Dawasa: Mtambo wa Maji Makongo juu wawashwa na maji yaongezeka, Mabwawa 26 yaliyochepusha maji ya Ruvu yakamatwa!

... cheap politics; hayo mabwawa 26 ya kufugia samaki yana-consume kiasi gani cha maji? Put facts on the table badala ya siasa!
Si ndio hapo mkuu, yaani Watanzania tumekubuhu in manufacturing lame excuses - hatikosi sababu - siasa tu 24X7, MTU ungetegemea kwamba Wizara yenyewe ingekuwa na kitengo maalumu cha kukaguwa main water pipes for illogical connections, vile vile na kubaini wanao chepusha vyanzo vya maji, hizi tabia za kufanya mambo wakati wa crisis kama za zima moto mpaka lini?

Mara oooh, tumemkamata Mchina anayelima mboga mboga tumekuta alikuwa anapampu maji mengi kwenye mradi wake usiku wa manane, akatozwa faini ya million sijui tatu na nusu bila ya kumfikisha kwenye vyombo vya Dola, vifaa vyake vikataifishwa, lakini cha ajabu kesho yake wakakuta Mchina kanunua mitambo mingine na kuendelea na mradi wake kama kawa - hana wasi hata kidogo, cha kujiuliza hapa ni,je, Mchina huyo jeuri hiyo anaipata wapi,je, huko kwao Uchina anaweza kufanya hujuma kama hizo akaendelea kupeta tu!! Haya tuje kwenye mabwa makubwa ya kufugia samaki, kwani si yanaonekana tu hata ukiwa ofisi kwako kwa kutumia Google Earth kupitia kwenye Computer au smart phone - tatizo LA wengi wetu hatuna ubunifu hata kidogo na hatujui jinsi kujituma na kuwajibika.
 
15 September 2021

ONYO KALI: UKINASWA UNACHOTA MAJI PEMBEZONI MWA MTO RUVU, UTAPEWA ADHABU HII
...

Bodi ya maji ya bonde la Wami Ruvu imewatahadharisha wakazi wa Dar es salaam na Pwani kutumia maji kwa uangalifu kufuatia kupungua kwa maji katika mto Ruvu ambapo kwa sasa maji yanayoingia katika mto huo ni lita elfu saba kwa sekunde moja mwaka huu 2021, ambapo kwa mwezi kama huu mwaka jana 2020 yalikuwa yakiingia lita 12380 kwa sekunde moja.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Afisa wa bodi ya maji bonde la wami Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmasi, alipotembelea mto Ruvu eneo la Ruvu Juu mkoani Pwani iliyopo mitambo ya kuzalisha maji ya mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Dsm (Dawasa) ambapo amesema kufuatia hali hiyo bodi imeamua kusitisha vibali vyote vya matumizi ya maji ya mto huo ikiwemo shughuli za umwagiliaji na ufyatuaji wa matofali ili kunusuru maji yaliyopo kuweza kuwafikia watumiaji wa majumbani.

Mhandisi Mmasi amesema hali hii imewahi kujitokeza katika miaka ya nyuma ambayo husababishwa na mabadiliko ya tabianchi hivyo ipo baadhi ya miaka hutokea ukosefu wa mvua na kusababisha kupungua kwa maji katika mito lakini shughuli za kibinadamu pia zikitajwa kuchangia kupungua kwa kina cha mto Ruvu.


Source : Global TV online
 
Wakati Dar imezungukwa na bahari. Na hayo mabwawa yakishakosa maji samaki wafe?
Hivi mtu akiweza kupampu maji toka baharini ili akuze Samaki wake kwa bwawa nalo kosa!?
Bora tuyachukue baharini basi!
 
Ina maana katika mpango kazi wa wizara/mamlaka za maji hakuna suala la ufuatiliaji wenye lengo la kutunza vyanzo vya maji !!?? ..... Maana hivi ndivyo vyanzo tegemewa kwa ajili ya kuzalisha umeme. Haiwezekani vyanzo vya maji viingiliwe halafu lisiweze kungundulika mpaka shida imejitokeza na wanachi kupaza sauti; UNLESS kuwe na sababu nyingine zaidi ya yanayoelezwa.
 
Kongole nyingi zikufikie Mh. Awesu, katika kipindi cha adha kubwa itokanayo na uhaba wa maji, kauli thabiti na zenye kutia moyo kama huwa ni muhimu mno kwa wananchi.
Huu nao ni uongo baada ya lawama kuzidi wanajifanya wamewasha, siku zote kabla walikuwa wapi!
 
Ina maana katika mpango kazi wa wizara/mamlaka za maji hakuna suala la ufuatiliaji wenye lengo la kutunza vyanzo vya maji !!?? ..... Maana hivi ndivyo vyanzo tegemewa kwa ajili ya kuzalisha umeme. Haiwezekani vyanzo vya maji viingiliwe halafu lisiweze kungundulika mpaka shida imejitokeza na wanachi kupaza sauti; UNLESS kuwe na sababu nyingine zaidi ya yanayoelezwa.
Mkuu wakati mwingine ni vigumu kuelewa Waafrika tulivyo kuwa wired by our MAKER, priorities zetu wakati mwingine ni totally incoherent - hapa tunazungumzia vyanzo vya MTO was Ruvu, je, kuna task force hipi inafatilia vyanzo vya MTO wa Rufiji tukiwekea maanani kwamba ujazaji was Bwana LA Nyerere utaanza mwezi March mwaka ujao,je, tuna uhakika katika hilo? Maana kwa mbali nimeanza kuona watu wameanza kupigia debe uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia, kisa? eti imegundurika Tanzania ina vyanzo vingi vya gesi asilia - wenye akili wakajua zimeanza lobbying za chini chini za kujenga hoja za kurudisha Dowans, Symbion na Agrecco - tusipo kuwa makini tutayumbishwa kweli kweli katika suala hili la Nishati ya UMEME,tukumbuke ushauri mzuri wa Dk.Magufuli aliyesema tukifanya ujinga was kuruhusu kampuni binafsi kuzalisha umeme tutakoma - watapandisha bei za umeme kiholela wanaweza hata kutu-blackmail na kutuacha njia panda.
 
MATAGA wakitoa taarifa kwa uma kuwa watu wanaofanya kilimo cha kisasa cha umwagiliaji wanahujumu matumizi ya maji👇🤡🤡🤡
1637308571637308570.jpg
 
Waziri wa maji Juma Awesu amesema mgao wa maji utapungua sana kama siyo kumalizika kabisa baada ya mitambo ya maji ya Makongo juu kuwashwa na maji kuingia kwa wateja.

Pia, mabwawa ya kufugia samaki zaidi ya 26 yaliyochepusha maji ya mto Ruvu yamekamatwa na hivyo maji yamerudishwa kwenye mkondo wake ili yaelekezwe kwa wananchi.

Source: ITV habari!
Huu ni upuuzi.. Awadanganye wajinga wenzake mazuzu. Hii nchi imesha tuona Watanzania mazuzu kabisa. Hayo mabwawa yana ingiza maji kiasi gani? Kwamba yana kausha mto? Ndiyo yale yankuambiwa mtu ana ekari 50 halafu ana nyonya maji lita milioni moja kwa saa si atapeleka mafuriko huko shambani???
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Back
Top Bottom