David Kafulila: Miaka 25 ijayo Serikali itajenga Uchumi wa $700bn Tanzania itakuwa karibu marambili ya Africa ya Kusini

Mwananchi Huru

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
2,167
1,923
IMG-20250107-WA0086.jpg

===
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia nchi Tanzània PPPC Mhe David Kafulila amewaeleza Watanzania lazima wafahamu kesho ya Tanzània yao ni bora kama tu hali ya Umoja na mshikamamo iliyopo Sasa itaendelea kuwa ilivyo leo.

David Kafulila anasema, Tanzania kwa kushirikiana na sekta binafsi ( PPP) toka ndani au nje ya Tanzania wataipeleka kwa Kasi Tanzania kwenye Uchumi wa viwango vya juu kama ilivyoainishwa kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo kwa miaka 25 ijayo ( 2025-2050 )

Mtakumbuka, David Kafulila amekuwa ni Mtendaji na mwanasiasa anayejikita zaidi kwenye kutetea hoja za Serikali yake kwa namba|takwimu na "fact" zenye kueleweka na watu wa Kada zote kitu kinachomfanya awe ni Mtendaji wa Serikali anayefuatiliwa zaidi mitandaoni na. Wananchi kwa sasa.

Mkurugenzi Mtendaji huyu anasema Tanzània mpaka kufikia mwaka 2050 kwa kushirikiana na PPP inatarajia kujenga Uchumi mkubwa zaidi wa $700bn ambazo ni zaidi ya TZS 1,750 Trilioni ambao ni karibu mara mbili ya Uchumi wote wa Africa ya Kusini ya leo ambao unafikia i karibu $380bn.

Kafulila anasema si kazi rahisi kujenga Uchumi wa $700bn kutoka Uchumi wa sasa wa Tanzania wa $85bn kwani ni kazi ambayo kamwe haiwezi ikatekelezwa kwa Kodi na Mikopo pekee hivyo sekta binafsi haiepukiki kwenye safari hii ya ujenzi wa Uchumi mkubwa kwa kipindi kifupi cha miaka 25.

Mkurugenzi Mtendaji huyu anaendelea kwa kusema jambo hili linawezekana bila mashaka yoyote kwani hata nchi ya Vietnam mwaka 1990 ilikuwa na Uchumi wa $6.4bn lakini leo Vietnam wana Uchumi wa zaidi ya $460bn sawa na ukuaji wa karibu mara themanini (X 80) zaidi.

HITIMISHO, Kama hivyo ndivyo ilivyo kwanini Tanzania tusiweze wakati Vietnam wao wameweza kwani wao Wana nini?









====
 
Nakumbuka 2000 wakati wa Mkapa walitoa projection ya maendeleo ya Tanzania kwa miaka 25 ijayo(2025), hopes were very high, promises were made, Tanzania would be the new Switzerland, ona sasa kiko wapi...hadi leo matundu ya vyoo ni mtihani mkubwa kwa watawala, matundu ya vyoo, can you imagine!!
 
Taarifa inayosema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitajenga uchumi wa $700 bilioni ifikapo miaka 25 ijayo inaweza kuonekana kuwa na matumaini, lakini kuna sababu kadhaa za kuhoji ukweli wa tangazo hili.

Katika muktadha wa maendeleo ya kiuchumi, ni muhimu kutathmini vigezo mbalimbali vinavyoathiri ukuaji wa uchumi, ikiwa ni pamoja na mazingira ya kisiasa, sera za kiuchumi, na uwezo wa rasilimali.

1. Muktadha wa Uchumi wa Tanzania

Tanzania inakabiliwa na changamoto mbalimbali kiuchumi. Ingawa kuna maendeleo katika sekta kama kilimo na utalii, bado kuna matatizo makubwa kama umaskini, ukosefu wa ajira, na maendeleo duni ya miundombinu. Hali hii inaweza kuathiri uwezo wa nchi kufikia malengo makubwa kama hayo.

2. Mikakati ya Utekelezaji

CCM imeweka mikakati ya kuendeleza uchumi, lakini utekelezaji wa mikakati hii umekuwa na dosari. Kwa mfano, miradi mingi ya miundombinu inakabiliwa na ucheleweshaji na ukosefu wa fedha. Aidha, kuna mkataba wa PPP (Public-Private Partnership) ambao umeonekana kuwa na mafanikio machache, na hivyo kuathiri uwekezaji wa sekta binafsi.

