ngulukizi
JF-Expert Member
- Oct 10, 2018
- 510
- 1,429
Ni miaka 3 sasa tangu rafiki ambaye kwa namna moja au nyingine tulishibana sana aliponitoka kimasihara tu.
Nakumbuka ilikuwa Kariakoo siku hiyo tulipokutana na wale jamaa wanaouza dawa za kuondoa sumu mwilini ndipo nasi tukaona kuna umuhimu wa kuzinunua na kuzitumia ili tuondoe mafuta mwilini.
Kweli tukanunua mimi na mwenzangu tukatumia baada ya muda tulikuwa tunaenda chooni kila mara kiasi kwamba tukaona ni mchezo tu kidogo chooni tunatoa haja kubwa kisha tunarudi kupiga story huku tukiambiana leo sumu na takataka zote zinaondoka mwilini.
Kumbe ile dawa ilienda kufanya figo za rafiki yangu zifeli ghafla akaanza kutapika na kuharisha mfululizo ikabidi tumuhamishe Muhimbili pale hapo muda huo mimi niilikuwa na afueni sijui kwangu nini kilitokea maana ile kuharisha ilikata ghafla baada ya kuona hali ya mwenzangu tulipofika Muhimbili wakasema twende Mloganzila tukaenda na hapo hapo baada ya kuangalia vipimo madaktari wakasema figo zimefeli hivyo acha wahangaike ili apate nafuu.
Nakumbuka usiku wa tarehe 23 kuamkia 24 December jamaa yangu alifariki.
Bado ninakukumbuka ndugu yangu na rafiki yangu RIP.
Nakumbuka ilikuwa Kariakoo siku hiyo tulipokutana na wale jamaa wanaouza dawa za kuondoa sumu mwilini ndipo nasi tukaona kuna umuhimu wa kuzinunua na kuzitumia ili tuondoe mafuta mwilini.
Kweli tukanunua mimi na mwenzangu tukatumia baada ya muda tulikuwa tunaenda chooni kila mara kiasi kwamba tukaona ni mchezo tu kidogo chooni tunatoa haja kubwa kisha tunarudi kupiga story huku tukiambiana leo sumu na takataka zote zinaondoka mwilini.
Kumbe ile dawa ilienda kufanya figo za rafiki yangu zifeli ghafla akaanza kutapika na kuharisha mfululizo ikabidi tumuhamishe Muhimbili pale hapo muda huo mimi niilikuwa na afueni sijui kwangu nini kilitokea maana ile kuharisha ilikata ghafla baada ya kuona hali ya mwenzangu tulipofika Muhimbili wakasema twende Mloganzila tukaenda na hapo hapo baada ya kuangalia vipimo madaktari wakasema figo zimefeli hivyo acha wahangaike ili apate nafuu.
Nakumbuka usiku wa tarehe 23 kuamkia 24 December jamaa yangu alifariki.
Bado ninakukumbuka ndugu yangu na rafiki yangu RIP.