Zijue faida za Mmea wa Mlonge, Jitibu magonjwa 300 kwa kutumia mlonge

G.MWAKASEGE

Senior Member
Jun 29, 2007
153
15
Tulikuwa na family day na haya ndio niliyoambulia nikaona they are good news worth sharing.

View attachment The Moringa Oleifera Tree.doc

======================

Moringa (Moringa spp.) maarufu kama Mlonge ni miongoni mwa miti muhimu kuliko yote duniani. Mti huu ukuao
haraka hupandwa katika maeneo mengi na hutumika kama chakula cha binadamu, lishe ya mifugo, tiba mbadala na
kusafisha maji.



7577309_orig.png


1. Karibu kila sehemu ya mti wa Moringa inatumika au inalika kama chakula. Majani ndio sehemu kuu ya mti wa Moringa, unaweza kuyala yakiwa mabichi au yakiwa yamepikwa kama mboga yoyote ya majani, na pia unaweza ukayakausha na kuyahifadhi kama unga-unga kwa miezi mingi huku ukitumia kama kiungo kwenye mboga na mchuzi.

Pia majani yanaweza kutumika kama lishe bora ya mifugo.

Utafiti wa kisayansi umeonyesha kuwa majani ya Moringa ni chanzo kikubwa cha virutubishi vingi sana. Virutubishi hivi ni pamoja na;

Vitamini C - Kirutubishi hiki ni muhimu katika kutengeneza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali. Kiwango chake katikamajani ya Moringa ni zaidi ya mara saba ya ile inayopatikana kutoka kwenye machungwa.

Calcium (madini chuma) - Kirutubishi hiki ni muhimu katika kuimarisha pamoja na kujenga mifupa na meno mwilini. Kiwango chake katika majani ya Moringa nimara nne zaidi ya yale yanayopatikana kutoka kwenye maziwa.

Protini - Kirutubishi hiki ni muhimu katika kujenga mwili na kuimarisha ngozi. Kiwango chake katika majani ya Moringa ni mara mbili zaidi ya ile inayopatikana kutoka kwenye maziwa.

Vitamini A - Kirutubishi hiki ni muhimu katika kuimarisha macho na kuongeza uwezo wa kuona. Kiwango chake katika majani ya Moringa ni mara nne zaidi ya ile inayopatikana kutoka kwenye Karoti.

Potassium - Kirutubishi hiki ni muhimu katika kujenga na kuupatia mwili nguvu. Kiwango chake katika majani ya Moringa ni mara tatu zaidi ya ile ipatikanayo kutoka kwenye ndizi. Maua ya Moringa yamejaliwa madini chuma (calcium) na Potassium kwa wingi na yanaweza kuchemshwa au kupikwa na kuliwa kama mboga.

2. Mboga
Majani ya Moringa huliwa kama mboga nyingine za majani kwa mfano mchicha. Majani yanaweza kuvunwa wakati wa kiangazi ambapo mboga nyingine hazipatikani. Pia matunda mateke ya Moringa huweza kutumika kama mboga, hutayariswa kama maharage mabichi (machanga). Matunda yalikomaa hutoa mbegu ambazo zinaweza kutumika kama njegere au kukaangwa kama karanga.


3. Mafuta
Mafuta kutoka kwenye mbegu za mti wa Moringa huweza kutumika katika kupikia na kuwasha katika nyumba. Pia hutumika sana kwenye viwanda katika utengenazaji wa sabuni na bidhaa za urembo. Mafuta hukamuliwa kutoka kwenye mbegu kama ambavyo alizeti hukamuliwa.


4. Lishe ya Mifugo
Majani ya Moringa huliwa na ng'ombe, mbuzi, kondoo, sungura na kuku. Mbegu huliwa na kuku pamoja na wanyama wengine kwenye jamii ya ndege.


5. Pambo la nyumba
Mti wa Moringa hupandwa kwa wingi kwenye bustani kama ua au mti wa kivuli na hutumika katika upambaji. Pia miti ya moringa ikipandwa karibu karibu inaweza kutumika kama fensi.


6. Chanzo cha kipato
Mti wa Moringa ukitumiwa vizuri ni chanzo kizuri cha kipato. Mfano ni uuzaji wa miche ya mti wa moringa na utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na moringa.


7. Tiba mbadala
Moringa ni mti muhimu sana katika utabibu kama tiba mbadala, majani, maua, mbegu na mizizi yake hutumika sana katika kutibu magonjwa mbalimbali.



Majani


  • Majani mabichi ya Moringa ni mazuri kwa kina mama wajawazito na wenye kunyonyesha, huongeza wingi wa maziwa na hushauriwa kwa kutibu Anaemia.
  • Juisi ya majani ya Moringa hutumika kusafisha tumbo na hutibu magonjwa ya zinaa. Juisi ikichanganywa na asali inatibu kuharisha.
  • Pia juisi ina uwezo wa kusawazisha presha (BP) na kudhibiti viwango vya sukari kwa wagonjwa wenye
  • kisukari.
  • Majani pia huweza kupakwa mwilini katika kutibu majipu na maambukizi ya ngozi.

Mbegu

  • Mbegu za mti wa Moringa ni kinga dhidi ya vijidudu (bacteria) wasababishao magonjwa na kuathiri ngozi.
  • Pia mbegu hutuminka katika kusafisha au kuchuja maji ambapo zikipondwa na kuwekwa kwenye maji yenye tope au machafu husababisha uchafu kujikusanya na kuzama chini kisha kuacha maji yakiwa safi na salama kwa kupikia au kunywa baada ya kuchemsha.

