DARUSO wamshukia kama mwewe Mhadhiri wao baada ya kusema wanafunzi UDSM hawajui kuoga ni wachafu

Doncy monco

Member
Jul 26, 2019
38
101
Uongozi wa Serikali ya wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO), wamejibu tuhuma zilizotolewa na Mhadhiri wa chuo hicho Kitivo cha Sanaa ya ubunifu Dkt. Vicensia Shule, kuhusu uwepo wa baadhi ya wanafunzi wachafu na hawajui kuoga.

Rais wa DARUSO Hamis Musa, amesema kuwa kauli hiyo imewapa doa na kuwashushia hadhi wanafunzi kwa sababu kitendo cha kumwambia mwanafunzi wa chuo ananuka ni cha fedheha lakini licha ya uwepo mijadala mbalimbali baada ya kauli hiyo kutolewa lakini wanafunzi walielewa kwa sababu wao si wachafu.

''Ni kweli hiyo kauli Dkt Shule aliitoa, sijajua aliitoa kwa mlengo gani, lakini sisi kama Serikali ya wanafunzi hatujaipokea kwa mlengo mzuri kwa sababu inalengo la kutushushia hadhi sisi wanafunzi, unapomuambia mwanafunzi wa chuo haogi sidhani kama ni kitu kizuri'' amesema Rais wa DARUSO.

Aidha Rais huyo wa DARUSO akizungumzia suala la malezi katika familia, ametoa rai kwa wazazi kuwafundisha watoto masuala ya usafi ili wakikua waweze kujitegemea wenyewe na si kuwaachia wafanyakazi wa ndani kuwafanyia kila kitu.


Kujua zaidi jinsi Dr.Shule alivyowaponda wanafunzi kwamba wananuka, soma
 
Uongozi wa Serikali ya wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO), wamejibu tuhuma zilizotolewa na Mhadhiri wa chuo hicho Kitivo cha Sanaa ya ubunifu Dkt. Vicensia Shule, kuhusu uwepo wa baadhi ya wanafunzi wachafu na hawajui kuoga.
Rais wa DARUSO Hamis Musa, amesema kuwa kauli hiyo imewapa doa na kuwashushia hadhi wanafunzi kwa sababu kitendo cha kumwambia mwanafunzi wa chuo ananuka ni cha fedheha lakini licha ya uwepo mijadala mbalimbali baada ya kauli hiyo kutolewa lakini wanafunzi walielewa kwa sababu wao si wachafu.
''Ni kweli hiyo kauli Dkt Shule aliitoa, sijajua aliitoa kwa mlengo gani, lakini sisi kama Serikali ya wanafunzi hatujaipokea kwa mlengo mzuri kwa sababu inalengo la kutushushia hadhi sisi wanafunzi, unapomuambia mwanafunzi wa chuo haogi sidhani kama ni kitu kizuri'' amesema Rais wa DARUSO.
Aidha Rais huyo wa DARUSO akizungumzia suala la malezi katika familia, ametoa rai kwa wazazi kuwafundisha watoto masuala ya usafi ili wakikua waweze kujitegemea wenyewe na si kuwaachia wafanyakazi wa ndani kuwafanyia kila kitu.
Kujua zaidi jinsi Dr.Shule alivyowaponda wanafunzi kwamba wananuka, soma
Ajiangalie asije akadisco maana hawa wahadhiri wakiwa chuoni ukiwasumbua/ukibishana nao ujue hatima yako kitaaluma inakaribia
 
ukiona wanafunzi wanahangaika na mambo madogomadogo jua UE inakaribia
 
Back
Top Bottom