Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Mkutano wa amani ulioandaliwa na Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini chini ya Sheikh wa mkoa Alhad Mussa Salim kama Mwenyekiti wa Kamati, umefanyika leo jijini Dar es salaam.
Mkutano huo umejadiliwa amani ya nchi sambamba na kuombea Taifa amani, pia ilikuwa fursa ya kukutana na Viongozi wa dini mbalimbali na kujenga mahusiano mema ya kibinadamu.
Akizungumza katika mkutano huo, mgeni rasmi, Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi amewataka Viongozi wa dini nchini kuanzisha kamati ya amani kila mkoa na ngazi ya Taifa ili kuwafundisha watu wote umuhimu wa amani kwa ajili ya kufikia maendeleo ya Taifa.
Mzee Alhaj Ali Hassan Mwinyi alisema amani ndiyo kichocheo cha maendeleo, ikizingatiwa kazi kubwa inayofanywa na Rais Dkt. John Magufuli ya kuipeleka Tanzania katika uchumi wa viwanda.
Mkutano huo umejadiliwa amani ya nchi sambamba na kuombea Taifa amani, pia ilikuwa fursa ya kukutana na Viongozi wa dini mbalimbali na kujenga mahusiano mema ya kibinadamu.
Akizungumza katika mkutano huo, mgeni rasmi, Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi amewataka Viongozi wa dini nchini kuanzisha kamati ya amani kila mkoa na ngazi ya Taifa ili kuwafundisha watu wote umuhimu wa amani kwa ajili ya kufikia maendeleo ya Taifa.
Mzee Alhaj Ali Hassan Mwinyi alisema amani ndiyo kichocheo cha maendeleo, ikizingatiwa kazi kubwa inayofanywa na Rais Dkt. John Magufuli ya kuipeleka Tanzania katika uchumi wa viwanda.