Magome

  • Magome ya mti wa Moringa hupondwa na kuwa rojorojo kisha hutumika kutibu majipu pia hupakwa ili kupunguza maumivu yatokanayo na kung'atwa na wadudu kama nyoka na nge.

Matumizi mengineyo
Miti ya Moringa ikipandwa shambani huweza kuwa msaada kwa mimea ipandayo kama vile maharage. Pia Moringa ikipandwa bustanini husaidia kupunguza joto la moja kwa moja kufikia mimea kama vile mboga mboga na kupunguza uwezekano wa mboga kusinyaa au kukauka. Mti wa Moringa unaota katika mazingira yote, kwenye ukame na meneo yenye maji. Angalizo huchukuliwa kuhakikisha kuwa maji hayatuami kwenye mti kwasababu maji huweza kusababisha ugonjwa na kufanya mizizi ioze. Karibu aina zote za udongo zinafaa kwa mti wa Moringa. Mbegu, kipande cha tawi na hata mzizi vinaweza kutumika kuotesha mti wa moringa.


My_moringa2_tree_9_2008.jpg


Namna ya kupanda mti wa Moringa

I. Mbegu
Mbegu iliyokomaa ya mti wa Moringa hulowekwa siku moja kabla ya kuoteshwa, kama maji sio tatizo mbegu inaweza kupandwa moja kwa moja kwenye udongo baada ya kuchimba shimo, weka maji na kisha changanya udongo na samadi angalau kilo tano kabla ya kupanda mbegu halafu endelea kumwagilia katika miezi ya mwanzo. Baada ya angalau siku kumi na tano mbegu inatakiwa iwe imeshachipua. Pia unaweza kuotesha mbegu za Moringa katika vifuko kwenye kitalu kisha kuhamishia shambani baada ya kuota.


II. Kipande cha tawi
Vipande vya tawi lililo komaa huweza kutumika katika kupanda mti wa Moringa, hivi hupandwa eidha moja kwa moja shambani au kwenye vifuko katika kitalu. Kama ukipandwa moja kwa moja angalau robo moja ya tawi inatakiwa ipandwe kwenye udongo, usimwagilie maji mengi sana kwani inaweza kusababisha kuoza.


UNAHITAJI MLONGE? PIGA 0769142586

Mlonge au moringa oleifera kwa kiingereza umekuwa ukijulikana kama mti wa miujiza kwa karne nyingi katika baadhi ya nchi za Afrika, Asia na katika nchi za Caribbean. Mti huu umeripotiwa kutibu zaidi ya magonjwa 300 ikiwemo magonjwa mbalimbali sugu.

Karibu kila sehemu ya mti huu hutumika kama dawa. Majani ya mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au yaliyokaushwa na kusagwa kuwa unga. Unga wa mlonge unaweza kuhifadhiwa kwa miezi kadhaa bila kupoteza ubora na faida zake za kiafya.

Mbegu za mlonge zimekuwa dili kubwa duniani kwa sasa, zinahitajika kwa kiasi kikubwa katika nchi ya Marekani na China na kwa mujibu wa taarifa ni kuwa zinauzwa mpaka 45000 ya Tanzania kwa gramu 500. Walikuja pia wachina kuzinunua kwa wingi na walikuwepo hapa bei ya mbegu za mlonge ilifika mpaka 11000 kwa kg kwa bei ya jumla yaani kwa anayechukua kg 100 au 500 au 1000 na kwenda juu. Taarifa zisizo rasmi zinadai wachinja hawa walikimbia nchini baada ya serikali kuanza kufuatilia na kuwakamata wakwepaji kodi bandarini. Isingekuwa hivi mpaka leo mlonge ungekuwa umeshatowka wote Tanzania.


Faida za mlonge zimeandikwa na majarida ya afya na lishe kadhaa duniani. Kile ulikuwa hujui ni kuwa viwanda na makampuni mengi ya dawa za hospitalini yamekuwa yakitumia virutubishi vilivyomo kwenye mti huu kutengenezea madawa kwa ajioli ya binadamu na wanyama.

Mlonge una:

Kalsiumu mara 17 zaidi ya ile ya maziwa ya ng’ombe

Potasiamu mara 15 zaidi ya ile ya kwenye ndizi

Una vitamini A mara 10 zaidi ya ile ya kwenye karoti

Una protini nyingi mara 9 zaidi ya ile ya kwenye mtindi

Una klorpfiti (kemikali ya rangi ya kijani ipatikanayo katika mimea) mara 4 zaidi ya ile ya kwenye nyasi au majani ya ngano (wheatgrass)

Una madini chuma mara 25 zaidi ya yale ya kwenye Spinach

Una vitamini A mpaka Z

Una omega 3, 6 na 9

Una asidi amino zile muhimu zinazohitajika na mwili

Una kiasi cha kutosha cha madini ya zinc ambayo ni madini muhimu katika kuongeza homoni za kiume na nguvu za kiume kwa ujumla

Mlonge ndicho chakula chenye afya zaidi juu ya ardhi:

Mlonge una jumla ya virutubishi 92, mmea au mti mwingine wenye virutubishi vingi basda ya mlonge una virutubishi 28. Mlonge una vionsa suku 46 na viondoa uvimbe mbalimbali mwilini 36, una asidi amino 18 na asidi amino muhimu zaidi 9 ambazo miili yetu haina uwezo wa kuzitengeneza.

