Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,558
- 21,494
Dar es Salaam. Wabunge wa CHADEMA, wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, wameshawasili katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo asubuhi saa 2.
Wabunge hao wanafika mahakamani kama walivyoamriwa na mahakama kutokana na mashtaka yanayowakabili, ikiwano ya kuhamasisha maandamano na uchochezi.
Miongoni mwa waliofika mahakamani ni pamoja na Katibu Mkuu wa chama hicho, Vincent Mashinji, Esther Bulaya wa Bunda, Halima Mdee (Kawe), Esther Matiko(Tarime Mjini), Naibu Katibu Mkuu bara, John Mnyika na Naibu Katibu Mkuu visiwani, Salum Mwalimu .
Wamefika mahakamai hapo kutokana na kesi inayowakabili namba 112 ya mwaka huu
Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri ataongoza kesi hiyo huku Wakili wa Serikali Mkuu Faraja Nchimbi akijibu hoja zilizowasilishwa jana na Wakili wa utetezi Peter Kibatala.
Chanzo: Mwananchi
Soma: Mbowe na viongozi 6 wa CHADEMA wafikishwa Mahakamani Kisutu, wasomewa mashitaka 8, wanyimwa dhamana hadi Machi 29
Soma: KISUTU, DAR: Mahakama yawapa dhamana Viongozi 6 wa CHADEMA bila kuwepo mahakamani. Kutoka gerezani Aprili 3, 2018...
Soma: Mbowe na wenzake waomba shauri lao kuhamia Mahakama Kuu. Mh. Ester Bulaya ameunganishwa katika kesi yao