DAR: Rais Magufuli amuapisha Bi. Anna Mghwira kuwa RC Kilimanjaro. Akabidhiwa Ilani ya CCM...

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,491
54,884
KUTOKA IKULU: Rais Magufuli kumuapisha RC mteule wa Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira leo asubuhi saa 3:30 Ikulu jijini Dar.

a67253be45215bee7dd7f00c5aa7a352.jpg


=======

UPDATE:

IKULU, DAR: Rais Magufuli ameshamuapisha Mkuu mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mama Anna Elisha Mghwira.



416cf765d38080d0be1e1ec9aea4779f.jpg

f360c959-3da8-418b-b64b-4ba053401b5b.jpg

unnamed (5).jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira Ikulu jijini Dar es Salaam.
18c32f372b0e7bd7b233bdefa1f70036.jpg

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo akimkabidhi Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira huku Rais Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapi pamoja na wakuuu wa Wilaya za Ubungo na Ilala wakipiga makofi. Picha na IKULU

HISTORIA YAKE

Bi. Anna Mghwira ni mwenyekiti wa kitaifa wa chama kipya cha siasa, ACT – Wazalendo. Alizaliwa tarehe 23 Januari 1959 katika hospitali ya mkoa wa Singida, Kata ya Mungumaji, Kitongoji cha Irao manispaa ya Singida Mjini. (Mwezi Januari mwaka huu ametimiza miaka 56).

Baba mzazi wa Anna alikuwa diwani na kiongozi wa TANU kabla ya CCM hadi mwaka 1985, mama yake alijishughulisha na kilimo na ufugaji na wazazi hawa kwa ujumla walijipatia watoto tisa, akiwemo Bi. Anna.

Bi. Anna Mgwira alianza safari ya kielimu katika shule ya msingi “Nyerere Road” mwaka 1968 – 1974 akaendelea na elimu ya sekondari kwenye Shule ya Ufundi Ihanja kati ya mwaka 1975 – 1978 kabla ya kuhitimisha masomo ya juu ya Sekondari (Kidato cha V na VI) Lutheran Junior Seminary kati ya mwaka 1979 – 1981.

Anna aliendelea na masomo ya Chuo Kikuu mwaka 1982 baada ya kujiunga Chuo Kikuu cha Thiolojia (Chuo Kikuu cha Tumaini) na kuhitimu shahada ya Thiolojia mwaka 1986.

Mwaka huohuo 1986 alijiunga Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam akitafuta shahada ya Sheria na akaimaliza na kutunukiwa mwaka 1986.

Kati ya mwaka 1987 – 1998, Bi Anna aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa, akifanya kazi ndani na nje ya nchi na kupata uzoefu mkubwa sana.

Safari ya Elimu ya Bi. Anna ilikamilikia Chuo Kikuu cha Essex nchini Uingereza ambako alianza shahada ya uzamili ya sheria (LLM) mwaka 1999 na kutunukiwa mwaka 2000.

Licha ya kuwa mwanasheria na mtheologia aliyebobea, pia amefanya kazi za maendeleo kwa muda mrefu na ana uzoefu katika uendeshaji wa serikali za mitaa, uzoefu wa utumishi katika mashirka ya kimataifa, kitaifa na mashirika ya dini ambamo amejihusisha na masuala ya wanawake, watoto, wakimbizi, utawala na haki za binadamu.

Anna ana historia ya kupenda siasa, masuala ya jamii na michakato ya maendeleo kama inavyojidhihirisha katika maandiko yake mbalimbali katika majarida na magazeti ya hapa ndani ya nchi.

Alianza siasa tangu wakati wa TANU akiwa ni mwanachama wa Umoja wa Vijana wa Tanu (Tanu Youth League) na aliwahi kushinda tuzo mbalimbali kutokana na ushiriki wa juu katika TANU lakini baadaye ilipoanzishwa CCM alipunguza ushiriki wake ili ajipe muda katika masomo na baadaye ndoa na malezi ya watoto.

Kwa kipindi kirefu hakuwa anajihusisha na siasa hadi alivyoamua kujiunga na CHADEMA mwaka 2009 ambako alishika nafasi mbili tu za Uenyekiti wa baraza la wanawake ngazi ya wilaya na Katibu wa Baraza la wanawake Mkoa.