Unga wa majani ya mlonge unao uwezo wa kutibu magonjwa zaidi ya 300 mwilini, magonjwa hayo ni pamoja na :

1. HUko Afrika magharibi madaktari hutumia mlonge kutibu kisukari.

2. HUko India mlonge hutumika kutibu shinikizo la juu la damu

3. HUtibu matatizo u maumivu ya mishipa

4. Hutuliza mapigo ya juu ya moyo

5. Hutibu kansa

6. Pumu

7. Hutuliza wasiwasi

8. Kikohozi

9. Maumivu ya kichwa

10. Inazuia na kushusha ile lehemu hata ile ya juu zaidi

11. Inapunguza mafuta tumboni

12. Inaweza sawa homoni

13. Inatibu maumivu wakati wa hedhi

14. Unasafisha ini

15. Inasafisha mkojo na kibofu cha mkojo

16. Inarekebisha matatizo kwenye tezi

17. Unatibu kipindupindu na kuharisha

18. Kifua kikuu

19. Kichwa kizito

20. Uchovu

21. Mzio

22. Vidonda vya tumbo

23. Maambukizi kwenye ngozi

24. Maumivu mbalimbali mwilini

25. Huondoa madoa doa meusi kwenye ngozi

26. Husafisha damu

27. Hutibu matatizo kwenye koo

28. Huondoa makohozi mazito kooni

29. Huondoa taka na msongamano kifuani

30. Hutibu kipindipindu

31. Huondoa moto wa jicho au uvimbe kwenye jicho

32. Hutibu maambukizi kwenye macho na kwenye masikio

33. Unatibu homa

34. Maumivu kwenye maungio

35. Huondoa chunusi

36. Hutibu matatizo karibu yote ya ngozi na kinga ya mwili

37. Matatizo kwenye mfumo wa upumuaji

38. Inatibu kiseyeye

39. Huongeza uwingi wa mbegu za kiume na nguvu kwa ujumla

40. Inatibu minyoo

41. Huongeza maziwa kwa wingi kwa mama anayenyonyesha

42. Huondoa uvimbe kwenye utumbo mpana

43. Inatibu ugonjwa wa kuvimba mwili

44. Inatibu kuhara damu

45. Inatibu kisonono

46. Unatibu tatizo la kukosa usingizi

47. Unatibu homa ya manjano

48. Unatibu malaria

49. Unatibu U.T.I na matatizo mengine kwenye mfumo wa mkojo

50. Unasaidia pia kujenga na kuimarisha misuli

51. Unatibu magonjwa ya mifupa

Mlonge uansafisha mwili wako wote, unasafisha ini, figo, moyo, macho, unaimarisha meno, ngozi na nywele. Wakati unatumia mlonge unakufanya ujisikie vizuri, ujisikie mpya na mwenye nguvu. Watu wengi wanaotumia mlonge huwa ni wenye afya nzuri hata kwa muonekano tu hata wanapokuwa na umri mkubwa zaidi ya miaka 90.

Majani ya mti wa mlonge pia yanaweza kutumika kutengeneza biogas. Hutumika pia kama chakala cha wanyama kama sungura , mbuzi, ng’mbe. Mbwa n.k. Sungura wanaonekana kupenda zaidi mlonge kuliko wanyama wote
 
Mapishi Mbali mbali ya mmea wa mlonge

10. MLONGE (MORINGA)

attachment.php


Majina ya Kiswahili Mlonge, Mzunze
Kingereza: Radish tree
Jina la Kisayansi: Moringa Oleifera


Matumizi ya Moringa

Katika nchi ya Tanzania moringa huota vyema lakini huliwi kwa wingi kwani watu hawana elimu ya kutosha kuhusu utayarishaji wake. Majani mabichi na makavu, matunda machanga, mizizi na maua yaweza kutumiwa katika upishi na dawa. Majani pia hutumiwa kama malisho kwa wanyama, chavua la maua huwavutia nyuki kwa minajili ya utoaji wa asali,hutumika katika utengenezaji wa sabuni na vyombo vingine vya urembo.

Faida yake mwilini

Majani na maua ya Moringa yanavirutubisho vingi kama vitamin A (mara tatu zaidi ya karoti), vitamin C (mara tatu zaidi ya ile ya machungwa), calcium
(mara 140 zaidi ya ile inayopatikana katika maziwa ya ngombe) na potasiamu. Umetumika katika kusaidia udhibiti wa matatanisho yanayoletwa na ugonjwa wa ukimwi.


Inakostawi

Nchi zote za joto tropics na subtropics, sana sana katika sehemu za pwani, hupendelea mwinuko wa kati ya 0-500m. Hustawi sana sehemu za Ukanda wa
Bahari ya Hindi. Asili ya mmea wa Moringa ni wenyeji wa sehemu ya Sub Himalaya kaskazini magharibi mwa nchi ya India.


Uhifadhi wa majani ya moringa Majani ya Moringa hukaushwa na kusagwa ili kutengeneza unga ambao huongezwa kwenye chakula kama viazi vilivyosetwa na uji wa mahindi ama mtama ili kuongeza ubora wake.

