DAR: Wasanii wote waliokuwa wameondolewa kwenye Fiesta warejeshwa; kuisha saa 11 alfajiri

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279


Waandaaji wa tamasha la kila mwaka la Fiesta, Clouds Media Group wamelazimika kuwarudisha wasanii wote waliotolewa kwenye 'list' ya watakaotumbuiza baada ya muda kuonekana kuwa kikwazo.

Kurudishwa huko kumetokana na muda wa kumalizika kwa tamasha hilo kusogezwa hadi saa 11 alfajiri kwa kibali maalumu kutoka Serikalini.

Fiesta imekuwa ikifanyika kila mwaka na kuisha 'majogoo' lakini siku chache zilizopita Uongozi wa mkoa ulitoa kauli kuwa tamasha lolote linalofanyika baada ya saa 6 usiku linalazimika kufanyika kwenye klabu na si eneo la wazi.
 
Ndo nasikia kwenye jahazi asaivi bora maana kuna baadhi walishavurugwa
 
Duu kuna mpambano mkali watoto wa baba mmoja wanaoneana wivu kwamba mmoja anapendwa zaidi Ruge na Bashite watoto wa mzee
 
Wasanii woote waliokuwa wameondolewa kwenye orodha ya 'kuperfom' kesho FIESTA 2017 Leaders Club Dar E Salaam kutokana na taarifa za awali kuonesha kuwa uongozi wa Mkoa uliagiza tamasha kuisha saa saba usiku wamerudishwa kwenye orodha.

Hii inamaanisha kuna kukesha? Nani kashinda sasa? Mkuu wa mkoa au Clouds

Swali moja kwa wadau, hivi kuna kitu gani alichowahi kufanya Makonda kwa hila kikafanikiwa?
 
Hayo mambo waachie wao inasemekana ni watoto wa baba mmoja wote... Wanapendwa japo mmoja ni mtoto wa kambo
 
Watoto wa baba mmoja...Mmoja ana wivu sana mwingine kapoa ila kifasihi yuko vizur sana...

btw! Bora wamerudishwa kwasabab. walokua wanaumia hapo ni wasanii na sio clouds kivile!!
 
Kutokana na kukurupuka kwa Bashite kukataza Tigo Fiesta isiendelee hadi asubuhi hali iliyosababisha baadhi ya wasanii kuondolewa kwenye orodha ya kuimba. Hatimae asubuhi ya leo waziri mwenye zamana ya Starehe Mh. Mwakyembe alifika kwenye ofisi za Clouds Media Group na kuyaweka sawa na kusikia kilio cha wasanii. Ndipo amri ya BASHITE ilipobatirishwa na kufanya sasa TIGO FIESTA KWENDA HADI ASUBUHI.
 
Back
Top Bottom