Dar: Wafanyabiashara rasmi 45,000 wafunga Biashara na kuhamia kwenye umachinga

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge amesema kwa miaka mitano au sita iliyopita kumekuwa na wimbi la wafanyabiashara wengi ambao wanafunga biashara rasmi na kuhamia umachinga.

“Kinondoni huwa tunapokea taarifa ya biashara zinazofungwa ambapo kila mwezi ni biashara 150 zinafungwa na hii ni kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita.

“Kwa hesabu za Kinondoni, zaidi ya wafanyabiashara rasmi 9,000 wamekuja kutoa tamko la kufunga biashara ili wasitambulike kwenye mfumo.

“Wanapofunga biashara wanapeleka tamko Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Lakini tumebaini wafanyabiasharta hawa wanakwenda kuwa wamachinga.

“Nimeuliza mameya wenzangu hali ni hiyohiyo. Tulikuwa tunachukua takwimu za mkoa mzima na kubaini mpaka sasa ni zaidi ya wafanyabiashara 45,000 waliokuwa kwenye mfumo rasmi wamebadilika na kuwa wamachinga,” amesema.

Aidha, aliwaonya viongozi wenzake ambao wanadaiwa kuingia kwenye biashara ya kuleta wamachinga kutoka mikoani na kuwaleta jijini Dar es Salaam.
 
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge amesema kwa miaka mitano au sita iliyopita kumekuwa na wimbi la wafanyabiashara wengi ambao wanafunga biashara rasmi na kuhamia umachinga.

“Kinondoni huwa tunapokea taarifa ya biashara zinazofungwa ambapo kila mwezi ni biashara 150 zinafungwa na hii ni kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita.

“Kwa hesabu za Kinondoni, zaidi ya wafanyabiashara rasmi 9,000 wamekuja kutoa tamko la kufunga biashara ili wasitambulike kwenye mfumo.

“Wanapofunga biashara wanapeleka tamko Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Lakini tumebaini wafanyabiasharta hawa wanakwenda kuwa wamachinga.

“Nimeuliza mameya wenzangu hali ni hiyohiyo. Tulikuwa tunachukua takwimu za mkoa mzima na kubaini mpaka sasa ni zaidi ya wafanyabiashara 45,000 waliokuwa kwenye mfumo rasmi wamebadilika na kuwa wamachinga,” amesema.

Aidha, aliwaonya viongozi wenzake ambao wanadaiwa kuingia kwenye biashara ya kuleta wamachinga kutoka mikoani na kuwaleta jijini Dar es Salaam.
Umachinga ni Tax evasion.
 
Karibuni ila mkae mkijua umachinga ni lifestyle sio tu sehemu unapouzia vitu😁
 
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge amesema kwa miaka mitano au sita iliyopita kumekuwa na wimbi la wafanyabiashara wengi ambao wanafunga biashara rasmi na kuhamia umachinga.

“Kinondoni huwa tunapokea taarifa ya biashara zinazofungwa ambapo kila mwezi ni biashara 150 zinafungwa na hii ni kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita.

“Kwa hesabu za Kinondoni, zaidi ya wafanyabiashara rasmi 9,000 wamekuja kutoa tamko la kufunga biashara ili wasitambulike kwenye mfumo.

“Wanapofunga biashara wanapeleka tamko Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Lakini tumebaini wafanyabiasharta hawa wanakwenda kuwa wamachinga.

“Nimeuliza mameya wenzangu hali ni hiyohiyo. Tulikuwa tunachukua takwimu za mkoa mzima na kubaini mpaka sasa ni zaidi ya wafanyabiashara 45,000 waliokuwa kwenye mfumo rasmi wamebadilika na kuwa wamachinga,” amesema.

Aidha, aliwaonya viongozi wenzake ambao wanadaiwa kuingia kwenye biashara ya kuleta wamachinga kutoka mikoani na kuwaleta jijini Dar es Salaam.
Sasa Mh.Meya anasikitika ama anatutaarifu tu sisi wa kijiji tujue yanayojiri mijini?
 
Kuna haja ya kuwapanga wamachinga kama Raisi alivyosema. Kila jambo lazima liwe na utaratibu pasipokuwa na utaratibu linageuka vurugu.

Ukweli wafanyabiashara hawaachi kufanya biashara. Wanachofanya wanawageuza wamachinga kuwa madalali wa biashara zao jioni wanaleta hesabu.

Kuwe na mitaa maalumu ya kufanyia biashara za umachinga. Isiwe ni biashara ya kila eneo. Kutengwe baadhi ya siku. Mfanano hata kama ni kariakoo biashara zao zianze saa 12 jioni mpaka saa 5 au 6 usiku wakati wafanyabiashara wa maduka wanapokuwa wanafunga/wamefunga biashara zao.

Njia nyingine ni kutenga mitaa maalumu katika siku maalumu za wiki. Hii inaweza chaguliwa mitaa isiyoingiliana na bidhaa wanazouza machinga. Mfano mitaa inayouza spare za magari.

Lazima tuione nia nzuri ya serikali ya awamu ya sita. Hata kama ni machinga anahitaji watoto waende shule, anahitaji matibabu ya gharama nafuu, anahitaji maji umeme barabara. Tukiendelea na hali iliyoko sasa tunakotaka kufika hatutafika.

Tusilichukulie hili jambo kisiasa wala kimzaha. Ni suala nyeti kwa mustakabali wa nchi yetu
 
Matching Guy hana Mgundi,Manzese yake Magomeni yake na Mbagala pia yake.
 
Back
Top Bottom