Mapishi mbalimbali ya Mlonge

Majani ya mlonge na maharagwe

VIAMBA UPISHI

Majani ya mlonge 2 vikombe
Nyanya 1 kubwa
Kitunguu saumu 3-4 punje
Kitunguu maji 1 kikubwa
Chumvi 1⁄2 kijiko cha chai.
Mafuta ya maji 2 vijiko vya kulia chakula
Tui la nazi 1⁄2 kikombe cha chai
Maharage 1 Kikombe
Nyama/samaki/kuku 1 kikombe cha vipande
vilivyokatwakatwa ili viwe vidogo


HATUA ZA MAPISHI

1. Chemsha maharage na kuku /nyama ya ngombe/ samaki mpaka iive.

2. Osha majani ya moringa vizuri, ondoa sehemu zisizohitajika na ukatakate.

3. Ambua, osha na ukatakate kitunguu maji na ukaange hadi kilainike.

4. Ambua, osha na uponde kitunguu saumu na uongeze kwenye kitunguuu maji.

5. Osha na ukatakate nyanya, ongeza kwenye mchanganyiko na uendelee kukaanga.

6. Ongeza majani ya moringa kwenye mchanganyiko,koroga na uendelee kukaanga.

7. Ongeza chumvi na upike hadi mboga zote ziive vizuri.

Chakula hiki cha majani kinaweza kuliwa pamoja na ugali, wali, na vyakula vinginevyo.

Mlonge na Matembele

VIAMBA UPISHI

Majani ya Mlonge 2 Vikombe
Matembele 2 Fungu
Mafuta ya kupikia 3 Vijiko vya kulia
vilivyosagwa 1 Kijiko cha chai
attachment.php

Kitunguu maji 1
Vitunguu saumu 3-4 punje
Nyanya 1
Karoti ndogo 1
Tui la nazi 1⁄2 kikombe cha chai
Chumvi 1⁄2 kijiko cha chai.


HATUA ZA MAPISHI

1. Osha Moringa na Matembele vizuri huku ukitoa sehemu zisizo hitajika.

2. Tayarisha tui la nazi na upashe moto kwenye sufuria tofauti.

3. Ambua kitunguu maji, vitunguu saumu na karoti na uoshe pamoja na nyanya.

4. Katakata kitunguu, nyanya na karoti na uponde vitunguu saumu.

5. Pasha mafuta moto kwenye sufuria na ukaange kitunguu maji hadi kilainike.

6. Ongeza karoti na nyanya, koroga hadi mchanganyiko uwe laini. Ongeza chumvi na kitunguu saumu na ukoroge.

7. Ongeza tui moto la nazi na ukoroge hadi kufikia kuishia tui.

Mboga hii yaweza kuliwa na ugali, mihogo, wali na vyakula vinginevyo.
mlonge 2.png
mlonge 3.png
mlonge 4.png
MLONGE.jpg
 
Naomba kujua mlonge unasaidiaje kama tiba? wenye kujua naomba mtuhabarishe.

=============

MTI WA MLONGE WENYE MAAJABU NA FAIDA ZAKE ZAIDI YA KUMI.

Eileen Kasubi ni mtanazania wa kwanza mwanamke ambaye ni mjasiriamali wa kazi za mikono aliyefanikiwa kufanya utafiti juu ya mti MLONGE ambao umekuwa na faida kubwa hapa nchini na kufanikiwa kuzitambua zaidi ya faida kumi za mti huo unaopatikana kwa uchache hapa Tanzania.

Mjasiriamali huyu anaweka wazi namna ya MLONGE ulivyokuwa na faida lukuki lakini kubwa kuliko yote ni kwamba watanzania wengi bado hawajazitambua faida za mti huu ambao ni adimu kwa kiasi fulani hapa Tanzania licha ya wajasiriamali hawa kuhamasisha.

Bi. Kasubi anasema MLONGE ni mti wenye maajabu hasa katika matumizi yake kuanzia majani yake, magome,mbegu ambazozimekuwa zikitoa tiba, kinga pamoja na lishe, haya ndiyo maajabu ya mtyi MLONGE.

KAMPUNI YA Makai Moringa Enterprises inayodiri na mkakati huu wa kutafiti kwa kina zaidi juu mti Mlonge, Bi. Kasubi ambaye ni mkurugenzi wa Makai Moringa, anasema kwa miaka mingi akishirikiana na wafiti wenzake ambao ni wajasiriamali kutoka nchini Malawi na Kenya, wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuzitambua faida ya mti huo na hivi sasa wanachopigania ni mtaji mkubwa ambao utaweza kuwaendeleza wajasiriamali wanaotafiti baadhi ya matumizi ya miti hapa Tanzania.

Mkurugenzi Kasubi anasema mafanikio ambayo anajivunia kuyapata katika utafiti wake juu ya mti huo Mlonge ni pamoja na kufanikiwa kuutambua kuwa ni miongoni mwa miti ambayo inatibu baadhi ya maradhi sugu kama vile ugonjwa wa kisukari ambao umekuwa tatizo katika maisha ya jamii ya ya kitanzania.

Bi.Eileen Kasubi anazianisha bidhaa zake zitokanazo na mti huo wa MLONGE ambapo anasema mafanikio ya mti huo na faida zake ni kama ifuatavyo: Majani ya mti wa MLONGE yakisagwa unga wake hutumika kwa lishe ya mwanadamu.

