Davis Mosha akusanya zaidi ya milioni 400 kanisa la KKKT-Arusha Mjini

Anasura ya kimafia aisee!,type hizi ukikosea tu njia unapigwa mbaya sana
Kwahiyo ni mimi tu ndio nimegundua kwamba huyo jamaa anatakatisha pesa zake kwa kisingizio kwamba kapewa na rafiki zake kama sadaka kwa ajili ya kanisa? Yaaani ni mimi tu?! Hivi wanatuchuliaje hawa watu, huo upendo wa Mungu wa hivyo unakujaje wakati hata laki ukimdhulumu huyo jamaa inaonekana anaweza kukumaliza.. , au laa inawezekana hizo pesa ni za kanisa ila zinatafutiwa sababu ya kuingizwa kwenye akaunti ya Kanisa, wakiulizwa waseme ni sadaka wamepewa, kumbe wanatakatisha tu
 
Kwahiyo ni mimi tu ndio nimegundua kwamba huyo jamaa anatakatisha pesa zake kwa kisingizio kwamba kapewa na rafiki zake kama sadaka kwa ajili ya kanisa? Yaaani ni mimi tu?! Hivi wanatuchuliaje hawa watu, huo upendo wa Mungu wa hivyo unakujaje wakati hata laki ukimdhulumu huyo jamaa inaonekana anaweza kukumaliza..
Hivi hilo neno Don lina maana gani?

Sent from my SM-G980F using JamiiForums mobile app
 
Yatima hawaishi kama ambavyo kipato chake kinavyoongezeka, mahekalu yanayokaa wazi wiki nzima kusubiri ibada mara moja kwa juma ni upuuzi wakati kuna watoto bado wengi mitaani.

Kwanza hizo sadaka za kujitangaza wakati Biblia yao inawataka mkono wa kushoto ukitoa wakulia usijue naamini hawajaisoma vizuri! Mbele ya fedha hata askofu aweza pindisha maandishi.
Sahihi sana mkuu
Binafsi nina mtazamo kama wako kabisa na sadaka huwa natoa kiasi kidogo sana nyingine naziacha mtaani
 
Imani inachezewa wewe unaongelea kuishi upendavyo? Waamini wanaongozwa na Amri na miiko, acha ujinga we jamaa, mambo yako ya kiimani ukiutangazia umma ni kwamba unataka maoni ya umma.
Sasa wewe unataka kumpangia mtu maisha aishi kama upendevyo? Hela atafute mwenyewe matumizi umpangie wewe?

Tafuta hele ndugu uipangie matumizi wewe?

Pia usirudia tena kuniita mjinga maana nikianza kukuporomoshea matusi hii account utaifunga!

Tujibizane tu kwa ustaarabu!
 
Huyu Jamaa kipindi cha Mwandazake alizimika kabisa baada ya lile sakata lake na Maafisa Wa Serikali..
 
Mfanyabiashara Davis Mosha leo ameongoza Harambee ya ujenzi wa Kanisa, Katika misa ya harambee hiyo iliyoendeshwa katika Kanisa la KKKT usharika wa Arusha Mjini, Davis Mosha aliyeongozana na Familia yake aliweza kuchangisha jumla ya kiasi cha Shilingi Milioni mia nne.

Akizungumza katika Hafla hiyo fupi kanisani hapo, Davis Mosha alisema yeye pamoja na rafiki zake aliowashirikisha kwa Muda mchache baada ya kujua hitaji la kanisa hilo waliweza kumuunga mkono na kumuomba Mchango wao utambuliwe kama sadaka katika kufanikisha lengo hilo la kanisa. Huku akiahidi kuendelea kuwa bega kwa bega na kanisa hilo mpaka kuhakikisha lengo kuu linakamilika kwa kiwango kinachohitajika.

"Leo kupitia waumini wenzangu pamoja na Rafiki zangu tumeweza kukusanya zaidi ya Shilingi Milioni Mia nne, Huu mi mwanzo mzuri katika Ujenzi wa kanisa na kukuza huduma ya kanisa, Nitoe wito kwa yeyote atakayeguswa kushiriki katika jambo hili basi ajiungane nasi katika kukamilisha kazi ya Mungu." Alisema Davis Mosha.

Ikumbukwe kuwa Mfanyabiashara Davis Mosha amekua Mstari wa mbele katika kujitoa katika ujenzi wa nyumba za ibada ikiwemo Misikiti na Makanisa katika maeneo mbalimbaliView attachment 2010522

Sent from my SM-G980F using JamiiForums mobile app
Kutakatisha pesa tu hapo Hamna cha nini wala nini
 
Yatima hawaishi kama ambavyo kipato chake kinavyoongezeka, mahekalu yanayokaa wazi wiki nzima kusubiri ibada mara moja kwa juma ni upuuzi wakati kuna watoto bado wengi mitaani.

Kwanza hizo sadaka za kujitangaza wakati Biblia yao inawataka mkono wa kushoto ukitoa wakulia usijue naamini hawajaisoma vizuri! Mbele ya fedha hata askofu aweza pindisha maandishi.
Hiyo ni Harambee kutimiza lengo Fulani .Tofauti na sadaka
 
Kwahiyo ni mimi tu ndio nimegundua kwamba huyo jamaa anatakatisha pesa zake kwa kisingizio kwamba kapewa na rafiki zake kama sadaka kwa ajili ya kanisa? Yaaani ni mimi tu?! Hivi wanatuchuliaje hawa watu, huo upendo wa Mungu wa hivyo unakujaje wakati hata laki ukimdhulumu huyo jamaa inaonekana anaweza kukumaliza..
Marafiki zake unawajua mkuu? GSM, OIL COM na wafanyabiashara wenzie wakubwa wa mafuta hiyo 400m kwa circle yake ni peanut
 
Marafiki zake unawajua mkuu? GSM, OIL COM na wafanyabiashara wenzie wakubwa wa mafuta hiyo 400m kwa circle yake ni peanut
Ni money Laundry scheme, kwani GSM na oilcom ndio nini? Hao wanauza hadi maji ya buku, yaani buku wanaitafuta, kitu kimoja unatakiwa ujue kuhusu pesa, pesa huwa haimtoshi mtu, na pesa kubwa huanza na pesa ndogo, hiyo 400m ni pesa nyingi sana hata kwa billgates, hata siku moja hakupi tu hivi hivi
 
Anatakatisha tu, baada ya hapo inaingizwa kwa akanti maisha yanaendelea
Wakiulizwa mmetoa wapi pesa nyingi ghalfla hivi wanakwambia tumepokea Sadaka, wakiulizwa nani katoa sadaka nyingi hivi wanasema Davis Mosha, Mosha akiulizwa anasema ni Marafiki zake ndio walimpa apeleke, akiulizwa ni akina nani hao atasema Sadaka ni siri, sipaswi kiwataja, kwisha mchezo
 
Yatima hawaishi kama ambavyo kipato chake kinavyoongezeka, mahekalu yanayokaa wazi wiki nzima kusubiri ibada mara moja kwa juma ni upuuzi wakati kuna watoto bado wengi mitaani.
Kama hukumshauri jinsi ya kupata...Usimpangie jinsi ya kutumia.

Wtoto wengi mitaani; wewe umesaidia wangapi?!
 
Back
Top Bottom