screpa
JF-Expert Member
- Sep 10, 2015
- 10,792
- 15,693
Salaam wandugu, nimeona humu jukwaani watu wengi wamekuwa wakisema wimbo wa Darasa 'Muziki' umewafunga midomo Wasafi na kusababisha nyimbo zao kubuma mfano 'Kokoro', kwa mtazamo wangu mimi huo wimbo wa 'Kokoro' ni wa kawaida tu na hata isingekuwa wimbo wa Darasa usingekuwa hit kubwa, ni kama wimbo wa Dimpoz 'Kajiandae' nao ni wimbo wa kawaida sana na ningeshangaa kama ungehit. Wimbo pekee ambao naona umeathiriwa sana na kuvuma kwa Darasa ni 'Dume Suruali' wa MwanaFA. Huu wimbo kwa content ya mashairi na hali halisi ya kiuchumi nchini ulistahili sana kuwa HIT, ni vile tu imekuwa bahati mbaya kutoka pamoja na MUZIKI 'Homa ya Jiji', pole sana MwanaFA jitahidi sikunyingine ufanye timing nzuri