Anaendelea kusema katika hayo majani pia bado yanaweza kutibu na kukinga maradhi zaidi ya magonjwa 300 kitu ambacho unaonyesha maajabu ya kutibu na kutumika kama lishe.

Si hivyo tu, unga huo wa mlonge bado unanafasi kubwa kulinda afya ya mwanadamu pamoja na kurutubisha mifumo mbalimbali ya mwili
hapo ndipo utagundua MLONGE ni mti wa maajabu.

FAIDA ZA MBEGU ZAKE

Mbegu za Mlonge hutibu maradhi kama Malaria, Saratani ya tumbo, hupunguza sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji, huongeza kinga ya mwili CD4s,

Mbegu hizo za mti huo wa ajabu bado zinahamasisha jamii kuamka na kuutambua umuhimu wa mti MLONGE kwa mbegu hizo hutoa mafuta ya kupikia pamoja na mafuta ya kujipaka mewilini kwa nyakati tofauti.

Kwa upande wa mafuta ya kupikia chakula Bi. Kasubi anasema mafuta yake ya kupikia huua sumu kwenye chakula yaani Bacteria na huondoa cholesterol. Mafuta ya kupaka mwilini yaani (Moringa Skin Care Oil).

Mlonge unaendelea kutoa faida kemkem kwa mtanzania na jamii yote duniani kwani umeweza kuwapendelea na wanamichezo kwa kutoa mafuta ambayo yanachua pindi mchezaji anapokuwa ameshikwa na misuli wakati akiwa anacheza, Bi. Kasubi anaainisha kwamba katika utafiti wa kampuni yake amefanikiwa kutambua faida nyingine ya matumizi ya mti huo baada ya kufanikiwa kutengeneza mafuta ya kuchua na kuondoa maumivu yatokanayo na kukaza kwa misuli ya mwili yaani (MORINGA MASSEGE OIL)ambayo huondoa maumivu ya mgongo, kiuno, miguu, hutibu baridi, na hupasha misuli joto.

Bado mti huo unazidi kushika nafasi za juu kabisa hasa pale mtafiti huyu mwanamke ambaye amepigana kwa miaka minane sasa tangu aanze kufanya utafiti kabla ya kuungana na wajasiriamali wenzake, pia amefanikiwa kugundua kuwa MLONGE unao uwezo wa kutoa sabuni za aina mbalimbali zikiwemo (Toilet soap) na kutibu magonjwa mengine mbalimbali kama vile ugonjwa wa ngozi, fangazi, chunusi, mba na hulinda ngozi kwa ,muda mrefu.

Kama hiyo haitoshi, bado mti wa mlonge unaendelea kutetea miti mingine ambayo bado haijafanyiwa utafiti na kampuni hiyo, Bi. Kasubi anasema katika utafiti wake amegundua kuwa mti wa MLONGE umeweza kutoa mafuta ya kupaka kwenye nywele na huiimarisha nywele vilivyo na kuzifanya kuwa na rutuba tofauti na mafuta mengine yatumikayo hapa nchini, huu ni MTI WA MAAJABU MLONGE, amesema Eileen Kasubi Mkurugenzi wa Makai Moringa (Mlonge) anayepatikana katika jengo la Pamba House karibu na Imalaseko Posta mjini Dar es Salaam.

 
MLONGE
Unga wa majani ya Mlonge ambao ni lishe, tiba na kinga hutibu magonjwa kama shinikizo la damu,kupooza viungo au kufa ganzi,homa ya matumbo(typhoid),kuwashwa mwili,vidonda vya tumbo,malaria sugu, enia, upele n.k.

Mbegu za Mlonge hutibu Malaria, Saratani ya tumbo,hupungusa sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji,huongeza kinga ya mwili CD4s. (Tumia mbegu 3x3 muhimu kila ukitafuna mbegu tatu kumbuka kutumia maji glass 3 au zaidi)

Maganda(magome) ya Mlonge husaidia kusafisha maji(water treatment).

Mizizi hutumika kutibu watu walio na malaria sugu au watu wanaopata homa ya usiku au wanaotiririka sana jasho wakati wa homa. Mizizi hutumika kwa kusaga unga wake na kutumia kijiko cha chai mara tatu kwa siku.

Pia mgonjwa anatakiwa kutafuna mbegu tatu mara tatu kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita.

Unahamasishwa na kushauriwa angalao nyumbani kwako uwe na mashina kadhaa ya mmea huu kwa matumizi yako.
 

Attachments

  • moringa.docx
    29.4 KB · Views: 958
[h=6]DRUMSTICK TREE Overview Information[/h]Drumstick tree is a plant that is native to the sub-Himalayan areas of India, Pakistan, Bangladesh, and Afghanistan. It is also grown in the tropics. The leaves, bark, flowers, fruit, seeds, and root are used to make medicine.

Drumstick tree is used for "tired blood" (anemia); arthritis and other joint pain (rheumatism); asthma; cancer; constipation; diabetes; diarrhea; epilepsy; stomach pain; stomach and intestinal ulcers; intestinal spasms; headache; heart problems; high blood pressure; kidney stones; fluid retention; thyroid disorders; and bacterial, fungal, viral, and parasitic infections.

