David Mwaibula, aliyebuni mistari ya daladala Dar es salaam yupo wapi?

Mbonea

JF-Expert Member
Jul 14, 2009
640
20
1624435659108.png

Wadau,

Najua mtakuwa mnamkumbuka sana huyu "mheshimiwa" kwa style aliyokuja nayo ya kupiga ufito wa rangi tofauti tofauti kwa kila daladala za jijini ili iwe rahisi kwa abiria kutambua gari husika linapoishia kitu ambacho mikoa mingine ilikuja ikaiga. Pongezi zake!

Lakini ilikuaje akapoteza nafasi yake na kupewa mtu mwengine?

Na je, mchango wake haukuwa "effective" to the extend of being withdrawn?

Where his he right now?

Mchango wa huyu Ndugu ni mkubwa kweli hasa kwa abiria tunaotumia usafiri wa daladala kwenda hapa na pale.

Utaratibu ulioanzishwa chini yake wa daladala kuandikwa njia unatusaidia sana hivi sasa na kutupunguzia gharama. Sipati picha ningekuwa natumia kiasi gani kwa siku kutoka na kurudi Kimara ninapojibanza. Sasa hivi hata konda akiitia mwisho Ubungo napanda tu ili mradi ni Kimara

Sijui yuko wapi, lakini mchango wake binafsi ninauthamini sana. Mwenyezi amjalie popote alipo Mheshimiwa sana David Mwaibula

Huyu Mwaibula alifanya kazi ya kusimamia na kubuni njia mbalimbali ili kupunguza foreni na kutumia gharama ndogo kusafiri.Mfano alibuni njia ndefu kama kutoka G'lamboto Ubungo,Mbagala mwenge,n.k.Alikuwa na mikakati mingi mizuri.Je jembe hili limetupwa wapi na mpini wake?
====

UNAMFAHAMU ALIYEBUNI MISTARI YA DALADALA DAR ES SALAAM?

Mabasi ya usafiri wa abiria Jijini Dar es Salaam yametofautishwa kwa rangi kulingana na barabara yanazopipa mabasi hayo sambamba na maeneo yanakotoka.

Mfumo huu umekuwa msaada mkubwa kwa abiria kwa kuweza kuwarahisishia kufahamu kwa haraka barabara ambayo gari inapita hivyo kuondoa sintofahamu juu ya kule wanakoelekea.

Licha ya hilo, mfumo huu umelisaidia Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama Barabarani kuweza kuwadhibiti madereva wanaoiba ama kukatisha ruti.

Kama msafiri ni mgeni na anataka kwenda Temeke au Tandika basi daladala zenye mstari wa kijani ndizo atakazopanda.

Kwa abiria anayeelekea Banana, Kitunda na Gongolamboto daladala zenye mstari wa rangi ya chungwa linaloiva ndiyo anazopaswa kupanda.

Halikadhalika yule wa kuelekea Mbagala, Temeke au Mbande kupitia Kilwa Road basi daladala zenye mstari wa rangi ya jani kavu ndizo atakazopanda.

Kwa wale wanaopita Morogoro Road kuelekea Ubungo, Kimara hadi Kibamba gari zenye mstari mwekundu ndizo zenyewe hasa kupanda.

Kuna mistari mingi sana na tofauti ambayo kwa hakika kama tutaendelea kuielezea hapa hatutamaliza kuichambua.

Swali la kujiuliza hapa ni;

NANI ALIYEBUNI RANGI HIZI ZA DALADALA?

Mzee David Mwaibula almaarufu "Makofia" aliyekuwa Mwenyekiti wa Mamlaka ya Leseni za Usafiri Dar es Salaam (DTLA) ndiye mbunifu na muasisi wa mfumo huu wa kupaka daladala mistari.

Ubunifu wa Mzee David Mwaibula uliigwa hata na Mamlaka zingine za Miji na Majiji Tanzania Bara.

Mara ya mwisho kuonekana hadharani Mzee David Mwaibula ilikuwa mwaka 2016 kipindi ambapo Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipotembelea mradi wa Mabasi yaendayo kwa haraka (DART).

Hakika Mzee wetu David Mwaibula anastahili pongezi za dhati kwa ubunifu huu ambao umeweza pia kuzinufaisha Mamlaka kama VETA.

Tuwaenzi Wazee wetu.
 
Last edited by a moderator:
yupo tu hapa mjini daily tunagongana naye huku Sinza kwenye sebule yetu pale T Garden
 
Jamani Amekwenda Zake IRINGA KULIMA NYANYA.
....Duh!! Nakumbuka alikuwa na dala dala lake kubwa akaliita City Train linaenda njia zote hapa mjini...Jioni tunakutana King Star Bar Sinza anajitobolesha!!!! I like him alibuni kitu kizuri sana kuhusu hizi route za dala dala na rangi zake!!!
 
Wadau, najua mtakuwa mnamkumbuka sana huyu "mheshimiwa" kwa style aliyokuja nayo ya kupiga ufito wa rangi tofauti tofauti kwa kila daladala za jijini ili iwe rahisi kwa abiria kutambua gari husika linapoishia kitu ambacho mikoa mingine ilikuja ikaiga. Pongezi zake...!


Lakini ilikuaje akapoteza nafasi yake na kupewa mtu mwengine?

Na je, mchango wake haukuwa "effective" to the extend of being withdrawn?

Where his he ryt now?

Mkuu Mbonea

David Mwaibula style yake ya kufanyakazi haitakiwi Tanzania.Nchi yetu inataka blah blah nyingi ukionekana unafanyakazi lazima utaondolewa kwenye system.
 
Mkuu Mbonea

David Mwaibula style yake ya kufanyakazi haitakiwi Tanzania.Nchi yetu inataka blah blah nyingi ukionekana unafanyakazi lazima utaondolewa kwenye system.

labda ndio maana kaamua kwenda kuliendeleza jimbo la iringa mjini akifanikiwa katika mbio zake
 
Mkuu Mbonea

David Mwaibula style yake ya kufanyakazi haitakiwi Tanzania.Nchi yetu inataka blah blah nyingi ukionekana unafanyakazi lazima utaondolewa kwenye system.


Ha ha ha! kwa hiyo madili yake haya kuweka mianya ya rushwa ili watu wale?
 
The guys was very conservative mkuu wangu mbonea katika mambo yake na ndio maana leo katika usafiri wa jiji umeweza kukaa vizuri sana katika utaratibu wake
 
huyu bwana alikubalika sana sisi wananchi wa kawaida hatukuona mapungufu zaidi ya kuona umahili wake ulivyokuwa na ndio maana tunamkumbuka........tumtakie kila la kheri.........angerudishwa angefanya zaidi ila kama aliwakosea wakubwa basi imekula kwake..............
 
Mwaibula was one of the hopeless people. Alikuwa na siasa za design ya Makamba, hakuna lolote la maana alilofanya. Tatizo la usafiri kuwa shaghalabagala Dar es salaa haliwezi kushughulikiwa kwa kupaka magari rangi, kunatakiwa njia yenye akili zaidi kama wanazotumia wenzetu wa nchi zilizoendelea. Sioi Mwaibula style, na akienda Iringa huenda atapiga kelele kelele tu, naona anfaa kufanya kazi ofisi moja na Makamba!
 
Well done Mr. Mwaibula and enjoy your retirement time. Every sensible daladala bus comuter in DSM appreciates what you did.
 
Mnamkumbuka A.L.Mrema, nae alikuwa hivyo hivyo kwa mafisadi, Kwani sasa yuko wapi?
 
Mwaibula was one of the hopeless people. Alikuwa na siasa za design ya Makamba, hakuna lolote la maana alilofanya. Tatizo la usafiri kuwa shaghalabagala Dar es salaa haliwezi kushughulikiwa kwa kupaka magari rangi, kunatakiwa njia yenye akili zaidi kama wanazotumia wenzetu wa nchi zilizoendelea. Sioi Mwaibula style, na akienda Iringa huenda atapiga kelele kelele tu, naona anfaa kufanya kazi ofisi moja na Makamba!

Bongolander sidhani kama unamtendea haki Mwaibula kwa kulinganisha mfumo wa usafiri Tanzania na nchi zilizoendelea wakati akiwa madarakani. Ungetathmini 'u-hopelessness' wake kwa kulinganisha hali ilivyokuwa nzuri au mbaya kabla hajaingia madarakani na hali ilivyokuwa wakati anamaliza muda wake. Kuilinganisha Tanzania na nchi zilizoendelea katika hili ni sawa na kumlinganisha tembo na sisimizi.
 
Back
Top Bottom