MR.NOMA
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 338
- 502
Wananzengo kwa wale waliopita MKWAWA sekondari,hasa waliokuwa darasa la mwisho,tukumbushane interesting stories za kunzia tukiwa pale 2003-2005 ambapo sekondari ilifutwa rasmi.Baadhi ninayoyakumbuka mimi ni:-Uwepo wa kijiwe kiitwacho love square ambacho kilikuwa maalumu kwa ajili ya kutongozeane, Kuvuma kwa jina maarufu la chapati dadaz wale mabinti waliokuwa wanaenda kujiuza usiku twn na wakirudi alfajiri wamebeba chapati tu, Kupigwa kwa disco kubwa multipurpose siku tukiagana na form 5 waliokuwa wakuhamishwa shule lakini disco lilizimwa ghafla saa 6 usiku baada ya mwalimu wa nidhamu Mr makwaya kubaini watu wakibambiana, Kuwepo kwa mdada maarufu aliyekuwa akiwauza wasichana warembo kwa ma pedeshee na ye kula cha juu,kuwepo kwa kundi la mapaster watoa mapepo ambao waliwatoa sana wanafunzi wa kike na mradi wao uliharibika pale walipoenda usiku kuiombea nyumba ya headmaster kwa madai kuwa ina mapepo.Nadhani hawatasahau asubuhi walichezea bakora tukiwa pared, pia kuibuka kwa kikundi cha vijana wachache wenye msimamo mkali wa dini ya kiislamu ambao waliwacharaza bakora wakristo kadhaa kwa kosa la kuwasalimia kwa kuwashika mikono mabinti waislam, Kuwepo kwa mwalimu mwenye vituko aliyependa sifa na alivaa suti kila Mara huyu aliitwa Tozi na alimuuliza maswali magumu Waziri wa Elimu alipokuja kutangaza kuhamisha fomu five wote na fomu six tukimaliza shule iwe CHUO,...............haya wanakoplex njoeni muongezee