Drumstick tree is also used to reduce swelling, increase sex drive (as an aphrodisiac), prevent pregnancy, boost the immune system, and increase breast milk production. Some people use it as a nutritional supplement or tonic.

Drumstick tree is sometimes applied directly to the skin as a germ-killer or drying agent (astringent). It is also used topically for treating pockets of infection (abscesses), athlete's foot, dandruff, gum disease (gingivitis), snakebites, warts, and wounds.

Oil from drumstick seeds is used in foods, perfume, and hair care products, and as a machine lubricant.

Drumstick tree is an important food source in some parts of the world. Because it can be grown cheaply and easily, and the leaves retain lots of vitamins and minerals when dried, the drumstick tree is used in India and Africa in feeding programs to fight malnutrition. The immature green pods (drumsticks) are prepared similarly to green beans, while the seeds are removed from more mature pods and cooked like peas or roasted like nuts. The leaves are cooked and used like spinach, and they are also dried and powdered for use as a condiment.

The seed cake remaining after oil extraction is used as a fertilizer and also to purify well water and to remove salt from seawater.


[h=4]How does it work?[/h]Drumstick tree contains proteins, vitamins, and minerals. As an antioxidant, it seems to help protect cells from damage.
TAKEN BY MOUTH
  • "Tired blood" (anemia).
  • Arthritis.
  • Asthma.
  • Cancer.
  • Constipation.
  • Birth control.
  • Diabetes.
  • Diarrhea.
  • Epilepsy.
  • Stomach pain (gastritis).
  • Stomach and intestinal ulcers.
  • Headache.
  • Heart problems.
  • High blood pressure.
  • Kidney stones.
  • Swelling (inflammation).
  • Thyroid disorders.
  • Infections.
  • Increasing breast milk production.
  • As a nutritional supplement.
  • Stimulating immunity.
  • Increasing sex drive.
  • Other conditions.
APPLIED TO THE SKIN
  • Athlete's foot.
  • Dandruff.
  • Warts.
  • Skin infections.
  • Snakebites.
  • Gum disease (gingivitis).
  • Other conditions.
More evidence is needed to rate the effectiveness of drumstick tree for these uses.


[h=6]DRUMSTICK TREE Side Effects & Safety[/h]
Drumstick tree leaves, fruit, and seeds might be safe when eaten as food. However, it's important to avoid eating the root and its extracts. These parts of the plant may contain a toxic substance that can cause paralysis and death.

There isn't enough information to know if drumstick tree is safe when used in medicinal amounts. [h=4]Special Precautions & Warnings:[/h]Pregnancy and breast-feeding: It's UNSAFE to use drumstick tree if you are pregnant. Chemicals in the root, bark, and flowers can make the uterus contract, and this might cause a miscarriage.

It's also best to avoid drumstick tree if you are breast-feeding. There isn't enough information to know whether it is safe for a nursing infant.
[h=6]DRUMSTICK TREE Interactions [/h]We currently have no information for DRUMSTICK TREE Interactions

[h=6]DRUMSTICK TREE Dosing[/h]The appropriate dose of drumstick tree depends on several factors such as the user's age, health, and several other conditions. At this time there is not enough scientific information to determine an appropriate range of doses for drumstick tree. Keep in mind that natural products are not always necessarily safe and dosages can be important. Be sure to follow relevant directions on product labels and consult your pharmacist or physician or other healthcare professional before using.

READ ALSO Trees for Life Journal - Moringa oleifera: A Review of the Medical Evidence for Its Nutritional, Therapeutic, and Prophylactic Properties. Part 1.
Table 1. Reported nutritional, therapeutic & prophylactic uses of Moringa oleifera


Traditional Use
Condition/Effect[SUP]a[/SUP]

Plant Part[SUP]b[/SUP]
References[SUP]c[/SUP]
ANT Antimicrobial / Biocidal
LFSPRBGO
8, 13, 19, 24, 27, 31, 34, 64, 68, 100, 104, 114, 115, 126, 140, 151, 160, 161, 162



Bacterial
LFS
25, 26, 55, 63, 77-81, 149
Urinary Tract Infection
L
141
Typhoid
G
47
Infection
LF
47
Syphilis
G
47
Dental Caries/Toothache
RBG
47



Fungal/ Mycoses
O
111
Thrush

88, 111



Viral


Common cold
FRB
47
Epstein-Barr Virus (EBV)
L
104
Herpes Simplex Virus (HSV-1)
L
84
HIV-AIDS
L
1, 124
Warts
S
47



Parasites


Dranunculiasis (guinea-worm)

36
Helminths
LFP
47
Schistosomes
S
113
Trypanosomes
LR
95



Other / Not Attributed to a Specific Pathogen


Skin (Dermal)
O S
15
Hepatic
L
6
Fever
LRGS
47
Earache
G
47
External Sores/Ulcers
LFRB
15
Bronchitis
L
47
Throat Infection
F
47
Water treatment (general)
S
11, 50, 75, 86, 169



AST Asthma
RG
47



CAN Cancer Therapy / Protection
LFPBS
12, 17, 28, 39, 45, 59, 61, 64, 104, 115
Anti-tumor
LFSB
45, 48, 57, 61, 87
Prostate
L
47, 48
Radioprotective
L
132
Skin
P
12



