlipa housegirl elfu sitini kwa mwezi au kumleta daycare for laki tano let say kwa mwezi, maana you will need a place in town which is bigger.
wengi wa hawa clients wao still wanakuwa na housegirls, je what will make s/he to love bringing baby at your centre and not leave with maid at their homes?? Remember our culture is still barrier in welcoming many western life style.

This just a challenge, note that quiters always dont like challenge, just relax think how you can make this superb in Dar es salaam

we are living to conquer
 
Thanks new Mzalendo kwa mchango wako.

Yaan unanipa sababu na nguvu ya kulifanyia swala hili kazi zaidi.Karibu,tuko pamoja.
 
wapendwa haka ka-idea kazuri sana ila msipuuzie angalizo alilotoa mdau Waberoya hapo juu.

any further info naomba mni-PM.
 
Mbona iko wazi chukua sheria ya watoto ,sheria ya vituo hivyo soma au tembelea wizara ya afya na ustawi wa jamii kila la kheri!
 
Wazo zuri sana hili.
Je utatenganisha Nursery na wale watoto wadogo kabisa mwaka 0 hadi 3, umri wa shule ni miaka 6/7.
Jaribu kuulizia sehemu kama masaki na oysterbay etc, kutakuwa na sehemu za day-care. Sio wazazi wote wanaweza kulipia daycare yenye huduma bora. Kwenye nchi za watu walioendelea serikali inalipia kiasi fulani mishahara ya baby-sitters ili mzazi alipie gharama za pamper na chakula, ukizingatia mzazi ataweza kuwa na tija zaidi kazini, kama mtoto wake yuko kwenye daycare makini. Hawa babysitter nao wanatakiwa wawe na mafunzo maalum!
Kila la kheri na hii project.
Mimi ninao watoto ambao hawajaanza shule, na ningependa waje kwenye daycare yako badala ya kukaa na hausigeli.
 
nategemea kuanza na watoto wa 0 hadi 3 kwanza kwa kua nafikiri ugumu zaidi uko katika watoto wa umri huu.

Thanks Katoto.ntakupm kwa kitakachokua kinaenelea.
 
Keep it up; mkizingatia sheria na trend ya wakazi wa dar, soko lipo watu wako willing....................tabia ya watu wa mijini na hasa mji wetu Dar wanapenda vitu vipya vinavyokwenda na uSASA walionao.........kama walivyosisitiza wadau muwe tayri kuwapa value for their money!
 
ni wazo zuri sana wala usivunjike moyo kabisa.Mimi nafikiri ungetafuta maeneo ya nje ya downtown yaani sehemu ambayo unaweza kupata eneo kubwa la watoto kucheza na vitu kama hivyo ili gharama ya lease isiwe kubwa sana.Kitu kingine ambacho nafikiri ni cha muhimu ni kuona jinsi gani utaongeza value yaani mtu aone mtoto wake anafaidika zaidi kuja daycare kuliko kukaa nyumbani na housegirl.Suala la fedha nafikiri siyo shida naamini kuna watu wengi wana fedha zao wangependa alternative.Mimi binafsi nina mtoto mdogo siwezi hata siku moja kumuacha na housegirl aliyemaliza darasa la saba.
Kwa hiyo nafikiri ni idea nzuri kabisa si unakumbuka shule za English medium zilivyoanza watu waliacha kupeleka watoto public school kwenda kulipa mamilion
 
Asanteni sana wa jf kwa kunitia moyo.I promose to work very hard on it ili siku moja hapahapa Jamvini nitoe tu taarifa ya kuwa ni wapi huduma hii itakuwa inapatikana.
 
Ushauri wangu, ni kuwa sehemu(nyumba ziko nyingi haswa Upanga area i.e on the way to City Centre) Sababu kubwa inayoweza kunifanya nimpeleke mtoto wangu kwenye day care ya ulivyoieleza ni 1)Usalama wa mtoto-kiafya na kutorudi nakutwa ameumia na sijui ni nini kilichomtokea
2)elimu -huwezi kuamini kitoto cha miaka 3 siku hizi kinaimba mistari ya bongo fleva, kiduku,michiriko na maneno yote yakiswahili,maana dada ndio headmistress wake,na hata uvifungie vitu vyao wanakwenda kwa jirani wanacheza wanakusubiria ukitaka kurudi nao wanarudi.
Watu pamoja na uwezo wetu mdogo tuna uwezo wa kulipa mpaka 750,000Tshs/ Yr kama mtoto anakaa angalu 7 hrs from 8 am.
Research ni rahisi wako watu wengi waliofanikiwa kuna kashule kanaitwa Patricia -kako Upanga karibu na Dr. Lwakatare yeye ana min. number of kids lakini you get what you pay for,nina imani hawezi kuwa mswahili kukunyima all that info unayotaka including ups and downs za hiyo kazi. Nina imani unajua lazima uwe na trained people wa kuvifundisha ku pupu,kusema baba, etc sio kazi rahisi sana-ALL THE BEST.
A%20S%20crown-1.gif
 
Back
Top Bottom