Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Rais Magufuli anaongoza Mkutano huo unaoendela katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar. Mkutano huo umehudhuriwa na wadau mbalimbali wa Sekta hiyo wakiongozwa na Waziri wa Ujenzi, Isack Kamwelwe
==============
Rais wa Tanzania, John Magufuli ametaja baadhi ya sababu zinazofanya wakandarasi wa ndani kushindwa kupewa miradi mikubwa ili kuitekeleza.
Miongoni mwa sababu hizo ni kukosa umoja na ushirikiano kati yao, kuendeleza vitendo vya rushwa, wakandarasi kuwa wazito kuomba zabuni ya kutekeleza miradi mikubwa inayotangazwa nchini na wengine wamekuwa wakishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali kuomba zabuni.
Magufuli amebainisha hayo leo Jumatano ya Septemba 4, 2019 katika mkutano uliowakutanisha watumishi wa bodi tatu zilizo chini ya wizara hiyo ikiwemo, Bodi ya usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) jijini Dar es Salaam.
Amesema mwaka jana nakumbuka tulitangaza mradi wa barabara ya kutoka Chamwino kwenda mjini Dodoma na nilitegemea kabisa kilomita 20 zitaombwa na kampuni za wazalendo wala hawakuomba. “Kuna miradi mingine midogo tu ya kuongeza mita 500 kama ile ya uwanja wa Dodoma, wazalendo hawakuomba, ninaweza nikataja miradi mingi na hapa unaweza ukajiuliza, hawa wazalendo kampuni zao hazijui kuomba kazi, hawana utaalamu wa kufanya au tatizo liko wapi,” amesema Magufuli amesema wakati mwingine hata miradi ya ndani midogo kabisa ambayo alidhani kampuni za ndani zitaomba hazifanyi hivyo.
“Lakini wakati mwingine kupata zabuni mmekuwa mkishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali, bado ndani ya serikali kuna watendaji wasio waadilifu na ndiyo maana wakati mwingine makadirio ya fedha inayowekwa kwenye miradi inakuwa iko juu sana.” “Kukosa ujuzi wa kusimamia miradi kwa baadhi ya wakandarasi wa ndani imekuwa ikichangia baadhi yao kushindwa kukamilisha miradi kwa wakati, kutekeleza miradi chini ya kiwango na gharama zao kuwa juu sana,” amesema
Rais wa Tanzania, John Magufuli ametaja baadhi ya sababu zinazofanya wakandarasi wa ndani kushindwa kupewa miradi mikubwa ili kuitekeleza.
Miongoni mwa sababu hizo ni kukosa umoja na ushirikiano kati yao, kuendeleza vitendo vya rushwa, wakandarasi kuwa wazito kuomba zabuni ya kutekeleza miradi mikubwa inayotangazwa nchini na wengine wamekuwa wakishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali kuomba zabuni.
Magufuli amebainisha hayo leo Jumatano ya Septemba 4, 2019 katika mkutano uliowakutanisha watumishi wa bodi tatu zilizo chini ya wizara hiyo ikiwemo, Bodi ya usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) jijini Dar es Salaam.
Amesema mwaka jana nakumbuka tulitangaza mradi wa barabara ya kutoka Chamwino kwenda mjini Dodoma na nilitegemea kabisa kilomita 20 zitaombwa na kampuni za wazalendo wala hawakuomba. “Kuna miradi mingine midogo tu ya kuongeza mita 500 kama ile ya uwanja wa Dodoma, wazalendo hawakuomba, ninaweza nikataja miradi mingi na hapa unaweza ukajiuliza, hawa wazalendo kampuni zao hazijui kuomba kazi, hawana utaalamu wa kufanya au tatizo liko wapi,” amesema Magufuli amesema wakati mwingine hata miradi ya ndani midogo kabisa ambayo alidhani kampuni za ndani zitaomba hazifanyi hivyo.
“Lakini wakati mwingine kupata zabuni mmekuwa mkishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali, bado ndani ya serikali kuna watendaji wasio waadilifu na ndiyo maana wakati mwingine makadirio ya fedha inayowekwa kwenye miradi inakuwa iko juu sana.” “Kukosa ujuzi wa kusimamia miradi kwa baadhi ya wakandarasi wa ndani imekuwa ikichangia baadhi yao kushindwa kukamilisha miradi kwa wakati, kutekeleza miradi chini ya kiwango na gharama zao kuwa juu sana,” amesema
==============
Rais wa Tanzania, John Magufuli ametaja baadhi ya sababu zinazofanya wakandarasi wa ndani kushindwa kupewa miradi mikubwa ili kuitekeleza.
