Dar: Polisi wamuua mtuhumiwa wa ujambazi

Tatizo wauza madawa ya kulevya sio watu wachovu, ni watu wakubwa na wenye heshima kubwa kwenye jamii yetu. Yaani hata wakitajwa watu mtashika midomo kwa mshangao na kwasababu wanaheshimika sana hamta amini kama kweli ni wauza madawa badala yake mtaanza kuwatetea na kisha kumshambulia yule aliye wataja kuwa ndio mtu mbaya.
Wanaharakati wataibuka kila kona kisa tu katajwa fulani na hata Kama akikamatwa nayo bado watu watakuja tu nakusema kuwa kabambikiwa kwasababu ya chuki binafsi.

Wauza madawa ni hao hao wafanya biashara wakubwa ambao wakitajwa huto amini, wachungaji, mashekh, wasanii, wanasiasa wakubwa n.k

Utawaambia watu mchungaji wao ni muuza madawa nani atakuamini mfano ( ni mfano tu nisieleweke vibaya) umtaje Mtu Kama Mwamposa, Askofu Mwamakula n.k we unadhani waumini wake maelufu watakuamini kweli?

Umtaje MO eti anauza madawa nani atakusikiliza wana Simba wote watakuvamia kumbuka kilicho tokea kwa Manji.

Umtaje mwanasiasa Kama Zitto, Mbowe, Makamba, Nape n.k eti wanauza madawa weee hiyo kesi hutoiweza utapopolewa mawe nchi nzima hakuna atakae kuamini.

Ila ukweli unabaki kuwa ukweli kwamba hakuna mchovu mlalahoi wa tandale kwa mtogole mwenyewe uwezo wa kusafirisha madawa kutoka Colombia kuyaleta bongo hayupo. Wanao fanya hivyo ni watu wenye pesa zao, wafanya biashara, watumishi wa mungu tunao waamini, viongozi wakisiasa na wasanii wenye majina makubwa ambao ni vipenzi vya mamia ya watu.
hakuna mkubwa wala mdogo mbele ya sheria, jambo la msingi uwe na uhakika na ushahidi sio kumsingizia mtu kwa chuki zako binafsi au umesikia kwenye kijiwe cha kahawa.

ukitoa taarifa za uhakika na vyombo pia vina chunguza na kisha wakijiridhisha bila kujali awe mkubwa au awe na fedha nyingi au vyovyote vile atakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Tanzania bila ya Madawa ya kulevya na Majambazi inawezekana.
Tuwafichue wauzaji na majambazi
 
hakuna mkubwa wala mdogo mbele ya sheria, jambo la msingi uwe na uhakika na ushahidi sio kumsingizia mtu kwa chuki zako binafsi au umesikia kwenye kijiwe cha kahawa.

ukitoa taarifa za uhakika na vyombo pia vina chunguza na kisha wakijiridhisha bila kujali awe mkubwa au awe na fedha nyingi au vyovyote vile atakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Tanzania bila ya Madawa ya kulevya na Majambazi inawezekana.
Tuwafichue wauzaji na majambazi
Sawa Kaka wacha tuendelee na hiyo nadharia unayo iamini hivo hivo huku watu wanashusha tani mbili za madawa.😂.
 
Tuhuma alafu Kifo ?

Ila nawapa benefit of Doubt itakuwa kifo ilikuwa bahati mbaya.... Ingawa heading inaleta ukakasi
 
Ndio maaana tuna kikosi maalum cha kupambana na wauza madawa na pia uzuri ni kwamba vita ya kupambana na wauza madawa ya kulevya inawashirikisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama, naamini endapo tutashirikiana basi wauza madawa ya kulevya nchini Tanzania hawawezi kuwa na guvu zaidi ya Serikali.
Hawana nguvu zaidi ya serikali ila wanasapoti ya watu wa serikali kubwa kubwa duniani.
 
Nipo Tabora,nadhani huku kuna chuo cha majambazi na vibaka,wanaiba mpaka mavi yaliofungwa
Mdogo wangu hebu tuache Mungu wako siku moja moja enzi za akina isa Kandege,surambaya,Mohamed simba na wengine haukuwepo hiyo ndio ilikua the siku hizi imebaki hadithi kama ya akina firauni na akina ndugu na wengine tabora ya sasa ni ya kijani
 
Majambazi na wauza madawa tunaishi nao ktk meneo yetu, mitaa yetu tuwafichue ili tuwe salama, hata kama unanufaika na pato la Jambazi au muuza madawa endapo tu utakapo toa taarifa za siri ndipo utakuwa salama endapo utawaficha kwa kudhani unalinda posho yako jua umekwisha.

kinachoendelea sasa ni kutokomeza Majambazi na masalia yake, pia Kutokomeza wauza madawa ya kulevya na maslia yake.
 
Enzi za gewe kulikuwa na jambaz alikuwa anasumbua sana alikuwa anafamika
Dar break....jamaa alitisha ila gewe alipokuwa rpc dsm,alideal naye vilivyo
Majambaz wa sahv wako kama wadokozi
Zamani jambaz linatoka tabora huko jitu katili
Roho kwatu

Ova
Kina Black september
 
Kwa Mujibu wa Amiri Jeshi Mkuu Mama Samia amesema kuwa kipimo cha RPC, OCD, CID kitakuwa ni kufanikiwa kutokomeza Ujambazi na uhalifu mwengine ktk maeneo yao husika. lkn vilevile kipimo hicho kitatimika kwa Ma RC na ma DC.

lkn pia kwa kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya.
 
Back
Top Bottom