Mwezi Machi 2015 alijiunga rasmi na chama cha ACT – Wazalendo na katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa chama hicho, yeye ndiye akachaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza wa ACT.

Bi. Anna aliolewa na Shedrack Maghwiya tangu mwaka 1982 na walibahatika kupata watoto 3 wa kiume: Fadhili, Peter na Elisha. Hata hivyo kwa bahati mbaya, mume wake hivi sasa ni marehemu.

MBIO ZA UBUNGE
Bi. Anna Mghwira alijitosa katika mbio za ubunge kwa mara ya kwanza mwezi Januari 2012 baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutangaza uchaguzi mdogo katika jimbo la Arumeru Mashariki baada ya kifo cha Solomon Sumari.

Anna alishiriki kura ya maoni ndani ya CHADEMA akihitaji kupewa ridhaa, hata hivyo chama hicho kilimpitisha Joshua Nassari (Josh) na Bi. Anna alikuwa na kazi ya kuendelea kumuunga mkono hadi ushindi ulipotangazwa kwa chama hicho.

Pia, amewahi kugombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki, kupitia CHADEMA japokuwa hakuchaguliwa kushikilia wadhifa huo.

Mwaka 2015 aligombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha ACT Wazalendo.
 
Hivi kadi ya act amerudisha?
Hivi ikitokea serikali inafanya kitu tofauti na kile kilichomo kwenye ilani ya act.Huyu mama atapinga kweli?
 
Ampe na kadi ya ccm
Kadi ya CCM anayo si umesikia alikuwa mwanachama toka TANU.
KUTOKA IKULU: Rais Magufuli kumuapisha RC mteule wa Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira leo asubuhi saa 3:30 Ikulu jijini Dar.
a67253be45215bee7dd7f00c5aa7a352.jpg

HISTORIA YAKE

Bi. Anna Mghwira ni mwenyekiti wa kitaifa wa chama kipya cha siasa, ACT – Wazalendo. Alizaliwa tarehe 23 Januari 1959 katika hospitali ya mkoa wa Singida, Kata ya Mungumaji, Kitongoji cha Irao manispaa ya Singida Mjini. (Mwezi Januari mwaka huu ametimiza miaka 56).

Baba mzazi wa Anna alikuwa diwani na kiongozi wa TANU kabla ya CCM hadi mwaka 1985, mama yake alijishughulisha na kilimo na ufugaji na wazazi hawa kwa ujumla walijipatia watoto tisa, akiwemo Bi. Anna.

Bi. Anna Mgwira alianza safari ya kielimu katika shule ya msingi “Nyerere Road” mwaka 1968 – 1974 akaendelea na elimu ya sekondari kwenye Shule ya Ufundi Ihanja kati ya mwaka 1975 – 1978 kabla ya kuhitimisha masomo ya juu ya Sekondari (Kidato cha V na VI) Lutheran Junior Seminary kati ya mwaka 1979 – 1981.

Anna aliendelea na masomo ya Chuo Kikuu mwaka 1982 baada ya kujiunga Chuo Kikuu cha Thiolojia (Chuo Kikuu cha Tumaini) na kuhitimu shahada ya Thiolojia mwaka 1986.

Mwaka huohuo 1986 alijiunga Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam akitafuta shahada ya Sheria na akaimaliza na kutunukiwa mwaka 1986.

Kati ya mwaka 1987 – 1998, Bi Anna aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa, akifanya kazi ndani na nje ya nchi na kupata uzoefu mkubwa sana.

Safari ya Elimu ya Bi. Anna ilikamilikia Chuo Kikuu cha Essex nchini Uingereza ambako alianza shahada ya uzamili ya sheria (LLM) mwaka 1999 na kutunukiwa mwaka 2000.

Licha ya kuwa mwanasheria na mtheologia aliyebobea, pia amefanya kazi za maendeleo kwa muda mrefu na ana uzoefu katika uendeshaji wa serikali za mitaa, uzoefu wa utumishi katika mashirka ya kimataifa, kitaifa na mashirika ya dini ambamo amejihusisha na masuala ya wanawake, watoto, wakimbizi, utawala na haki za binadamu.

