Mikocheni A Uswahilini hapa. Watu wamejiunga kwenye system kinyemela bila kuwa na matanki ya septiki majumbani kwao na kukiziba hawawajibiki kwa kuwa hawaathiriki na maji yanayotiririka... Watu wa DAWASCO huja mara kwa mara lakini sioni suluhu ya kudumu. Baada ya siku kadhaa mbubujiko huanza upya....ndugu mwananchi. huduma ya Majitaka kwa jiji la Dar es salaam linalohudumiwa na Dawasco ni asilimia 13. maeneo mengi yaliyobaki wanachi wanatumia matanki yao ya kuhifadhi majitaka maarufu kama "Septic tank". tunakusanya malipo ya huduma ya majitaka kwa maeneo yenye mtandao wetu. hivyo basi tusaidie kujua eneo gani lenye kutiririsha Majitaka ili tukasafishe
Kunduchi mtongani pia kuna bomba lenu limepasuka. Maeneo ya karibu na kota za polisi ila ukitokea mtongani kwenyewe ile barabara ya mikokoni ambako gari haIpiti kuelekea kota za polisi kuna bomba lenu linavuja sana.
Habari, bomba lenu mmelikata na kulifunga toka juzi na kuliacha hivyo hivyo, kwa hiyo maji hamna, tafadharini, leo ijumaa mje tusaidia kuliweka sawa maana tumeanza kuwa ma shida ya maji eneo hili.Nashukuru taarifa imefika, leo watu wenu wamekuja ila wamefunga maji, na kukata kipande kilichokuwa kimepasuka, hatuna maji mitaa hii, tunaomba warudi fasta kuweka kipande kipya tuendelee kupata huduma, msichukue muda mrefu.
Naomba kujua tunapata lini maji maeneo ya Goba hii njia inayoelekea madale, ni gharama sana kununua maji kwenye magari. Hebu tuoneeni huruma.
bunju b eneo ganiTunaomba mtupatie huduma ya maji wakazi wa Bunju b njia ya kwenda mabwepande
Eneo hili ni jipya kuna viwanja vya serikali viliuzwa tukanunua tukajenga ila maji ni sheeda tusaidieni
asante kwa taarifa itafanyiwa kaziHata external pale, baada ya mataa njia ya kwenda mabibo/maziwa opposite na Marriot hotel mabomba yanamwaga maji njia nzima ni tope
ndugu mwananchi..utaratibu wa kulipa Maji ni siku 7 tangu kuletewa bili yako. zaidi ya hapo usikubali utaratibu wowote zaidi ya huo. jua sheria na taratibu zinazokulinda kama mteja ikiwa ni pamoja na kutoa muda wa siku 7 kuweza kulipia bili tangu ulivyopokea bili yako.Inashangaza sana mimi account yangu haina deni la mwezi april, dawasco wameniletea bill (50,000) ya mwezi may, siku NNE zimepita wanakuja kukata maji. Mwezi haujaisha mnakuja kukata maji, ni kwa nini kama sio dalili za kutengeneza mazingira ya rushwa kwa anayekuja kurudisha maji. Hii si haki hata kidogo. Najipanga kuwapandia huko huko ofisini kwenu, mkishindwa kutoa maelezo nawapandia kwa waziri. Ninyi ni waonevu sana. Cc: mtumbua majipu
bitoz dawasco haiwezi kukupa bili kwa maji usiyotumia. kaangalie kwenye mita yako uangalie jinsi mita yako ilivyozunguka na uzidishe kwa bei ya Tsh 1663 kwa unitDawasco acheni wizi
Mwezi huu mvua zimenyesha mfululizo sijatumia maji yenu sana nashangaa mnaleta bili na kudai 35,000/= eti mnadai nimetumia unit 25 acheni upuuzi
Huu ni utapeli uliopitiliza
Latest:Habari, bomba lenu mmelikata na kulifunga toka juzi na kuliacha hivyo hivyo, kwa hiyo maji hamna, tafadharini, leo ijumaa mje tusaidia kuliweka sawa maana tumeanza kuwa ma shida ya maji eneo hili.
DAWASCO.
Habari, bomba lenu mmelikata na kulifunga toka juzi na kuliacha hivyo hivyo, kwa hiyo maji hamna, tafadharini, leo ijumaa mje tusaidia kuliweka sawa maana tumeanza kuwa ma shida ya maji eneo hili.
DAWASCO.
Wapo bize kuwaunganishia maji kinyemera watu. Apa ubungo Msewe kuna Mama mmoja anaitwa Mama Kapinga anaiba maji. Wale wasoma mita wakija anawapa Tshs 3,500 na wanakausha. Shirika la dawasco linaujumiwa sana mpaka inasikitisha. Na huyu mama alishawai kukatiwa maji, na akamfanyizia mambo ya ushirikina, yule mama aliyemkatia maji akaamishwa sehemu ya kazi. Huyu Mama ana tank la Lita laki moja na anauza maji.HukuTabata Kisiwani aka Tabata Mwananchi ndio usiseme. Mqji yanamwagika kila baada ya nyumba tatu ya nne inamaji yanavuja. Sijui hao wasoma mita wao hawaoni.
Naomba unipe tofauti kati ya wholesome water ,potable water na palatable waterNdugu wana JamiiForums,
Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu yaliyo Jijini Dar es salaam , miji ya Kibaha na Bagamoyo Mkoani pwani. DAWASCO inapokea maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.
Ndugu wana jukwaa, DAWASCO inajipambanua kwa kusimamia maadili ,kutoa huduma iliyotukuka pamoja na kuhakikisha huduma ya Maji inapatikana kwa kila mwananchi.
Kama kutatokea kuharibika kwa bomba, wizi wa Maji, umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:
1. Kupitia tovuti: DAWASCO - Welcome to new site
2. Kupitia mitandao yetu ya kijamii ikiwa ni pamoja na Twitter|DawascoOfficial..Facebook|DawascoOfficial ...Instagram|DawascoOfficial
3. Kwa mwananchiposta ; Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:
Afisa Mtendaji Mkuu
DAWASCO
P. O. Box 5340
Sokoine Drive
Dar es Salaam, Tanzania.
4. Au kwa kupiga simu huduma kwa wateja dawasco
0800110064 /022 2164800 ( Kupiga namba hizi ni Bure)