Dawa ya waongo

Bayo

Senior Member
Jul 2, 2009
195
34
Mwanasayansi mmoja, alifanikiwa kutengeneza robort ambalo lilikua na uwezo wa kugundua kama mtu anadanganya na linampiga kibao. Paaaaaah!! Tajiri mmoja aliekua anamiliki shule aliamua kulinunua ili kuwakomesha watoto watoro na wahongo shuleni kwake.

Kwanza aliamua kulijaribishia nyumbani kwake. Mda wa dinner, yeye, mtoto wao Johnny na mkewe.
BABA: Johnny jana ulikua wapi?
JOHNNY: nilienda shule baba. (KIBAO..Paaaah) nilikua kwa kina Mark.
BABA: Ulikua unafanya nini?
JOHNNY: Tulikua tuna fanya home work… Paaaaaaaah,, aahh Tulikua tunaangalia movie
BABA: Movie gani mbona hapa nyumbani zipo nyingi tu?
JOHNNY: Harry Potter… Paaaaahh, ahah Porn movies
BABA: (Hasira) Pumbavu, sie wakati wa umri kama wenu tulikua tunawaza masomo na.. …. Paaaaaah
JOHNNY: (Kicheko… kwi kwi kwi kwi..)
MAMA: We tabia gani kumcheka Baba yako? Paaaaah Kibao!

Duh?
 
Hiyo ipelekwe mahakamani na kwenye viwanja vya mikutano ya kampen wakati wa uchaguzi!
 
ha ha ha maza naye alisema uongo kuwa yule alikuwa baba yake na Johnny!!! akaambulia kibao.....
 
Mmmmh naogopa kama litapelekwa huko maana itabidi lianze na Kiranja Mkuu mwenyewe, siju FFu watalifanyeje huko??
Hiyo ipelekwe mahakamani na kwenye viwanja vya mikutano ya kampen wakati wa uchaguzi!
 
Pale kwenye jibu la kuangalia porn...angepigwa tena angesema tulikuwa tunafanya......
 
hilo robort lilitakiwa kuwekwa chumbani kwa wana ndoa wanaume wangekuwa wanalabuliwa kila siku kwa kweli me nitalinunua
 
Linafaa lipelekwe ikulu kwa jk, ahadi zake zote ni za uongo.
 
Mwanasayansi mmoja, alifanikiwa kutengeneza robort ambalo lilikua na uwezo wa kugundua kama mtu anadanganya na linampiga kibao. Paaaaaah!! Tajiri mmoja aliekua anamiliki shule aliamua kulinunua ili kuwakomesha watoto watoro na wahongo shuleni kwake. Kwanza aliamua kulijaribishia nyumbani kwake. Mda wa dinner, yeye, mtoto wao Johnny na mkewe.
BABA: Johnny jana ulikua wapi?
JOHNNY: nilienda shule baba. (KIBAO..Paaaah) nilikua kwa kina Mark.
BABA: Ulikua unafanya nini?
JOHNNY: T hiyo inafaa sana wakati wa kawpeni za uchaguzi na wapewe magamba litawanyosha sana.


Mh!!!
 
naomba unitumie li roboti moja manake huyu gf wangu mmmh..naona itasaidia

Ha ha ha ha ha ha... Litamuua bure mana hawa dada zetu walivyo waongo cku hz... Hata likiletwa humu JF itakuwa ni balaa tupu
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom