Shayu
Platinum Member
- May 24, 2011
- 608
- 1,653
Elimu yetu ya sasa ni kama chupa tatu kubwa; Moja ya nusu lita, nyingine ya lita moja na nyingine ya lita mbili. Zote hizi baada ya kujazwa maji kiwandani zilifungwa vizibo.
Chupa hizi ni maarifa tunayowapa watoto wetu kuanzia shule ya msingi, sekondari na chuo kikuu. Ili tuendelee kama taifa ni lazima tufungue vizibo hivi.
Ni lazima elimu yetu ielekezwe kukuza ufikiri watoto wetu na sio kumwingizia maarifa kama maji yanavyojazwa kwenye chupa na kufungwa. Ni lazima ielekezwe kwenye kukuza ufahamu wao.
Kwa njia hii pekee watu wetu watakuwa wabunifu na wagunduzi. Ni muhimu kutokutengeneza watu wa kulishwa maarifa bali watu wanaofikiri.
Hatuwezi kuendelea katika misingi ya elimu ya namna hii. Kuendelea kwa binadamu ni kukua kwa akili zake. Watu wanaofikiri ndio wanaounda mifumo na kugundua na kutengeneza dunia tunayoona kwa sasa.
Fikiri Fikiri Fikiri, tumia ubongo wako mwenyewe... Usikubali mtu afikiri kwa niaba yako... Shule zilijengwa na watu wanaofikiri wakawa wana wafuasi waliyatafuta maarifa kwa nguvu na jasho na nidhamu ya hali ya juu.
"Dare to use your own mind" Be a master and not a disciple.
Elimu yetu lazima ifundishe watu wetu watumie akili yao wenyewe....And that is true freedom.
Ni muhimu kufahamu hata mbwa anaweza kufundishwa lakini binadamu ni lazima afikiri na aendelee kukua katika fikra. Ni kwa kukuza fikra za watu wetu tu ndipo watu wetu watakuwa wenye maarifa na wazalishaji.
Kwa njia hii pekee tutajenga jamii yenye busara na maarifa.
Popote ulipo tumia uwezo wako wa kufikiri kuna nguvu katika uwezo wa kufikiri, kumtegemea mtu mwingine kwa fikra ni utumwa ambao hautatufanya tupige hatua kama mtu na kama taifa. Tutajitegemea kama taifa tutakapo jitegemea kifikra.
Shaabany@yahoo.com: Note from the book ''KIU YA UZALENDO''
Chupa hizi ni maarifa tunayowapa watoto wetu kuanzia shule ya msingi, sekondari na chuo kikuu. Ili tuendelee kama taifa ni lazima tufungue vizibo hivi.
Ni lazima elimu yetu ielekezwe kukuza ufikiri watoto wetu na sio kumwingizia maarifa kama maji yanavyojazwa kwenye chupa na kufungwa. Ni lazima ielekezwe kwenye kukuza ufahamu wao.
Kwa njia hii pekee watu wetu watakuwa wabunifu na wagunduzi. Ni muhimu kutokutengeneza watu wa kulishwa maarifa bali watu wanaofikiri.
Hatuwezi kuendelea katika misingi ya elimu ya namna hii. Kuendelea kwa binadamu ni kukua kwa akili zake. Watu wanaofikiri ndio wanaounda mifumo na kugundua na kutengeneza dunia tunayoona kwa sasa.
Fikiri Fikiri Fikiri, tumia ubongo wako mwenyewe... Usikubali mtu afikiri kwa niaba yako... Shule zilijengwa na watu wanaofikiri wakawa wana wafuasi waliyatafuta maarifa kwa nguvu na jasho na nidhamu ya hali ya juu.
"Dare to use your own mind" Be a master and not a disciple.
Elimu yetu lazima ifundishe watu wetu watumie akili yao wenyewe....And that is true freedom.
Ni muhimu kufahamu hata mbwa anaweza kufundishwa lakini binadamu ni lazima afikiri na aendelee kukua katika fikra. Ni kwa kukuza fikra za watu wetu tu ndipo watu wetu watakuwa wenye maarifa na wazalishaji.
Kwa njia hii pekee tutajenga jamii yenye busara na maarifa.
Popote ulipo tumia uwezo wako wa kufikiri kuna nguvu katika uwezo wa kufikiri, kumtegemea mtu mwingine kwa fikra ni utumwa ambao hautatufanya tupige hatua kama mtu na kama taifa. Tutajitegemea kama taifa tutakapo jitegemea kifikra.
Shaabany@yahoo.com: Note from the book ''KIU YA UZALENDO''