Darassa afunguka kuhusu kumponda diamond kwenye wimbo wake...sio simba sio chui sio mamba

Nucky Thompson

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
1,817
4,058
Msanii Darassa amefunguka kuhusu kumponda diamond kwenye wimbo wake ambapo kuna mashairi yanayosema 'sio simba sio chui sio mamba' na kudai mashairi hayo hayamuhusu Diamond ila watu wameelewa vibaya
Pia ameongezea diamond hakustahili kujiita simba kwa kuwa simba anaweza kuuwawa na wanakijiji lakini yeye hawezi kuuwawa kirahisi kama simba

Wanyama wa simba chui na mamba ndio wanyama wakali wanaoogopwa lakini yeye amesema ana kitu kingine kikubwa cha kuogopwa kuliko wanyama hao
 
Mbona alichokisema Darasa sicho hicho ulicho andika ?
Mna kazi na hizi team zenu
 
umbeatz_-20170104-0001.jpg
 
Naomba umuulize kuhusu tetesi kwamba nae anatumia yale madudu ya Chid Benz.Kama ndivyo mwambie aache mara moja..
 
hawa kwani wanafanya mziki unaofanana.....?
kuna ushindani baina yao....?
 
Mimi nadhani music lazima umguse mtu mmoja au mwingine kwa namna moja au nyingine iwe kwakuelemisha au kuburudisha , hiyo ndio dhamira ya music aina zote duniani, hata music wa diamon (salome) utakuwa unamgusa mtu fulani kwa namna yoyote, hivyo basi wimbo wa Darassa kama unamgusa diamond kwa namna moja au nyingine binafsi sioni ajabu kwani diamond ni nani hadi asiguswe na waimbaji wenzake katika mashairi yao…?
 
Ujinga nikujiita majina meeeengi..ya kisanii..alafu nyimbo zenyewe mahudhui ni mapenzi na sarakasi kwenye video. .. mbona J.mo ..yaani Juma Mchopanga..tunamuelewa... Bernad Paul ..anajiita Ben poul..na tunamuelewa ...ila unakuta wasanii wanagombania majina ... Hizo ndo tunaziita brabraa. Mbona Saida Karori hana a.k.a. ..alafu nyie kizazi kipya ndo kwanza mnagombea melody za na vocal zake..acha maswara nyie wasanii sisi tunachotaka ni Muziki ... Au mmeota mapembe??? ...eti. Kajiandae..hahaa..eti ... Kokoro... Ndo Nini???!! Mapenzi kila nyimbo ...tumechoka ..ebu nyie wekeni Muziki ...Maisha na Muziki ambao hauna maneno ya kwenye kanga..Safari na Muziki...acheni maneno weka Muziki..
 
  • Thanks
Reactions: SIM

Similar Discussions

Back
Top Bottom