Anna ana historia ya kupenda siasa, masuala ya jamii na michakato ya maendeleo kama inavyojidhihirisha katika maandiko yake mbalimbali katika majarida na magazeti ya hapa ndani ya nchi.

Alianza siasa tangu wakati wa TANU akiwa ni mwanachama wa Umoja wa Vijana wa Tanu (Tanu Youth League) na aliwahi kushinda tuzo mbalimbali kutokana na ushiriki wa juu katika TANU lakini baadaye ilipoanzishwa CCM alipunguza ushiriki wake ili ajipe muda katika masomo na baadaye ndoa na malezi ya watoto.

Kwa kipindi kirefu hakuwa anajihusisha na siasa hadi alivyoamua kujiunga na CHADEMA mwaka 2009 ambako alishika nafasi mbili tu za Uenyekiti wa baraza la wanawake ngazi ya wilaya na Katibu wa Baraza la wanawake Mkoa.

Mwezi Machi 2015 alijiunga rasmi na chama cha ACT – Wazalendo na katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa chama hicho, yeye ndiye akachaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza wa ACT.

Bi. Anna aliolewa na Shedrack Maghwiya tangu mwaka 1982 na walibahatika kupata watoto 3 wa kiume: Fadhili, Peter na Elisha. Hata hivyo kwa bahati mbaya, mume wake hivi sasa ni marehemu.

MBIO ZA UBUNGE
Bi. Anna Mghwira alijitosa katika mbio za ubunge kwa mara ya kwanza mwezi Januari 2012 baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutangaza uchaguzi mdogo katika jimbo la Arumeru Mashariki baada ya kifo cha Solomon Sumari.

Anna alishiriki kura ya maoni ndani ya CHADEMA akihitaji kupewa ridhaa, hata hivyo chama hicho kilimpitisha Joshua Nassari (Josh) na Bi. Anna alikuwa na kazi ya kuendelea kumuunga mkono hadi ushindi ulipotangazwa kwa chama hicho.

Pia, amewahi kugombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki, kupitia CHADEMA japokuwa hakuchaguliwa kushikilia wadhifa huo.

Mwaka 2015 aligombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha ACT Wazalendo.
 
KUTOKA IKULU: Rais Magufuli kumuapisha RC mteule wa Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira leo asubuhi saa 3:30 Ikulu jijini Dar.
a67253be45215bee7dd7f00c5aa7a352.jpg

HISTORIA YAKE

Bi. Anna Mghwira ni mwenyekiti wa kitaifa wa chama kipya cha siasa, ACT – Wazalendo. Alizaliwa tarehe 23 Januari 1959 katika hospitali ya mkoa wa Singida, Kata ya Mungumaji, Kitongoji cha Irao manispaa ya Singida Mjini. (Mwezi Januari mwaka huu ametimiza miaka 56).

Baba mzazi wa Anna alikuwa diwani na kiongozi wa TANU kabla ya CCM hadi mwaka 1985, mama yake alijishughulisha na kilimo na ufugaji na wazazi hawa kwa ujumla walijipatia watoto tisa, akiwemo Bi. Anna.

Bi. Anna Mgwira alianza safari ya kielimu katika shule ya msingi “Nyerere Road” mwaka 1968 – 1974 akaendelea na elimu ya sekondari kwenye Shule ya Ufundi Ihanja kati ya mwaka 1975 – 1978 kabla ya kuhitimisha masomo ya juu ya Sekondari (Kidato cha V na VI) Lutheran Junior Seminary kati ya mwaka 1979 – 1981.

Anna aliendelea na masomo ya Chuo Kikuu mwaka 1982 baada ya kujiunga Chuo Kikuu cha Thiolojia (Chuo Kikuu cha Tumaini) na kuhitimu shahada ya Thiolojia mwaka 1986.

Mwaka huohuo 1986 alijiunga Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam akitafuta shahada ya Sheria na akaimaliza na kutunukiwa mwaka 1986.

Kati ya mwaka 1987 – 1998, Bi Anna aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa, akifanya kazi ndani na nje ya nchi na kupata uzoefu mkubwa sana.

Safari ya Elimu ya Bi. Anna ilikamilikia Chuo Kikuu cha Essex nchini Uingereza ambako alianza shahada ya uzamili ya sheria (LLM) mwaka 1999 na kutunukiwa mwaka 2000.

Licha ya kuwa mwanasheria na mtheologia aliyebobea, pia amefanya kazi za maendeleo kwa muda mrefu na ana uzoefu katika uendeshaji wa serikali za mitaa, uzoefu wa utumishi katika mashirka ya kimataifa, kitaifa na mashirika ya dini ambamo amejihusisha na masuala ya wanawake, watoto, wakimbizi, utawala na haki za binadamu.

Anna ana historia ya kupenda siasa, masuala ya jamii na michakato ya maendeleo kama inavyojidhihirisha katika maandiko yake mbalimbali katika majarida na magazeti ya hapa ndani ya nchi.

Alianza siasa tangu wakati wa TANU akiwa ni mwanachama wa Umoja wa Vijana wa Tanu (Tanu Youth League) na aliwahi kushinda tuzo mbalimbali kutokana na ushiriki wa juu katika TANU lakini baadaye ilipoanzishwa CCM alipunguza ushiriki wake ili ajipe muda katika masomo na baadaye ndoa na malezi ya watoto.

Kwa kipindi kirefu hakuwa anajihusisha na siasa hadi alivyoamua kujiunga na CHADEMA mwaka 2009 ambako alishika nafasi mbili tu za Uenyekiti wa baraza la wanawake ngazi ya wilaya na Katibu wa Baraza la wanawake Mkoa.

Mwezi Machi 2015 alijiunga rasmi na chama cha ACT – Wazalendo na katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa chama hicho, yeye ndiye akachaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza wa ACT.

Bi. Anna aliolewa na Shedrack Maghwiya tangu mwaka 1982 na walibahatika kupata watoto 3 wa kiume: Fadhili, Peter na Elisha. Hata hivyo kwa bahati mbaya, mume wake hivi sasa ni marehemu.

MBIO ZA UBUNGE
Bi. Anna Mghwira alijitosa katika mbio za ubunge kwa mara ya kwanza mwezi Januari 2012 baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutangaza uchaguzi mdogo katika jimbo la Arumeru Mashariki baada ya kifo cha Solomon Sumari.

Anna alishiriki kura ya maoni ndani ya CHADEMA akihitaji kupewa ridhaa, hata hivyo chama hicho kilimpitisha Joshua Nassari (Josh) na Bi. Anna alikuwa na kazi ya kuendelea kumuunga mkono hadi ushindi ulipotangazwa kwa chama hicho.

Pia, amewahi kugombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki, kupitia CHADEMA japokuwa hakuchaguliwa kushikilia wadhifa huo.

Mwaka 2015 aligombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha ACT Wazalendo.

Kwa aliyeandaa hii historia ya Anna kuna jambo linanipa utata kuhusu kipengele cha elimu yake! "Alihitimu Chuo Kikuu cha Tumaini mwaka 1986 na kutunukiwa shahada ya Teolojia! Akajiunga na Chuo Kikuu Dsm mwaka huo huo 1986 na kuhitimu kwaka huo huo 1986 na kutunikiwa shahada ya sheria" !!! Kwa mifumo yetu ya elimu Tanzania hili limewezekanaje? Au mwandishi kachanganya miaka?
 
Kwa aliyeandaa hii historia ya Anna kuna jambo linanipa utata kuhusu kipengele cha elimu yake! "Alihitimu Chuo Kikuu cha Tumaini mwaka 1986 na kutunukiwa shahada ya Teolojia! Akajiunga na Chuo Kikuu Dsm mwaka huo huo 1986 na kuhitimu kwaka huo huo 1986 na kutunikiwa shahada ya sheria" !!! Kwa mifumo yetu ya elimu Tanzania hili limewezekanaje? Au mwandishi kachanganya miaka?

Na mimi nimejiuliza hilo swali jibu sijalipata.
 
Back
Top Bottom