Darasa la saba Dar kufanya mitihani 16 Jan 2020, Necta watoa ufafanuzi

Wanafunzi wa darasa la saba wote tz nzima hawakufunga almost mwezi wa kumi na mbili wote walikuwa wakisoma wakijiandaa kwa mitihani ya taifa kwa kuwa mwaka huu watawahi kufanya kwaajili ya uchaguzi mkuu, sidhani kama watakosa cha kujibu.
Wanagunzi wamefungua shule tarehe 6 january, kesho ni tarehe 16
Hivi ndani ya huo muda, walimu na wanafunzi wanaweza kuwa wamesoma kiasi cha kucover mada zote za darasa la saba?
 
Mkuu kwa mujibu wa serikali mwaka wa masomo unaanza january, hata wakaguzi wanapowakagua walimu huangalia walimu wamefundisha kutoka january katika mwaka husika

Hilo la kufundisha likizo ni kwa baadhi ya shule na halikuwa agizo kutoka serikalini
Huu mtihani walimu na wanafunzi hawajajiandaa, Necta hawatatoa matokeo ya mtuhani huu licha ya kuutangaza
Wanafunzi wa darasa la saba wote tz nzima hawakufunga almost mwezi wa kumi na mbili wote walikuwa wakisoma wakijiandaa kwa mitihani ya taifa kwa kuwa mwaka huu watawahi kufanya kwaajili ya uchaguzi mkuu, sidhani kama watakosa cha kujibu.
 
Ninapokujibu hivyo hiyo yote naifahamu
Semina ilitolewa siku ya jumamos, zaidi walitoa maagizo na kuonya juu ya wizi wa mitihani unaofanywa na shule za hapa jijini pia waliwaagiza walimu wakajipange kwa kujiandaa na mtihani huo
Ajabu ni kesho mtihani utafanyika, je hayo maandalizi yatafanyika lini?
Wanafahamu kwa nini wanafanya hivyo, tujifunze kwa team inapocheza uwanjani, tulio nje (watazamaji) huwa tunakuwa wakufunzi great kuliko wataalam.
 
Wanafunzi wamefungua shule tarehe 6 january, kesho ni tarehe 16
Hivi ndani ya huo muda, walimu na wanafunzi wanaweza kuwa wamesoma kiasi cha kucover mada zote za darasa la saba?
Inawezekana kiongozi mtihani itatungwa mfumo Wa necta ila topics zitaishia za darasa LA sita .wataacha topics za darasa LA saba
 
Wanafunzi wamefungua shule tarehe 6 january, kesho ni tarehe 16
Hivi ndani ya huo muda, walimu na wanafunzi wanaweza kuwa wamesoma kiasi cha kucover mada zote za darasa la saba?
Darasa la saba kwa asilimia 95 halina mada mpya, masomo ya msingi yanaishia darasa la sita, darasa la saba ni "revision" tu (waste of time and resources).
 
Dada hawa ni mtaala wa zamani,usichanganye madesa

Sent using Jamii Forums mobile app
"Mtaala" wa zamani ndiyo darasa la saba kuna topics mpya ambazo hujafundishwa kuanzia la kwanza mpaka la sita?

Tanzania kwa vijana kama wewe tuna safari ndefu sana ya kwenda, sikushangai, nafahamu ni shule zetu, Mwalim aliyekusomesha utakuta ni failure tu, tutegemee nini?
 
Wanafunzi wamefungua shule tarehe 6 january, kesho ni tarehe 16
Hivi ndani ya huo muda, walimu na wanafunzi wanaweza kuwa wamesoma kiasi cha kucover mada zote za darasa la saba?
Kwani mtihani wa darasa la saba unahusisha mafundisho yaliyofanyika mwaka wa saba tu?
 
Darasa la saba kwa asilimia 95 halina mada mpya, masomo ya msingi yanaishia darasa la sita, darasa la saba ni "revision" tu (waste of time and resources).
Kama hujui kitu kuhusu elimu ya shule za msingi ni vema ukapiga kimya
 
Mtihani huo unafanyika leo 16/01/2020 na utahusisha Wanafunzi wa Darasa la saba katika shule za Umma na binafsi katika Mkoa wa Dar es Salaam pekee. Ni Mtihani wa ndani kwa ajili ya kuwapima Walimu baaba ya kufundishwa mbinu mpya za utungaji wa Mitihani.
===

1579156372761.png
Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetoa ufafanuzi kuhusu mitihani itakayofanyika kesho Alhamisi Januari 16, 2020 jijini Dar es Salaam kwa wanafunzi wa darasa la saba.

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetoa ufafanuzi kuhusu mitihani itakayofanyika kesho Alhamisi Januari 16, 2020 jijini Dar es Salaam kwa wanafunzi wa darasa la saba.

Mtihani huo utahusisha shule zote za umma na binafsi na utafanyika kwa siku moja ya kesho.

Limesema mitihani hiyo ni mazoezi ya ndani ya wanafunzi katika shule za Mkoa huo.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Januari 15, 2020 katibu mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde amesema kinachofanyika kesho si mitihani ya Necta, ni jaribio kwa walimu wa Mkoa huo baada ya kupewa mafunzo ya namna bora ya kutunga mitihani.

“Hawana mtihani kama watu wanavyotaka kupotosha, usahihi ni kwamba watakuwa na mazoezi ya ndani ya shule zao ambayo yatasimamiwa na Necta.”

“Tuliwapa walimu mafunzo ya namna bora ya kuwapa mitihani na mazoezi wanapokuwa shuleni kuhakikisha ufaulu unakuwa vizuri zaidi na wanafunzi wanaizoea mitihani ya Taifa na kuwa tayari watakapokutana nayo,” amesema Msonde.

Amesema lengo la mazoezi hayo ni kuhakikisha walimu wa shule zote za msingi wanakuwa na umahiri wa kutunga mtihani.

“Tunaamini shule zikiimarika Taifa linaimarika, tunataka ubora wa maswali uongezeke ili wanapofika kwenye mtihani wa mwisho wawe wamebobea. Tunataka tuone kama kuna chochote wamekipata kwenye mafunzo yetu na kama kuna shida tuone ni namna gani tunaweza kuweka sawa,” amesisitiza Msonde

MWANANCHI
 
Kwa uelewa wangu mdogo mkoa ambao umefanya vibaya zaidi ndio hii semina ilitakiwa ipelekwe.

Halafu utungaji mitihani sidhani kama una uhusiano na kufaulu, shida kubwa niionayo mimi ni wanafunzi kutomaliza mitaala na upungufu wa walimu ndio unaofanya matokeo kuwa mabaya.

Unforgetable
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom