Watu wanaweza kusema mengi, lakini nadhani matatizo yote haya yameletwa na serikali hasa kuchukua misingi mibovu iliyopo ndani ya ccm. Nasema hivi kwa sababu, seheria za nchi haziangalii cheo chochote cha mtu au nafasi yake kumpa nafasi ya kutenda uhalifu. "Hakuna nafasi kabisa kuwa atavua gamba". Sio kweli kuwa mwizi atapalekwa tu kwenye sheria andapo ni mtu mdogo ("minor"). Hii imedhihirika sana sehemu nyingi, na bahati mbaya hata wahanga wa wananchi kujichukulia sheria mkononi ni hawa hawa wasiokuwa na nafasi (say) ndani ya jamii. Kweli leo hii hao wanaoitwa majina yote mabaya kwa kulifikisha taifa hapa, wananchi wasingekuwa wamechukua sheria mikononi juu yao? Sasa hii janja ya ccm na serikali yake kutokusimamia haki ndio inayoifikisha nchi mahali pabaya, na matokeo yake kutafuta visingizio vya kipuuzi kama hivi vya kuotojana na wala kutowafikisha mbele ya vyombo vya seheria. Ieleweke, MHALIFU NI MHALIFU TU, bila kujali wadhifa wake au nafasi yake ndani ya chombo chochote cha kiserikali au kijamii.
Hizi double standards zitaisha lini? ndizo zinazolimaliza taifa hili! Shule kuanzai chakechea, afya, polisi, mahakama n.k ni double double, sasa hata makanisa na misikiti naona navyo vitakuwa double double
TZ bado ni nchi inayoendeshwa na vigogo. Vigogo hawapelekwi mahakamani. Sasa hawa viongozi waliokamatwa ni vogogo wakubwa wa Makanisa hapa TZ, lakini pamoja na rais kuwa na majina yao, kuna mpango nashaka wa kusamehee kutokana na sensitive ya issue ya kidini, kwa sababu Rais ni Muislamu na hawa waliokamatwa ni viongozi wa dini ya Kikiristo.