CIR Circulatory/Endocrine Disorders
LFSPR
56, 93
Anti-anemic
L
47, 125
Anti-hypertensive
LP
40, 41, 42, 43, 44, 53, 83, 137
Cardiotonic
R
47
Diabetes/hypoglycemia
LP
6, 45, 71, 87, 101, 167
Diuretic
LFRG
6, 14, 62
Hypocholestemia
L
52, 94
Thyroid
L
153
Tonic
F
47
Hepatorenal
LR
93, 120



DET Detoxification
BO
76, 135, 166
Antipyretic

148
Purgative
O
47
Snakebite
B
47
Scorpion-bite
B
47



DIG Digestive Disorders
LSRBG
53
For TRTMNT of:


Colitis
LB
47
Diarrhea
LR
47, 62, 64
Digestif
B
47
Dysentery
LG
47
Flatulence
R
47
Ulcer / Gastritis
LS
3, 115, 136



INF Inflammation
LFSPRG
14, 28, 35, 45, 62, 64, 68, 110, 131, 160, 161
Rheumatism
LFSPRG
28
Joint Pain
P
47
Edema
R
47
Arthritis
S
47



IMM Immunity
SO
69
Immune-stimulant
S
69
Lupus
O
28



NER Nervous Disorders
LFRBGO
58, 59, 62, 96
Anti-spasmodic
SR
14, 53
Epilepsy
RB
47
Hysteria
FRBO
47
Headache
LRBG
47



NUT Nuritional
LSBO
6, 7, 18, 22, 28, 30, 31, 32, 46, 47, 48, 51, 65, 66, 67, 70, 92, 102, 112, 116, 133, 163



Antinutritional factors
B
88, 89, 90, 110, 127, 128, 139, 156, 164, 165
Antioxidant
LO
110, 147
Carotenoids
L
29, 105, 152
Energy
LSO
85
Goitrogen
S
2
Iron deficiency
LS
16
Oil quality
O
5, 98, 110, 158, 159
Protein
LS
47
Vitamin/Mineral deficiency
LS
7, 9, 54, 56, 85, 119



REP Reproductive Health
LFPRBGO
44, 53, 64, 121, 122
Abortifacient
FRBG
106, 107, 155
Aphrodisiac
RB
47
Birth Control
B
45, 53, 142-146
Lactation Enhancer
L
47
Prostate function
O
47



SKI Skin Disorders
LRSG
160, 161
Antiseptic
L
47
Astringent
R
47
Pyodermia
S
15
Rubefacient
RG
47
Vesicant
R
47



GEN General Disorders/Conditions
LFSPRBO
4, 6, 8, 20, 21, 45, 48, 64, 66, 67, 68, 73, 74, 82, 91, 92, 99, 102, 103, 109, 116, 117, 118, 123, 125, 128, 129, 130, 134, 150, 163
Bladder
OS
47
Catarrh
LF
47
Gout
RO
47
Hepatamegaly
R
47
Lactation
L
47
Low.Back/Kidney Pain
R
47
Scurvy
LSRBO
47
Splenomegaly
R
47
"Tonic"
 
hi!i kindly request NGOSHWE to put in swahili the uses of Moriga oliefera so that most tanzanian can understand its usefulness.its a movolous lecture i benefited alot.
its true that this forums is of great thinkers...pull it up
 
hi!i kindly request NGOSHWE to put in swahili the uses of Moriga oliefera so that most tanzanian can understand its usefulness.its a movolous lecture i benefited alot.
its true that this forums is of great thinkers...pull it up

Sasa unamshauri mwenzako atumie kiswahili wakati huo huo wewe mwenyewe umetumia kiingereza.
 
Nimesikia mengi kuhusiana na mti wa Mlonge lakini hii ni kali zaidi
CAPE TOWN, (IPS). Wakati tatizo linalipolikabili Bara la Afrika, watu wanaangalia uwezekano wa kupata misaada kutoka kwenye mashirika ya kimataifa kutoka nje ya bara hilo.

Lakini hali ya ukame inayoongezeka kwa kasi, miti yenye kuhimili ukame huku ikiwa na majani yenye viini lishe vingi inaweza kuwasaidia watu maskini, pia maeneo ya usalama wa chakula na utapiamlo, wao wenyewe.

Shamba lenye hekta 15 lilipandwa miti ya Mlonge au wengine huuita mti wa miujiza ambao kwa Kiingereza unaitwa Moringa Oleifera, tayari umeshaanza kuleta mabadiliko katika jimbo moja maskini zaidi la Afrika Kusini la Limpopo.