3. Ushirikiano na Sekta Binafsi

Ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi ni muhimu katika kuleta maendeleo. Hata hivyo, sekta binafsi mara nyingi inakabiliwa na vikwazo kama vile ukosefu wa uwazi na urasimu katika mchakato wa kupata leseni na kibali. Hali hii inafanya wawekezaji wengi kukwepa kuwekeza nchini, hali inayoweza kuathiri malengo ya ukuaji wa uchumi.

4. Sera za Kiuchumi

Serikali ya CCM imeanzisha sera nyingi zinazokusudia kuimarisha uchumi. Hata hivyo, kuna maswali kuhusu ufanisi wa baadhi ya sera hizi. Kwa mfano, sera za kodi zimekuwa na athari hasi kwa biashara ndogo na za kati, na hivyo kuathiri uwezo wa mazingira ya biashara. Mabadiliko ya mara kwa mara katika sera za kiuchumi yanachangia pia kutokuwa na uhakika kwa wawekezaji.

5. Rasilimali na Uwekezaji

Uwekezaji katika rasilimali ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi. Ingawa Tanzania ina rasilimali nyingi kama madini na ardhi nzuri kwa kilimo, bado kuna changamoto katika usimamizi wa rasilimali hizi. Ufisadi na ukosefu wa uwazi katika usimamizi wa rasilimali umekuwa kikwazo kikubwa. Hii inahitaji serikali kuimarisha mifumo ya uwajibikaji ili kuvutia wawekezaji wa ndani na wa kigeni.

6. Elimu na Ujuzi

Kuimarisha elimu na ujuzi wa wananchi ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi. Hata hivyo, mfumo wa elimu nchini unakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa vifaa, walimu wenye ujuzi, na mtaala usioendana na mahitaji ya soko. Bila kuimarisha elimu, nchi itashindwa kuandaa vijana wenye uwezo wa kushiriki katika uchumi wa kisasa.

7. Sera za Ushirikiano wa Kimataifa

Tanzania inahitaji kushirikiana zaidi na nchi nyingine ili kuimarisha biashara na kuvutia wawekezaji. Ushirikiano huu unaweza kujumuisha makubaliano ya biashara na nchi nyingine, lakini pia ni muhimu kuimarisha mahusiano na mashirika ya kimataifa. Hata hivyo, ukosefu wa mipango ya muda mrefu na mkakati wa kueleweka katika ushirikiano wa kimataifa umeathiri uwezo wa nchi kufikia malengo yake.

8. Matarajio ya Baadaye

Ingawa matarajio ya uchumi wa $700 bilioni ni ya kuvutia, ni muhimu kukumbuka kuwa maendeleo ya uchumi yanahitaji muda, mipango thabiti, na ushirikiano wa kweli kati ya Serikali, sekta binafsi, na wananchi. Ni lazima kuwe na mkakati wa kueleweka na wa muda mrefu, ambao unazingatia mahitaji halisi ya nchi na wananchi wake.

Hitimisho

Kwa hiyo, ni muhimu kutathmini kwa makini taarifa inayosema kuwa CCM itajenga uchumi wa $700 bilioni. Ingawa kuna matumaini, ukweli ni kwamba changamoto nyingi zinahitaji kushughulikiwa ili kufikia malengo haya.

Ushirikiano wa dhati kati ya serikali, sekta binafsi, na wananchi utakuwa muhimu katika kufanikisha maendeleo endelevu ya uchumi wa Tanzania.
 
Taarifa inayosema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitajenga uchumi wa $700 bilioni ifikapo miaka 25 ijayo inaweza kuonekana kuwa na matumaini, lakini kuna sababu kadhaa za kuhoji ukweli wa tangazo hili.

Katika muktadha wa maendeleo ya kiuchumi, ni muhimu kutathmini vigezo mbalimbali vinavyoathiri ukuaji wa uchumi, ikiwa ni pamoja na mazingira ya kisiasa, sera za kiuchumi, na uwezo wa rasilimali.

