Msaada: Ipi dawa asilia na ya haraka ya kuondoa mipasuko unyayoni?

Kichankuli

JF-Expert Member
Dec 18, 2008
887
189
JF DR. au mdau mwingine yeyote wa JF tafadhali nieleze iwapo kuna dawa inayoweza kutibu Sagamba (mipasuko ya kwenye visigino)
 
Wadau mbona kimya, hakuna mwenye kujua habari za tiba ya sagamba?
 
unaongelea sagamba kama ugonjwa au sagamba kama hali inayoweza kumpata mtu asiyeangalia miguu yake?
Ili kuzuia sagamba nakushauri uwe na kawaida ya kuiloweka miguu yako kwenye maji ya uvuguvugu na sabuni kisha uisugue na jiwe au brashi ( pumice stone).Kisha kausha na upake mafuta.Pia pendelea kulala na soksi baada ya kupaka mafuta hadi hali iwe ya kuridhisha.Endelea kuwa unaisugua unapooga.Miguu yako itabaki soft bila mipasuko.
 
Pia upunguze 'rate' ya kuvaa viatu vya wazi...tatizo linakuja kama pia una matatizo ya fungus za vidoleni, manake nazo zinachachamaa ukikazana kuzifunika!
 
Ikena nashukuru ngoja nikaisakanye madukani

Mafanikio mema,, ila uhakikishe unaipata dawa yenyewe kwani maduka mengi wakikosa dawa hiyo wanakutafutia substute.

Boksi la dawa hiyo ni kama la zambarau na picha ya mtu mwenye sagamba nyayoni imeonyeshwa hali kadhalika mtu mwenye fungus/ukurutu pia imeonyeshwa.
 
Mi nijuavyo hali ile inatokana na mara nyingi kutoijali sana miguu.

Mimi nikiwa nimekulia vijijini, nilishambuliwa sana na hayo makenya, lakini ilikuwa inatokana na kutovaa viatu almost muda wote, na ile hali ya baridi sana. Mara baada ya kuhamia mijini na kuanza kuvaa viatu fully, hali hiyo ilipotea na haijarudi tena.

Unless kama hiyo hali ni special ambayo kwa mimi sijaizowea. Fuata ushauri wa hiyo cream kama ulivyoshauriwa na dada WoS.
 
unaongelea sagamba kama ugonjwa au sagamba kama hali inayoweza kumpata mtu asiyeangalia miguu yake?
Ili kuzuia sagamba nakushauri uwe na kawaida ya kuiloweka miguu yako kwenye maji ya uvuguvugu na sabuni kisha uisugue na jiwe au brashi ( pumice stone).Kisha kausha na upake mafuta.Pia pendelea kulala na soksi baada ya kupaka mafuta hadi hali iwe ya kuridhisha.Endelea kuwa unaisugua unapooga.Miguu yako itabaki soft bila mipasuko.

Hili tatizo analo mai waifu, na sidhani kuwa linasababishwa na kutoijali miguu/visigino, kwani mwenyewe huwa anaviosha na kuvisugua kwelikwweli. Labda kwa suala la kutovaa viatu vya kufunika visigino hilo naweza kubaliana nalo kwani mara nyingi huvaa viatu vya wazi.

Lakini kitu kingine ambacho kinanitatiza ni kuwa, hata mimi nimekulia kijijini na nakumbuka kutovaa viatu vya kufunika nadhani hadi nilipojiunga na kidato cha kwanza lakini sijawahi kupasuka visigino. Katika familia yetu Mama na dada zangu wawili walikuwa na tatizo la kupasuka visigino. Lakini nakumbuka pia kuna dada mmoja tulikuwa tunasomo shule moja ya msingi, yeye visigino vyake vilikuwa vinatoka unyevunyevu mwingi kiasi kwamba tulikuwa tunamshangaa kweli. Je kuna uwezekano wa upasukaji wa visigino kuwa ni suala la kibayolojia kama ilivyo kuota ndevu, sharafa au gadern love?
 
Mafanikio mema,, ila uhakikishe unaipata dawa yenyewe kwani maduka mengi wakikosa dawa hiyo wanakutafutia substute.

Boksi la dawa hiyo ni kama la zambarau na picha ya mtu mwenye sagamba nyayoni imeonyeshwa hali kadhalika mtu mwenye fungus/ukurutu pia imeonyeshwa.
Nimejaribu kupitapita kwenye maduka ya hapa Dodoma nimekosa, na kuna duka moja walitaka kunichomekea kunipa mbadala kwa mantiki kuwa zote ni anti-fungus. Unaweza kunieleda jina la duka (Dar) ambalo naweza kwenda straight nikapata hiyo dawa tafadhal
 
JF DR. au mdau mwingine yeyote wa JF tafadhali nieleze iwapo kuna dawa inayoweza kutibu Sagamba (mipasuko ya kwenye visigino)

Mafuta ya vaselini ni dawa tosha. Safisha miguu vuzuri paka mafuta ya vaselini. Tumia mafuta ya vaselini kila wakati na tatizo la sagamba halitajirudia tena.
 
Hili tatizo analo mai waifu, na sidhani kuwa linasababishwa na kutoijali miguu/visigino, kwani mwenyewe huwa anaviosha na kuvisugua kwelikwweli. Labda kwa suala la kutovaa viatu vya kufunika visigino hilo naweza kubaliana nalo kwani mara nyingi huvaa viatu vya wazi.