Miongoni mwa sababu hizo ni kukosa umoja na ushirikiano kati yao, kuendeleza vitendo vya rushwa, wakandarasi kuwa wazito kuomba zabuni ya kutekeleza miradi mikubwa inayotangazwa nchini na wengine wamekuwa wakishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali kuomba zabuni.
Magufuli amebainisha hayo leo Jumatano ya Septemba 4, 2019 katika mkutano uliowakutanisha watumishi wa bodi tatu zilizo chini ya wizara hiyo ikiwemo, Bodi ya usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) jijini Dar es Salaam.
Amesema mwaka jana nakumbuka tulitangaza mradi wa barabara ya kutoka Chamwino kwenda mjini Dodoma na nilitegemea kabisa kilomita 20 zitaombwa na kampuni za wazalendo wala hawakuomba. “Kuna miradi mingine midogo tu ya kuongeza mita 500 kama ile ya uwanja wa Dodoma, wazalendo hawakuomba, ninaweza nikataja miradi mingi na hapa unaweza ukajiuliza, hawa wazalendo kampuni zao hazijui kuomba kazi, hawana utaalamu wa kufanya au tatizo liko wapi,” amesema Magufuli amesema wakati mwingine hata miradi ya ndani midogo kabisa ambayo alidhani kampuni za ndani zitaomba hazifanyi hivyo.
“Lakini wakati mwingine kupata zabuni mmekuwa mkishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali, bado ndani ya serikali kuna watendaji wasio waadilifu na ndiyo maana wakati mwingine makadirio ya fedha inayowekwa kwenye miradi inakuwa iko juu sana.” “Kukosa ujuzi wa kusimamia miradi kwa baadhi ya wakandarasi wa ndani imekuwa ikichangia baadhi yao kushindwa kukamilisha miradi kwa wakati, kutekeleza miradi chini ya kiwango na gharama zao kuwa juu sana,” amesema
Rais wa Tanzania, John Magufuli ametaja baadhi ya sababu zinazofanya wakandarasi wa ndani kushindwa kupewa miradi mikubwa ili kuitekeleza.
Miongoni mwa sababu hizo ni kukosa umoja na ushirikiano kati yao, kuendeleza vitendo vya rushwa, wakandarasi kuwa wazito kuomba zabuni ya kutekeleza miradi mikubwa inayotangazwa nchini na wengine wamekuwa wakishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali kuomba zabuni.
Magufuli amebainisha hayo leo Jumatano ya Septemba 4, 2019 katika mkutano uliowakutanisha watumishi wa bodi tatu zilizo chini ya wizara hiyo ikiwemo, Bodi ya usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) jijini Dar es Salaam.
Amesema mwaka jana nakumbuka tulitangaza mradi wa barabara ya kutoka Chamwino kwenda mjini Dodoma na nilitegemea kabisa kilomita 20 zitaombwa na kampuni za wazalendo wala hawakuomba. “Kuna miradi mingine midogo tu ya kuongeza mita 500 kama ile ya uwanja wa Dodoma, wazalendo hawakuomba, ninaweza nikataja miradi mingi na hapa unaweza ukajiuliza, hawa wazalendo kampuni zao hazijui kuomba kazi, hawana utaalamu wa kufanya au tatizo liko wapi,” amesema Magufuli amesema wakati mwingine hata miradi ya ndani midogo kabisa ambayo alidhani kampuni za ndani zitaomba hazifanyi hivyo.
“Lakini wakati mwingine kupata zabuni mmekuwa mkishirikiana na wafanyakazi wasio waadilifu wa serikali, bado ndani ya serikali kuna watendaji wasio waadilifu na ndiyo maana wakati mwingine makadirio ya fedha inayowekwa kwenye miradi inakuwa iko juu sana.” “Kukosa ujuzi wa kusimamia miradi kwa baadhi ya wakandarasi wa ndani imekuwa ikichangia baadhi yao kushindwa kukamilisha miradi kwa wakati, kutekeleza miradi chini ya kiwango na gharama zao kuwa juu sana,” amesema