1. Muktadha wa Uchumi wa Tanzania

Tanzania inakabiliwa na changamoto mbalimbali kiuchumi. Ingawa kuna maendeleo katika sekta kama kilimo na utalii, bado kuna matatizo makubwa kama umaskini, ukosefu wa ajira, na maendeleo duni ya miundombinu. Hali hii inaweza kuathiri uwezo wa nchi kufikia malengo makubwa kama hayo.

2. Mikakati ya Utekelezaji

CCM imeweka mikakati ya kuendeleza uchumi, lakini utekelezaji wa mikakati hii umekuwa na dosari. Kwa mfano, miradi mingi ya miundombinu inakabiliwa na ucheleweshaji na ukosefu wa fedha. Aidha, kuna mkataba wa PPP (Public-Private Partnership) ambao umeonekana kuwa na mafanikio machache, na hivyo kuathiri uwekezaji wa sekta binafsi.

3. Ushirikiano na Sekta Binafsi

Ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi ni muhimu katika kuleta maendeleo. Hata hivyo, sekta binafsi mara nyingi inakabiliwa na vikwazo kama vile ukosefu wa uwazi na urasimu katika mchakato wa kupata leseni na kibali. Hali hii inafanya wawekezaji wengi kukwepa kuwekeza nchini, hali inayoweza kuathiri malengo ya ukuaji wa uchumi.

4. Sera za Kiuchumi

Serikali ya CCM imeanzisha sera nyingi zinazokusudia kuimarisha uchumi. Hata hivyo, kuna maswali kuhusu ufanisi wa baadhi ya sera hizi. Kwa mfano, sera za kodi zimekuwa na athari hasi kwa biashara ndogo na za kati, na hivyo kuathiri uwezo wa mazingira ya biashara. Mabadiliko ya mara kwa mara katika sera za kiuchumi yanachangia pia kutokuwa na uhakika kwa wawekezaji.

5. Rasilimali na Uwekezaji

Uwekezaji katika rasilimali ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi. Ingawa Tanzania ina rasilimali nyingi kama madini na ardhi nzuri kwa kilimo, bado kuna changamoto katika usimamizi wa rasilimali hizi. Ufisadi na ukosefu wa uwazi katika usimamizi wa rasilimali umekuwa kikwazo kikubwa. Hii inahitaji serikali kuimarisha mifumo ya uwajibikaji ili kuvutia wawekezaji wa ndani na wa kigeni.

6. Elimu na Ujuzi

Kuimarisha elimu na ujuzi wa wananchi ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi. Hata hivyo, mfumo wa elimu nchini unakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa vifaa, walimu wenye ujuzi, na mtaala usioendana na mahitaji ya soko. Bila kuimarisha elimu, nchi itashindwa kuandaa vijana wenye uwezo wa kushiriki katika uchumi wa kisasa.

7. Sera za Ushirikiano wa Kimataifa

Tanzania inahitaji kushirikiana zaidi na nchi nyingine ili kuimarisha biashara na kuvutia wawekezaji. Ushirikiano huu unaweza kujumuisha makubaliano ya biashara na nchi nyingine, lakini pia ni muhimu kuimarisha mahusiano na mashirika ya kimataifa. Hata hivyo, ukosefu wa mipango ya muda mrefu na mkakati wa kueleweka katika ushirikiano wa kimataifa umeathiri uwezo wa nchi kufikia malengo yake.

8. Matarajio ya Baadaye

Ingawa matarajio ya uchumi wa $700 bilioni ni ya kuvutia, ni muhimu kukumbuka kuwa maendeleo ya uchumi yanahitaji muda, mipango thabiti, na ushirikiano wa kweli kati ya Serikali, sekta binafsi, na wananchi. Ni lazima kuwe na mkakati wa kueleweka na wa muda mrefu, ambao unazingatia mahitaji halisi ya nchi na wananchi wake.

Hitimisho

Kwa hiyo, ni muhimu kutathmini kwa makini taarifa inayosema kuwa CCM itajenga uchumi wa $700 bilioni. Ingawa kuna matumaini, ukweli ni kwamba changamoto nyingi zinahitaji kushughulikiwa ili kufikia malengo haya.