Lakini kitu kingine ambacho kinanitatiza ni kuwa, hata mimi nimekulia kijijini na nakumbuka kutovaa viatu vya kufunika nadhani hadi nilipojiunga na kidato cha kwanza lakini sijawahi kupasuka visigino. Katika familia yetu Mama na dada zangu wawili walikuwa na tatizo la kupasuka visigino. Lakini nakumbuka pia kuna dada mmoja tulikuwa tunasomo shule moja ya msingi, yeye visigino vyake vilikuwa vinatoka unyevunyevu mwingi kiasi kwamba tulikuwa tunamshangaa kweli. Je kuna uwezekano wa upasukaji wa visigino kuwa ni suala la kibayolojia kama ilivyo kuota ndevu, sharafa au gadern love?


Mkuu hilo ni swala la kurithi na wakati mwingine ni la mazingira.
Mi ni wa huko dom, ila kwasasa sipo dom. Nami nilikuanayo hayo masagamba kabla ya kutoka dom.Miezi ya kwanza baada ya kutoka dom ni nilianza kuona mabadiliko katika nyayo zangu na hasa baada ya kutumia fungnil.
Siku hizi situmii kabisa na visigino vimekua kama vya mtoto mchanga.
Nikienda maeneo flan flan na hasa huko dom sagamba zinarudi upya.
So actually ni hali ya hewa au tuseme mazingira yanachangia sana. Nauhakika kuna mazingira ambayo favourable kwa waifu wako.

Endelea kumshauri kuosha miguu, kupaka mafuta na kuvaa viatu vya kufunika kama ulivyoshauriwa na wanajamii.
 
wakuu mambo vp, naomba msaada kwa anayefahamu dawa ya kuzuia kupasuka kwa miguu ktk unyayo, na nipo kwenye barid irnga pia sifany shughuli inayofanya nikanyage maji. msaada plz.
 
uana vaa viatu au unatembea tu bila viatu?
unapo oga unakumbuka kunawa miguu na nyao vizuri na kukausha kabla ya kuvaa viatu?
je unatumia aina gani ya sabuni...ina cloro au sodium nyingi?
naomba unjibu hayo maswali then tuendelee...
 
spaceout.gif
MATUNZO ya miguu ni jambo muhimu kwa mwanamke yeyote. Miguu isiyotunzwa vizuri humfanya mtu asiwe huru kuvaa mavasi na viatu vya ina falani hata kama anavipenda.
Magaga
(Kupasuka kwa nyayo) miguuni ni tatizo linalowakumba watu wengi na kuwafanya wasiwe huru kuvaa baasdhi ya nguo na aina za viatu.
Miguu inahitaji matunzo, hewa ya kutosha ili iwe mikavu ili kuepeukana fangasi na maambukizi mengine kama magaga.

Ili miguu yako iwe na muonekano mzuri, ni vizuri kama utashiriki mazoezi ya kutosha kwa kutembea, kuruka kamba, kuibonyezabonyeza,

kuinyoosha, kufanya mazoezi ya kukimbia, au mazoezi ya viungo yatakayo jumuisha na miguu.
Ili kuzuia miguu yako kupasuka, hakikisha unaisafisha mara kwa mara.

Tumia scrubs kusugua miguu yako kuanzia juu hadi chini,ukishasugua vizuri safisha na maji ya uvuguvugu kisha paka mafuta ya Zaituni ‘Olive Oil’ au mafuta ya Nazi au mafuta yako ya kila siku , lakini yasiwe na kemikali zinazoweza kuzidisha tatizo.

Ukiwa na magaga au nyayo ngumu, hakikisha unaiosha mara kwa mara na kuisugua kwa kutumia kifaa maalum. Ikiwezekana nenda duka la vipodozi uulizie kifaa cha kukwangulia nyayo na kununua krimu au losheni maalum za kulainisha miguu yako .

Njia rahisi ya kuosha miguu ukiwa nyumbani, loweka miguu kwenye maji ya uvuguvugu yenye chumvi, baada ya hapo sugua kwa kifaa maalum cha kusugulia miguu kuondoa seli zilizokufa, kisha paka losheni.

Kuna dawa zinapatikana sadalia zinaitwa 'cracket heels'. Hizi zinasaidia kiasi. Pia iwapo utaloweka miguu katika maji ya moto kiasi kisha kuikausha kwa taulo na kupakaa mafuta ya vaseline. Mafuta haya hutelezesha miguu kwahiyo ni bora kupakaa usiku wakati wa kulala kisha kuvaa soksi ili usichafue matandiko.Jaribu hivyo kisha unipe Feedback Mkuu.@ruston8919

 
Habari zenu madaktari wooote?,
Naombeni utatui wa tatizo hili, maana naita tatizo sababu awali sikuwa hivi lakini tangu nihamie Singida kikazi mpaka najionea huruma.
Nimesha haribu net yangu na mashuka, naona mpaka aibu kuvaa sandalz mtaani, da!
Masaada jamani, kipi cha kufanya...
 
Habari zenu madaktari wooote?,
Naombeni utatui wa tatizo hili, maana naita tatizo sababu awali sikuwa hivi lakini tangu nihamie Singida kikazi mpaka najionea huruma.
Nimesha haribu net yangu na mashuka, naona mpaka aibu kuvaa sandalz mtaani, da!
Masaada jamani, kipi cha kufanya...

mFICHA MARADHI KIFO HUMUUMBUA!!!as mbona hujasema kama una magaga kama una fungus kama ni funza sasa tutakusaidiaje ?
 
Back
Top Bottom