Majani ya Mlonge yamepachikwa jina la chakula chenye viwango kwasababu wanasayansi waligundua yana kiasi cha madini ya Kalisium yanayoweza kupatiakana katika glasi nne za maziwa, kiasi cha vitamini c inayopatikana kwenye machungwa saba, Potasium ya kwenye ndizi mbivu tatu. Pia unapata kiasi cha madini ya chuma mara nne zaidi ya kiasi kile kinachopatikana kwenye spinachi. kiasi cha vitamani A mara nne zaidi ya kile kinachopatikana kwenye karoti na kiasi cha protini mara mbili zaidi ya kile kinachopatikana kwenye maziwa. Ukiwa na mti wa Mlonge ni sawa na kuwa na Supermarket kwenye mti.
Mavis Mathabatha aliyewahi kuwa mwalimu kutoka Tooseng, amekuwa akifanya bidii ya kufungua mashamba ya Mlonge kwa kipindi cha miaka mitatu sasa ambalo litamuwezesha kuzalisha majani ya kutosha ya Mlonge ili kusaidia kuleta mabadiliko katika jamii yake.
"Nataka kuleta mabadiliko katika jimbo langu na nchi nzima kupitia mradi huu," alisema.
Mwaka 2009, alianza kuvuna na kuyakausha na kisha kuyasaga majini ya Mlonge kutoka kwenye miti michache aliyokuwa ameipabnda.
Unga huo wa Mlonge alikuwa ukiwachanganyia watoto 400 kutoka katika familia masikini waliokuwa wakipata chakula kutoka kwenye kituo maalum.
Kituo hicho kinalisha watoto wanaotoka katika familia zenye kipato kidogo ambacho kiko chini ya dola 250 kwa mwezi.
Hii inahusuisha watoto wote wa kike na kiume kutoka kwenye jamii hiyo ambayo ina tatizo la ukosefu wa ajira, umasikini na utapiamlo, wengine wana maambukizi ya UKIMWI.

"Matokeo yake yalikuwa dhahiri kwa muda mfupi sana, Afya za watoto ziliboreka kwa muda mfupi.
Anasema Elizabeth Serogole, meneja wa kituo hicho cha kulisha watoto ambaye anafanya kazi kwa kushirikiana na Mathabatha.
Anasema watoto wengi waliokuwa wakionesha kuwa na utapiamlo, kama vile vidonda kwenye ngozi walianza kupona mara baada ya kula mlo huo uliochanganywa na unga wa Mlonge.

Nyongeza hiyo ya Mlonge kwenye chakula chao iliwasaidia kupambana na magonjwa mengine yaliyojitokeza, pia iliwasaidia kuboresha uwezo wao wa kiakili," anasema Seregole.

"Wengi sasa wanaweza kusoma vizuri shuleni," anasema. Walichokuwa wanahitaji ni kjiko kimoja cha unga wa molonge katika chakula chao kwa siku. Dk.Samson Tesfay anayseoma Afrika Kusini kwenye chuo kikuu cha Zulu Natal idara inayohusika na masuala ya mbogamboga na matunda,alisema Mlonge ni mmea wenye kutenda maajabu kwenye lishe.

"Mlonge ni mmea wa kipekeeunaoweza kuutumia kwa faida nyingi, kama vile dawa, chakula, kuponyesha viungo mwilini na kusaidia kupambana na utapiamlo," anasema.

Source-Gazeti la Nipashe Ijumaa Februari 24, 2012

Binafsi nimeshasikia kuwa Mlonge unatibu magonjwa 300, bila ya kusahau kansa,maralia,vidonda vya tumbo,kuondoa sumu mwilini na hata kuongeza nguvu za kiume. Maderava wengi wa safari ndefu hutumia Mlonge kuondoa uchovu. Mlonge watu wa kule Tanga wanatumia kama mti wa kujengea fensi, Uzaramoni umepandwa karibu kabisa na vyoo vyao, Dodoma na Morogoro umejaaa tele. Dar mbegu zake zinauzwa kwa Shilingi 1000 kwa pakti.

Mbegu hizo zina dozi ya 3x3x3 na ukizila kwa wingi huweza kukufanya kuhalisha na kutoa uchafu mwilini. Tafakari ndugu yangu dawa tunazo tunatimia madawa yenye sumu yaliyotayalishwa na wazungu.... Tafakari.
 
Hii ni thread educative, hongera sana.These are the kind of threads one would like to read,sio thread za kijinga jinga tu.Okay,ninayo Milongelonge shambani kwangu.

Lakini taste ya mbegu zake au unga wake mm, inahitaji moyo.Sijawahi kula majani yake kama mboga,lakini nasikia nayo ni extremely nutritious.Kwa wale wanaoweza kula unga wake while mixed with warm water,nasikia ni dawa nzuri ya kisukari pia.
 
Huwa natumia moringa powder kwa kutibu malaria, inakinga malaria pia kama ukijizoesha kunywa kama chai, jaribu na hakika malaria utaisikia redioni..,.

Inatibu na sukari, iwe ya kupanda au kushuka..

pia ikichanganywa na asali ya nyuki wadogo ni dawa nzuri sana kwa kifua/kikohozi na mafua!
 
Mkuu , mlonge nimeupanda hapa home yaani ndani ya miezi nane limekuwa ni bonge la mti inabidi kukata matawi. Yaani kila kitu kuanzia majani, maua, mbegu n.k kina virubisho vingi. Mimi huwa nayatafuna majani kama mbuzi. Bado najiuliza kwanini huu mmea hautangazwi sana hapa tanzania.
 
huwa natumia moringa powder kwa kutibu malaria, inakinga malaria pia kama ukijizoesha kunywa kama chai, jaribu na hakika malaria utaisikia redioni..,.

Inatibu na sukari, iwe ya kupanda au kushuka..

Pia ikichanganywa na asali ya nyuki wadogo ni dawa nzuri sana kwa kifua/kikohozi na mafua!

ila asali za town hapo mmm unawza kukupa molasense!
 
Duh! Yaani pamoja na sifa zote hizo lakini bado wala sifahamu huo mti unafananaje!! Kwa wakazi wa dar, je kuna mtu anaweza kunijuza unapatikana sehemu zipi ili angalau nikauone ulivyo?!
 

Similar Discussions

10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom