David McAllister hajawahi kuipenda Serikali ya Tanzania "Ni vita ya uchumi"

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Jul 17, 2019
322
645
TUSIHOFU, HII NDO VITA YA KIUCHUMI

Na Elius Ndabila
0768239284


Jana kumezuka mtifuano mkali kwenye mitandao ya kijamii baada ya kile kilichoelezwa kuwa ni maazimio ya bunge la EU kwa Tanzania. Lakini baada ya ufafanuzi wa Balozi wa Tanzania juu ya wapotoshaji hali imetengamaa. Lakini pamoja na utengamano huo inaonyesha sura ya kesho ya Tanzania namna tunavyopaswa kujidhatiti kujitegemea.

Sitaki kuzungumzia sana hilo, lakini ninataka kumzungumzia David James McAllister aliyepata air time sana na vijana wa CHADEMA na ACT wakiongozwa na akina Maria Sarungi.

McAllister ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya nje ya Bunge la EU anatoka nchi ya Ujerumani. Huyu ni mwanachama wa Christian Democratic Union (CDU). Chama Cha CDU ni mwanachama wa vyama vya Kidemokrasia Duniani. Chama cha CDU ndicho cha rafiki na ambacho kimekuwa kikitoa msaada wa Fedha kwa Chama Cha CHADEMA nchini Tanzania. Hivyo walichokifanya CHADEMA ni kumtumia David James McAllister kuwashawishi wajumbe wa EU kuwa wao wanaonewa na Tanzania ipewe vikiwazo. Walimtumia huyu bwana kwa kuwa amekuwa mshirika wao wa muda mrefu kama ilivyo kwa CCM kwa chama cha Kikomunisti cha China.

Ukimsikiliza kwa umakini akichangia hoja hii Ndg McAllister amesema kuwa EU iangalie njia mpya ya kuisaidia Tanzania. Amesema wanaweza kupitishia misaada yao kwa watu ambao wanaona misaada yao itakuwa Salama. Lakini anasisitiza kuwa wao walikuwa wakifuatilia uchaguzi wa Tanzania wakishirikiana na CHADEMA.

McAllister hajawahi kuipenda serikali ya Tanzania, yeye siku zote amekuwa anaipenda CHADEMA ambacho ndicho chama masilahi kwake.

McAllister hawezi kuisifia Tanzania, hata iweje. Linapokuja suala la Tanzania kwake nyeusi ni nyeupe. Ataisifia Tanzania tu, pale mtakapoona CHADEMA inaisifia CCM, kinyume na hapo hakuna lolote. McAllister ndiyo silaha ya CHADEMA kwenye vikao vya EU.

Tafakari.
 
Vita na nchi masikini iliyoshindwa hata kujenga vyoo vya mashule uko seriously kweli.
Ishu sio kuipenda why ni Utawala huu pekee?

Utawala huu dhalimu ukiondoka kila kitu kitarejea kwenye mstari maana tutapata mtu ambae ni civilized educated and matured kuweza kuendesha gari.
 
Jamani huyu Eliasi Ndabila nilifikiri ni Elias Nawera yule aliyekuwa DAS,

Hata hivyo, nafikiri Kiongozi wenu ameshawaambia kwamba nyinyi ni Donor country, kwaiyo haina haja ya kulalamika, Hiyo vita unayoisema ni vita kati ya demokrasia na udikteta, haki za binadamu kuheshimiwa na kukataliwa, Uchaguzi huru au ubabe

Utawala wa kikundi au utawala unaotokana na wananchi,
Uhuru wa kuhoji au uhuru wa kusifia na kuabudu,

Kwaiyo nchi yetu haina vita yoyote ya kiuchumi,
Labda wangesema china kati ya Huawei na Iphone,

Kitu gani hicho mnachokifanya kinachotishia Marekani, Propaganda za Lumumba zinawafaa wana Lumumba,
 
Back
Top Bottom