Ushirikiano wa dhati kati ya serikali, sekta binafsi, na wananchi utakuwa muhimu katika kufanikisha maendeleo endelevu ya uchumi wa Tanzania.
Analysis nzuri sana hii,
 
===
Mkurugenzi wa Ubia nchi Tanzània Mhe David Kafulila amewaeleza Watanzania lazima wajue ya kuwa kesho ya Tanzània yao ni bora kama hali itaendelea kuwa ilivyo leo.

Kafulila anasema Tanzania kwa kushirikiana na sekta binafsi PPPP ya ndani au nje ya Tanzania wanaipeleka Tanzania kwenye Uchumi wa viwango vya juu kama walivyoainisha kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo kwa miaka 25 ijayo,

David Kafulila amekuwa ni Mtendaji na mwanasiasa anayejikita kwenye kutetea hoja zake kwa namba na fact zenye kueleweka na watu wa Kada zote,


Msikilize vizuri mtaalamu huyu mpaka Mwisho
View attachment 3196797
Thubutuuuu ma stories tu upitishe muda wako ule upate cha juu kudalalia.....matajiri na mafisafi.....pato 20m mchezo ? Kwa unafikii huuuu? Miaka 100 milele aminaaa
 
Nakumbuka 2000 wakati wa Mkapa walitoa projection ya maendeleo ya Tanzania kwa miaka 25 ijayo(2025), hopes were very high, promises were made, Tanzania would be the new Switzerland, ona sasa kiko wapi...hadi leo matundu ya vyoo ni mtihani mkubwa kwa watawala, matundu ya vyoo, can you imagine!!
Kila kitu kinakwenda hatua kwa hatua mkuu,

Tanzania ya mwaka 2000 sio hii ya leo
 
===
Mkurugenzi wa Ubia nchi Tanzània Mhe David Kafulila amewaeleza Watanzania lazima wajue ya kuwa kesho ya Tanzània yao ni bora kama hali itaendelea kuwa ilivyo leo.

Kafulila anasema Tanzania kwa kushirikiana na sekta binafsi PPPP ya ndani au nje ya Tanzania wanaipeleka Tanzania kwenye Uchumi wa viwango vya juu kama walivyoainisha kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo kwa miaka 25 ijayo,

David Kafulila amekuwa ni Mtendaji na mwanasiasa anayejikita kwenye kutetea hoja zake kwa namba na fact zenye kueleweka na watu wa Kada zote,


Msikilize vizuri mtaalamu huyu mpaka Mwisho
View attachment 3196797
Anatupanga tuu anajua hatakuwepo.
 
===
Mkurugenzi wa Ubia nchi Tanzània Mhe David Kafulila amewaeleza Watanzania lazima wajue ya kuwa kesho ya Tanzània yao ni bora kama hali itaendelea kuwa ilivyo leo.

Kafulila anasema Tanzania kwa kushirikiana na sekta binafsi PPPP ya ndani au nje ya Tanzania wanaipeleka Tanzania kwenye Uchumi wa viwango vya juu kama walivyoainisha kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo kwa miaka 25 ijayo,

David Kafulila amekuwa ni Mtendaji na mwanasiasa anayejikita kwenye kutetea hoja zake kwa namba na fact zenye kueleweka na watu wa Kada zote,


Msikilize vizuri mtaalamu huyu mpaka Mwisho
View attachment 3196797
Siku hizi haongelei Adani Group tena,
RIP Jaji Werema ulikuwa sahihi.
 
===
Mkurugenzi wa Ubia nchi Tanzània Mhe David Kafulila amewaeleza Watanzania lazima wajue ya kuwa kesho ya Tanzània yao ni bora kama hali itaendelea kuwa ilivyo leo.

Kafulila anasema Tanzania kwa kushirikiana na sekta binafsi PPPP ya ndani au nje ya Tanzania wanaipeleka Tanzania kwenye Uchumi wa viwango vya juu kama walivyoainisha kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo kwa miaka 25 ijayo,

David Kafulila amekuwa ni Mtendaji na mwanasiasa anayejikita kwenye kutetea hoja zake kwa namba na fact zenye kueleweka na watu wa Kada zote,


Msikilize vizuri mtaalamu huyu mpaka Mwisho
View attachment 3196797
Wakati huo itakuwa 20m haitoshi hata kununua Toyo.
 
Back
Top Bottom