Dawasco Yamwomba Radhi Dr. Mwakyembe

Hiyo habari ilitoka idara ya serikali wala haikuandikwa kama udaku.

Mkuu Heshima tena, mimi nilifikiri kuwa tupo hapa JF kwa sababu hatuamini habari zinazotolewa na serikali na media outlets zake, nilidhani kuwa siku zote kazi yetu muhimu hapa ni kuweka record straight za driveby media ya bongo, anyways nimekusikia mkuu tuendelee kukata ishus taifa liko njia panda!!
 
vikashfa vya kipuuzi kama hivi kwa ulimwengu wa manyang`au huwezi kuvikwepa,sasa inapodhihirika kuwa ulikuwa ni ushuzi mtupu aliyepika hilo jungu inabidi atafute pa kujificha.

dr wetu simama imara,Mungu wetu yuko nawe.pole kwa hilo.
 
Its better wameweka records clear kwani sasa hivi kila idara ya serikali inatumika kuwatetea CCM, na ndo maana Kubenea anaandamwa kama nini.
 
(A) Bosi wa DAWASCO ni tunda la EL akiwa Wizara ya Maji.

Wote wanatokea Arusha.

Wafanyakazi wa DAWASCO walipogoma mapema mwaka huu, moja ya hoja yao ilikuwa ni kuondolewa kwa huyo CEO.

(B) Mwakyembe na ripoti iliyomuondoa PM madarakani.

U can see the connection!
 
Suala la kashfa ya Dr.Mwakyembe na DAWASCO ilikuwa katika kutafuta mahala pa kumchafua Dr. Ikumbukwe kuwa Alex Kaaya (DAWASCO CEO) siyo tu kwamba ni chaguo la EL kuwa CEO pale DAWASCO lakini pia ni ndugu kabisa na kwa taarifa toka kwa Kaaya mwenyewe wamewahi kulelewa nyumba moja wakati wa utoto/ujana wao.

Kwa kuconnect hizo dots utaelewa ni kwanini Mh.Dr.Mwakyembe alitengenezewa kashfa ile kutokea upande huo kupitia DAWASCO.

Nafikiri wizara inatakiwa kumlazimisha CEO-DAWASCO kujiuzulu kazi kwa kutoa kashfa nzito kwa mtu "safi" kama Dr.Mwakyembe au hata ingekuwa kwa mteja yoyote ambayo haijafanyiwa utafiti wa kutosha.
 
Back
Top Bottom